Sunday, 26 October 2025

ASAS AWATOA HOFU WANANCHI KUHUSU VURUGU ZA UCHAGUZI


MJUMBE wa Kamati Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa, Salim Abri Asas, amewataka wananchi kujitokeza kwa wingi kupiga kura katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, huku akiwatoa hofu juu ya uvumi unaoenezwa mitandaoni kuhusu uwepo wa vurugu siku ya uchaguzi huo.

Asas amesema kumekuwepo na taarifa zisizo sahihi kutoka kwa baadhi ya watu, ndani na nje ya nchi, wanaotumia mitandao ya kijamii kuhamasisha maandamano na kuchochea vurugu ambazo zinaweza kuhatarisha amani na kuathiri zoezi la uchaguzi.

Akihutubia maelfu ya wanachama na wananchi katika mkutano wa kufunga kampeni za CCM Jimbo la Mafinga Mjini, uliofanyika katika kijiji cha Ugute, kata ya Isalavanu, Halmashauri ya Mji Mafinga, Asas aliwahakikishia wananchi kuwa nchi ipo salama na vyombo vya ulinzi na usalama vimejipanga kikamilifu kulinda amani.

“Nataraji katika siku hizi mbili mtajitokeza kwa wingi kupiga kura siku ya Oktoba 29. Msiogope wala kuwa na hofu, amani ipo na kutakuwa na ulinzi wa kutosha. Nchi yetu imetulia — hayo yote ni maneno ya mitaani,” alisema Asas.

Amesisitiza kuwa Tanzania ipo kwenye mikono salama ya vyombo vya ulinzi na usalama, hivyo wananchi wanapaswa kutumia hali hiyo kama motisha wa kushiriki uchaguzi na kutimiza haki yao ya kikatiba.








Kwa upande wake, Mgombea Ubunge wa Jimbo la Mafinga Mjini, Dickson Lutevele maarufu kama Villa, aliwataka wananchi kujitokeza kwa wingi kupiga kura kama ishara ya shukrani kwa Serikali kwa utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo katika eneo hilo.

Aidha, aliwasisitiza wananchi wote—bila kujali itikadi za kisiasa au imani za kidini—kudumisha amani ambayo ndiyo msingi wa maendeleo endelevu.

“Ni imani yangu kuwa Mufindi kwa mara nyingine tena tutaongoza kwa wingi wa kura kukichagua Chama Cha Mapinduzi kama kawaida yetu,” alisema Villa.


 

Asas urges voters to turn out in large numbers, dismisses election violence fears


 

Iringa. A member of the CCM Central Committee (MCC), Salim Abri Asas, has urged Tanzanians to turn out in large numbers to cast their votes in the upcoming General Election on October 29, assuring them that the country remains peaceful and well-secured.

Mr. Asas dismissed circulating rumours on social media suggesting that there might be violence on election day, saying such claims are being spread by individuals with ill intentions to create fear and discourage voter participation.

He said in recent weeks, there have been coordinated attempts by certain groups, both within and outside the country, to incite youths and other sections of the community to engage in demonstrations and acts that could disrupt peace and affect the election process.

Speaking during a well-attended CCM rally to close the party’s campaigns for Mafinga Urban Constituency, held at Ugute Village in Isalavanu Ward, Mr. Asas assured citizens that the security organs are fully prepared to maintain order and safety throughout the election period.

“I expect all of you to turn out in large numbers to vote on October 29. Do not be afraid or worried — peace prevails, and there will be enough security everywhere. Our country is calm; those stories are just rumours,” said Asas.

He added that Tanzania is in safe hands under its security institutions, urging citizens to take advantage of the prevailing peace to fulfil their constitutional right to vote.

On his part, Dickson Lutevele, popularly known as Villa, who is vying for the Mafinga Urban parliamentary seat, expressed confidence that residents will show up in large numbers to vote as a sign of appreciation for the government’s development efforts in the area.

He emphasized that regardless of political affiliation or religious belief, citizens should prioritize peace, which he described as the foundation of inclusive and sustainable development.

“I strongly believe that once again, Mufindi will lead with overwhelming votes in favour of the CCM, as has always been our tradition,” said Villa.


 

No comments:

ASAS AWATOA HOFU WANANCHI KUHUSU VURUGU ZA UCHAGUZI

MJUMBE wa Kamati Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa, Salim Abri Asas , amewataka wananchi kujitokeza kwa wingi kupiga kura katika Uchagu...