Tuesday, 23 September 2025

Mgombea Ubunge Kalenga Aomba Ridhaa ya Wananchi, Aahidi Kuboresha Huduma za Afya




Iringa. Mgombea Ubunge wa Jimbo la Kalenga kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), ameomba wananchi wa kata ya Lyamgungwe, Wilaya ya Iringa, kumpa tena ridhaa ya kuendelea kulitumikia jimbo hilo katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 29, mwaka huu.

Akizungumza na wananchi na wanachama wa CCM wakati wa kampeni, mgombea huyo alisema kipindi cha miaka mitano iliyopita kilikuwa cha kujifunza, huku akieleza kuwa endapo atapewa nafasi nyingine, ataendeleza miradi ya maendeleo aliyoianzisha.

Alibainisha kuwa moja ya changamoto zinazowakabili wananchi ni ukosefu wa vyumba vya kuhifadhi maiti katika vituo vya afya, na kuahidi kushirikiana na Serikali kuhakikisha kila kituo kinakuwa na huduma hiyo ili kupunguza gharama za kupeleka maiti katika Hospitali ya Tosamaganga.

Aidha, alitaja mafanikio aliyoyapata katika kipindi chake cha ubunge ikiwemo kufanikisha ujenzi wa barabara ya lami kutoka Mgama, hatua ambayo imesaidia kurahisisha usafirishaji wa mazao na huduma muhimu.

“Chama Cha Mapinduzi ndicho chama pekee chenye uwezo wa kudumisha amani na usalama wa nchi hii. Tuendelee kukiamini na kukipa kura zetu ili maendeleo yawe endelevu,” alisema.

 


Iringa. Mgombea Ubunge wa Jimbo la Kalenga kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), ameomba wananchi wa kata ya Lyamgungwe, Wilaya ya Iringa, kumpa tena ridhaa ya kuendelea kulitumikia jimbo hilo katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 29, mwaka huu.

Akizungumza na wananchi na wanachama wa CCM wakati wa kampeni, mgombea huyo alisema kipindi cha miaka mitano iliyopita kilikuwa cha kujifunza, huku akieleza kuwa endapo atapewa nafasi nyingine, ataendeleza miradi ya maendeleo aliyoianzisha.

Alibainisha kuwa moja ya changamoto zinazowakabili wananchi ni ukosefu wa vyumba vya kuhifadhi maiti katika vituo vya afya, na kuahidi kushirikiana na Serikali kuhakikisha kila kituo kinakuwa na huduma hiyo ili kupunguza gharama za kupeleka maiti katika Hospitali ya Tosamaganga.

Aidha, alitaja mafanikio aliyoyapata katika kipindi chake cha ubunge ikiwemo kufanikisha ujenzi wa barabara ya lami kutoka Mgama, hatua ambayo imesaidia kurahisisha usafirishaji wa mazao na huduma muhimu.

“Chama Cha Mapinduzi ndicho chama pekee chenye uwezo wa kudumisha amani na usalama wa nchi hii. Tuendelee kukiamini na kukipa kura zetu ili maendeleo yawe endelevu,” alisema.

 



 

Iringa Regional Commissioner Calls On Kilolo Leaders To Strictly Supervise Government Projects

IRINGA – The Iringa Regional Commissioner, Kheri James, has urged leaders of the Kilolo District Council—particularly those in the secondary...