MGOMBEA kiti cha Ubunge Jimbo la Temeke kupitia tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM), Abasi Zuberi Mtemvu amewatoa wasiwasi wapangaji wa nyumba za kota zilizopo Temeke mwisho kwa kuwaeleza kuwa zoezi la kuvunjwa kwa nyumba hizo sasa limesitishwa.
Mgombea huyo alitoa kauli hiyo jana kwenye mkutano wa hadhara wa kampeni za uchaguzi uliyofanyika katika uwanja wa MjiMpya Kata ya Azimio jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa na umati wa watu.
Akifafanua zaidi kuhusu kauli yake hiyo Mtemvu alisema serikali iliyoko madarakani imejipanga kujenga majengo ya ghorofa katika eneo hilo ambapo ujenzi wake ukikamilika wapangaji wa awali wa kota watapewa umuhimu wa kwanza kufikiriwa katika kupanga kwenye maghorofa hayo.
Alisema si vyema kuanza zoezi la uvunjaji wa kota hizo bila kuzingatia usalama wa wananchi na mali zao katika kipindi cha mpango huo.
Kota hizo zilizopo eneo la Temeke mwisho zilijengwa miaka mingi iliyopita katika mfumo wa familia moja, mbili na tatu hata hivyo nyumba hizo zimeanza kuchoka na hata baadhi yake kuanza kuharibika.
Kwa upande mwingine mgombea huyo aliwataka wanawake wa jimbo hilo kujiunga pamoja na kuunda vikundi vidogo vidogo (VICOBA) ili waweze kupata misaada ya uwendelezaji wa vikundi vyao ili kuondokana na umasikini wa kipato na kuboresha familia zao.
Akizumgumzia huduma za jamii upande wa elimu alisema endapo atachaguliwa tena kuongoza jimbo hilo atahakikisha kuwa kata ya Azimio inapata sekondari ya kidato cha tana na sita.
Pamlomo24 is essentially a digital news platform that shares different types of news updates — social, political, economic, sports, entertainment, and community stories. From the context you’ve given, it is based in Iringa, Tanzania, and functions mainly as an online outlet (likely through social media such as Facebook, YouTube, or other channels) where audiences can get real-time updates.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Iringa Regional Commissioner Calls On Kilolo Leaders To Strictly Supervise Government Projects
IRINGA – The Iringa Regional Commissioner, Kheri James, has urged leaders of the Kilolo District Council—particularly those in the secondary...

-
KIKUNDI cha Upendo ni kikundi cha kina mama 20 walioamua kujiunga kwa pamoja na kuanz...
-
Peter Mbata's the Deputy Headmaster and Amon Chota (academic master). Headmaster of Ifunda Technical School, Mpambwe Paul ...
-
Iringa. Mgombea Ubunge wa Jimbo la Kalenga kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), ameomba wananchi wa kata ya Lyamgungwe, Wilaya ya Iringa, kum...
No comments:
Post a Comment