Mlinzi wa kampuni hiyo (wa pili kutoka kulia) ambaye hakutaka kutaja jina lake akiongea na waandishi hivi karibuni ambapo alisema kuwa kampuni hiyo ina jumla ya walinzi watatu, lakini wana miezi miwili na siku 20 bila malipo.
Mpishi Mkuu wa Kampuni ya ujenzi ya Canopies International, Agape Mgongola akiendelea na kazi yakuwapikia wafanyakazi wa kampuni hiyo bila malipo kwa miezi minne sasa.
Na MARTHIAS KANALI,
Iringa
Wakazi wa Kitongoji cha
Msosa mkoani Iringa wameilalamikia kampuni ya Canopies International (T) Ltd kutoka
Mwananyamala jijini Dar es Salaam ambayo inajishugulisha na ujenzi wa barabara
kutoka njia panda ya Kalenga kuelekea Tosamaganga kutokana na kushindwa
kuwalipa fedha zao takribani miezi minne sasa.