Na Friday Simbaya, Iringa | | | ||
ASKARI polisi amefariki dunia baada ya kujipiga risasi mbili chini ya kidevu, kifo kinachosadikiwa kuwa kinahusiana na wivu wa kimapenzi baina yake na askari mwingine. Kamanda wa polisi mkoa wa Iringa, Evarist Mangalla alisema askari huyo alijipiga na kufa papo hapo Julai 8, mwaka huu saa 3:00 usiku katika eneo la makazi ya mkuu wa mkoa wa Iringa eneo la Gangilonga, manispaa ya Iringa. Alimataja askari huyo kuwa ni G13 Mashauri (24) ambaye kabla ya kujiua alikuwa kwenye lindo eneo la benki ya CRDB ambako aliingia lindoni saa 12:00 jioni Julai 8, mwaka huu na kutoka saa 1:30 usiku kuelekea nyumbani kwa askari wa kike. Akielezea tukio Alisema baada ya kuachana kila mmoja aliendelea na mambo yake na hadi siku ya tukio Mangalla alisema askari huyo aliondoka kwenye lindo “Baada ya kufunguliwa alimkuta Zahara amekaa na kijana mmoja aitwae Sunday Tumaini mfanyakazi wa Bayport akawatishia, ndipo askari wa kike alipiga kelele kuomba msaada, askari mwingine aliyekuwa amepanga kwenye nyumba hiyo alitoka na kusaidia”alisema kamanda huyo. Alisema askari aliyekuja kumsaidia Zahara, alimnyang’anya silaha aliyekuwa nayo Mashauri na baada ya kunyang’anywa aliondoka eneo Alisema baada ya kuzungumza nao ghafla alimnyang’anya silaha askari mwenzake na kuondoka nayo kwenda kwenye eneo alilojiulia kwa kujipiga risasi mbili chini ya kidevu. Hata hivyo Mangalla alisema kuwa taarifa za awali za kujiua kwa askari huyo zinaonyesha alijiua kutokana na wivu wa kimapenzi lakini polisi wanaendelea na uchunguzi zaidi wa tukio | ||||
|
|
|
|
|
Pamlomo24 is essentially a digital news platform that shares different types of news updates — social, political, economic, sports, entertainment, and community stories. From the context you’ve given, it is based in Iringa, Tanzania, and functions mainly as an online outlet (likely through social media such as Facebook, YouTube, or other channels) where audiences can get real-time updates.
Saturday, 10 July 2010
ASKARI POLISI AJIUA KWA KUJIPGA RISASI
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Iringa Regional Commissioner Calls On Kilolo Leaders To Strictly Supervise Government Projects
IRINGA – The Iringa Regional Commissioner, Kheri James, has urged leaders of the Kilolo District Council—particularly those in the secondary...

-
KIKUNDI cha Upendo ni kikundi cha kina mama 20 walioamua kujiunga kwa pamoja na kuanz...
-
Peter Mbata's the Deputy Headmaster and Amon Chota (academic master). Headmaster of Ifunda Technical School, Mpambwe Paul ...
-
Iringa. Mgombea Ubunge wa Jimbo la Kalenga kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), ameomba wananchi wa kata ya Lyamgungwe, Wilaya ya Iringa, kum...
No comments:
Post a Comment