Sunday, 12 February 2017
Thursday, 9 February 2017
BARAZA LA VIONGOZI WA DINI LAUNGA MKONO JITIHADA ZA MAKONDA ...
Mwenyekiti wa Baraza la Viongozi wa Dini la Kupambana na Dawa za Kulevya Tanzania, Sheikh Alhad Mussa Salum.
Mwenyekiti wa Baraza la Viongozi wa Dini la Kupambana na Dawa za Kulevya Tanzania, Sheikh Alhad Mussa Salum (kushoto), akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam leo, kuhusu baraza hilo kuunga mkono jitihada za Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda za kupambana na wanaojihusisha na dawa za kulevya. Kulia ni Katibu wa Baraza hilo, Padre John Solomon.
Baadhi ya viongozi wa dini (waliokaa), wakiwa kwenye mkutano huo. Wengine ni wanahabari.
Mkutano na wanahabari ukiendelea.
Na Dotto Mwaibale
BARAZA la Viongozi wa dini la kupambana na dawa za kulevya Tanzania ambalo liko chini ya Tume ya kupambana na dawa za kulevya limeunga mkono jitihada zinazofanywa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda za kupambana na watu mbalimbali wanaotumia dawa za kulevya.
Katika hatua nyingine baraza hilo limeiomba serikali kumuongezea ulinzi Makonda kwa kuthubutu kutaja watu wanaojihusisha kwa namna moja au nyingine na dawa hizo.
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake Dar es Salaam leo, Mwenyekiti wa Baraza hilo, Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhadi Mussa Salum ,alisema Makonda anapaswa kuongezewa ulinzi kutokana na ujasiri aliouonesha wa kuthubutu kuwataja kwa majina watu hao.
"Sisi kama baraza tunapinga vita na kulaani hatua yoyote ya kushiriki katika biashra au utimiaji wa dawa za kulevya kwa kuwa matumizi ya dawa hizo yamekuwa ni kikwazo kikubwa cha maendeleo katika nchi yetu na yanapotokea nguvu kazi ya Taifa kwa vile wahanga wakubwa wa matumizi ya dawa hizi ni vijana"alisema.
Alisema kutokana na ugumu wa kazi hiyo aliyoianzisha baraza hilo linamuombea kwa mwenyezi mungu ili ampe ulinzi wake na kinga yake na azidi kumpa moyo wa ujasiri wa kupambana na maovu yote yanayo haribu sifa ya Taifa letu na vijana kwa ujumla.
Salum alisema hivi sasa Makonda ameshanza kutengenezewa majungu, fitina na uzushi mbalimbali ili kumkatisha tamaa na aonekane mbaya kwa watanzania lakini hawatafanikiwa endapo atamtanguliza mwenyezi mungu katika mapambano hayo.
Alisema inawezekana wanaopinga au kubeza juhudi hizo ni kwa sababu tu madhara ya dawa za kulevya hayajawagusa wao na familia zao hivyo hawana uchungu na watanzania wenzao walioathirika hivyo wapuuzwe badala yake wasimame pamoja kama watanzania dhidi ya vita hiyo.
Mwenyekiti huyo wa baraza hilo alitumia fursa hiyo kuwaomba viongozi wengine waige mfano wa Makonda wa kupambana na uovu huo mkubwa ambao ni janga kwa Taifa kwani Tanzania bila dawa za kulevya inawezekana.
LADY IN RED 2017 KUTIKISA JIJI LA DAR
Ni siku chache tu! zimesalia kuikamata Tarehe 11 mwizi huu 2017, kumbuka siku hiyo ni siku pendwa ya Wanamitindo wa hapa Tz, coz wanategemea kukutatishwa kwenye Big Fashion Show ambayo hufanyika kila mwaka yaani hapa naizungumzia “Lady In Red”.
Muandaaji wa show hiyo Mama wa mitindo maarufu kama Asya Idarous Khamsin, akizungmza na wabahabari Jana Tarehe 8/2/2017 huku akiwa ameambatana na wanamitindo wengine amesema kuwa,
“Kwanza Show hii ni yakipekee pia inafaida kubwa sana kwa upcoming Designers, Lady in red huwa inatoa kipaumbele kwa upcoming Designers kuweza kuonesha kazi zao jukwaani, hivyo mwaka huu 11/2/2017 mambo yatakuwa mazuri sana ndani ya King Solomoni Hall”.
Hivyo kwa wadau wote wapenzi wa mitindo mnaombwa kuhudhuria usiku huo ili sanaa ya mitindo iweze kukua zaidi Asante.
Wanamitindo wakiwa kwenye Press ya Lady In Red 2017
Asya Idarous
Picha ya pamoja ya wanamitindo baada ya Press ya Lady In Red 2017
RC MTAKA AKABIDHI NG'OMBE KWA AJILI YA AROBAINI YA KIFO CHA MZEE KAYOMBO
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe Antony Mtaka akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili kijiji cha Misasi
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe Antony Mtaka (kulia) akiwa na Mkurugenzi wa Manispaa ya Ubungo Ndg John Lipesi Kayombo (kushoto)
Mkurugenzi wa Manispaa ya Ubungo Ndg John Lipesi Kayombo
Ng'ombe aiyetolewa na Rc Mtaka kwa ajili ya Arobaini ya Mzee Kayombo
Mwenyekiti wa Asasi ya Wazalendo na Maendeleo Tanzania (AWAMATA) Chief Mrindoko Babu Mwidadi akisaini kitabu cha wageni ishara ya ushiriki wa asasi hiyo katika msiba wa Mzee Kayombo
Mazungumzo yamenoga mara baada ya makabidhiano ya Ng'ombe
Rc Antony Mtaka Mtaka
Rc Mtaka akiwasalimu ndugu wa marehemu Mzee Kayombo mara baada ya kukabidhi Ng'ombe
MD Kayombo akiwa na ndugu na jamaa katika mazungumzo ya jioni
Na Mathias Canal, Mwanza
Ikiwa ni siku tatu zimepita tangu Marehemu Mzee Antony Raphael Kayombo kuhifadhiwa katika nyumba yake ya milele (kaburini) Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe Antony Mtaka amezuru kijijini Misasi, Wilayani Misungwi kwa ajili ya kutoa pole kwa familia ya Mzee huyo.
Rc Mtaka aliyeambatana na Mkewe wamefanya sala ya kumuombea mapumziko mema Mzee Kayombo ikiwa ni ishara ya ukamilifu wake wa haki na kheri hapa Duniani.
Pamoja na mkono wa pole kama mila za kiafrika zinavyoarifu Rc Mtaka pia ameikabidhi familia hiyo Ng'ombe kwa ajili ya Arobaini itakayofanyika kijijini hapo ikiwa ni ishara ya ukamilisho wa Msiba huo (HITMA)).
"Binafsi naamini katika matendo mema hapa Duniani, Mzee wetu ametutoka ni pigo kwa familia na kwetu sote lakini hakuna namna tuna kila sababu ya kulipokea jambo hili kama jambo la kila mmoja wetu japo halizoeleki" Aliongeza RC Mtaka
Akipokea Ng'ombe huyo na kuzungumza kwa niaba ya familia Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo Ndg John Lipesi Kayombo ambaye ni mjukuu wa marehemu Mzee Kayombo amesema kuwa kwa kuwa safari ya kifo ni ya kila mmoja hivyo familia imepokea kifo hicho kama safari ya mwisho kwa Mzee wao lakini inaendelea kumuombea ili aishi maisha ya amani huko alipo.
MD Kayombo amemshukuru Mkuu huyo wa Mkoa wa Simiyu kwa kufika na kuwasalimu waombolezaji ambao bado wapo kijijini hapo sawia na kumtakia majukumu mema katika utendaji wake ili kuhakikisha wananchi wanapata maendeleo kote nchini.
Marehemu Mzee Kayombo aliugua ugonjwa wa kibofu cha mkojo ambao ulianza ghafla tarehe 29/1/2017 na kupelekwa katika hospitali ya Misasi, Baadae hospitali ya Sekou Ture na mwishowe Hospitali ya Bugando ambapo alifanyiwa upasuaji ambapo hata hivyo hali yake iliendelea kudhoofika mpaka mauti ilipomkuta tarehe 4/2/2017 majira ya saa mbili usiku.
MUNGU AILAZE MAHALA PEMA PEPONI ROHO YA MAREHEMU MZEE ANTONY RAFAEL KAYOMBO. AMENI
Subscribe to:
Posts (Atom)
WATOTO WAITAKA SERIKALI KUTUNGA SHERIA KALI ...
Na Friday Simbaya, Mufindi Wanafunzi wa shule za msingi na sekondari wilayani Mufindi mkoani Iringa wameiomba serikali kwa kush...
-
KIKUNDI cha Upendo ni kikundi cha kina mama 20 walioamua kujiunga kwa pamoja na kuanz...
-
Peter Mbata's the Deputy Headmaster and Amon Chota (academic master). Headmaster of Ifunda Technical School, Mpambwe Paul ...
-
Habari ndugu msomaji wetu wa blog, Natumaini unaendelea vyema. Leo tutaanza kujifunza kilimo cha bora cha nyanya, na tutaanza kufahamu vit...