Tanzania ina ungana na dunia kusherehekea siku ya kuzaliwa mkombozi wa ulimwengu. Hapa ndipo mtoto Yesu alipozaliwa katika zizi la ng'ombe Bethlehemu.
Kutoka kushoto kwenda kulia ni Kris Simbaya (Jr) na Ken Simbaya (Jr) wakiwa katika pozi ya picha maeneo ya Peramiho Songea, Mkoa wa Ruvuma.
Kutoka kushoto kwenda kulia ni Friday Simbaya, Kris Simbaya, Ken Simbaya na Lina Changwa wakiwa katika picha ya pamoja siku ya Krismas.
Mama Simbaya ambaye ni mke mpendwa wa mmiliki wa blog hii akiwa na watoto wake walipokuwa wa kisherekea siku kuu ya Krismas leo jioni.
Pamlomo24 is essentially a digital news platform that shares different types of news updates — social, political, economic, sports, entertainment, and community stories. From the context you’ve given, it is based in Iringa, Tanzania, and functions mainly as an online outlet (likely through social media such as Facebook, YouTube, or other channels) where audiences can get real-time updates.
Saturday, 25 December 2010
ZAWADI YA MKESHA WA NOELI
Muuguzi wa Zamu wa St. Joseph's Mission Hospital Peramiho akiwa anawaangalia watoto ambao walizaliwa kabla ya umri yaani 'Premature babies' katika Chumba cha Joto 'Premature Unit or Incubator Room' Jumamosi kuangalia kama wanaendelea vizuri lakini hawakuzaliwa kwenye Mkesha wa Krismasi wako wanne.
Na Friday Simbaya,
Peramiho
JUMLA ya watoto 13 wamezaliwa, wakiwemo wakike tisa na wakiume wanne katika Hospitali ya Mission ya Mtakatifu Joseph Peramiho mkoani Ruvuma katika Mkesha wa Noeli (Krismasi) usiku wa kuamkia LEO.
Akiongea na BLOG HII, Muuguzi wa Zamu (Nursing Office in charge), Bi. Sirah Nchimbi alisema kwamba watoto wote walizaliwa kwa njia ya kawaida isipokuwa watoto watatu ndiyo waliozaliwa kwa njia ya upasuaji (surgical operation) lakini hali zao zinaendelea vizuri pamoja na mama zao.
“Watoto hao walizaliwa na uzito wa kawaida, hali zao zinaendelea vizuri sana pamoja mama zao. Wakina mama wengine wameruhusiwa baada ya kujifungua lakini wamebaki wale walioji fungua kwa opresheni ambao wako katika uangalizi maalumu,” alisema muunguzi wa zamu.
Aidha, alisema kuwa yapo matatizo wanayokubiliana nayo kama vile kina mama kutofika mapema hospitalini pindi wapatapo uchungu wa uzazi kunako sababisha wengi wao kinamama kujifungulia njiani kabla ya kufika hosptali na wengi wao hujifungua watoto waliokufa katokana na kuchelewa kufika hospitali mapema.
Tatizo jingine ni kwamba wa kinamama walio wengi maeneo haya hutumia dawa ya mitishamba kuongeza uchungu wa kujifungua kabla ya kuletwa hospitali, matokeo yake wengi wao kina mama wanashindwa kujifungua kwa njia ya kawaida (normal delivery) au hujifungua watoto waliokufa kutokana na dawa hizo wanazozitumia.
“Yaani ni tatizo kubwa sana kwa kina mama wanaokuja kujifungua hapa kutokana kutumia dawa za kienyeji za uchungu lakini huwatunawapa elimu wanapofika na kuwapa ushauri wakina mama wajawazito waweze kufika hospitalini mapema na kuacha kutumia dawa hizo za kuongeza uchungu, ambapo mara nyingi hutiwa kwenye chain a uji,” alisema muunguzi huyo wa zamu.
Lakini pamoja na hayo, hakuweza kuelezea ni dawa ya aina gani mara nyingi wa kina mama hao hutumia kama dawa ya kuongeza uchungu, na kuongeza kuwa wanatumia mizizi Fulani Fulani ambayo hakutaja aina gani ya mizizi hiyo.
Mwisho
Subscribe to:
Posts (Atom)
Iringa Regional Commissioner Calls On Kilolo Leaders To Strictly Supervise Government Projects
IRINGA – The Iringa Regional Commissioner, Kheri James, has urged leaders of the Kilolo District Council—particularly those in the secondary...

-
KIKUNDI cha Upendo ni kikundi cha kina mama 20 walioamua kujiunga kwa pamoja na kuanz...
-
Peter Mbata's the Deputy Headmaster and Amon Chota (academic master). Headmaster of Ifunda Technical School, Mpambwe Paul ...
-
Iringa. Mgombea Ubunge wa Jimbo la Kalenga kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), ameomba wananchi wa kata ya Lyamgungwe, Wilaya ya Iringa, kum...