MGOMBEA Mwenza wa Urais kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Mohamed Gharib Bilal ataanza ziara ya kampeni za uchaguzi kwa siku nne (4) mkoani Iringa, imeelezwa leo.
Katika taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari leo na Katibu wa CCM Mkoa wa Iringa, Mary Tesha, ilielezwa kuwa mgombea mwenza wa urais kwa tiketi ya CCM ataanza ziara yake mkoani hapa tarehe 03-06/09/2010.
Katibu huyo wa mkoa amesema kuwa mgombea mwenza ataanzia Wilaya ya Ludewa ambapo atafanya mikutano mbalimabli katika maeneo ya Manda, Nsungu, Mkoma-ng’ombe, Ludewa mjini na kumalizia na Mlangali kabila yakuendelea ziara katika wilaya zingine mkoani hapa.
Wilaya hixo atakazozitembelea katika ziara yako ya kampeni ya uchaguzi ni pamoja na Njombe, Makete, Mufindi, kilolo na kumalizia na Iringa Mjini.
Aidha, Katibu huyo wa mkoa amesema akiwa Mjini Iringa Dkt. Bilal, atapewa taarifa fupi ya wilaya na baada ya hapo atahutubia wananchi wa Manispaa ya Iringa kwenye mkutano utakaofanyika katika viwanja vya Mwembetogwa.
Hatamaye, mgombea mwenza wa urais kwa tiketi ya CCM, tarehe 06/09/2010 asubuhi ataagana na viongozi wa Mkoa wa Iringa katika Uwanja wa Ndege Nduli tayari kuelekea Mkoa wa Shinyanga.
Pamlomo24 is essentially a digital news platform that shares different types of news updates — social, political, economic, sports, entertainment, and community stories. From the context you’ve given, it is based in Iringa, Tanzania, and functions mainly as an online outlet (likely through social media such as Facebook, YouTube, or other channels) where audiences can get real-time updates.
Subscribe to:
Comments (Atom)
ASAS AWATOA HOFU WANANCHI KUHUSU VURUGU ZA UCHAGUZI
MJUMBE wa Kamati Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa, Salim Abri Asas , amewataka wananchi kujitokeza kwa wingi kupiga kura katika Uchagu...
-
Peter Mbata's the Deputy Headmaster and Amon Chota (academic master). Headmaster of Ifunda Technical School, Mpambwe Paul ...
-
KIKUNDI cha Upendo ni kikundi cha kina mama 20 walioamua kujiunga kwa pamoja na kuanz...
-
Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate ...