Saturday, 30 April 2011

BREAKING NEWS

Kesho ni Siku Kuu ya Wafanyakazi duniani (Mei Mosi), ambapo timu ya soka ya wafanyakazi wa misioni Peramiho itamenyana na timu ya watumishi wa serikali katika viwanja vya Peramiho wilayani Songea, mkoani Ruvuma, ikiwa ni sehemu yao ya maadhimisho ya siku ya wafanyakazi duniani. Pia timu ya wanawake ya mpira wa Pete (Netball) ya Peramiho vile vile itashuka dimbani kumenyana na timu ya wafanyakazi wa serikali katika mechi zitakazoanza Saa Kumi jioni. Mgeni Rasmi anatarajia kuwa Mbunge wa Jimbo la Peramiho, Mhe. Jenister Mhagama (CCM) akiambatana na viongozi wengine chama hicho na viongozi serikali. 

No comments:

Iringa Regional Commissioner Calls On Kilolo Leaders To Strictly Supervise Government Projects

IRINGA – The Iringa Regional Commissioner, Kheri James, has urged leaders of the Kilolo District Council—particularly those in the secondary...