Friday, 12 September 2025

MKUU WA MAJESHI YA ULINZI NCHINI AWASILI MKOANI IRINGA






Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi wa Wananchi wa Tanzania (JWTZ), Jenerali Jacob John Mkunda, amewasili mkoani Iringa leo kwa ziara ya kikazi.

 

Katika ziara hiyo, Jenerali Mkunda amekutana na Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Komredi Kheri James, pamoja na wajumbe wa Kamati ya Usalama ya Mkoa ambapo walijadiliana masuala mbalimbali yanayohusu usalama na ulinzi wa wananchi.

CHIEF OF DEFENCE FORCES ARRIVES IN IRINGA REGION


The Chief of Defence Forces of the Tanzania People’s Defence Force (TPDF), General Jacob John Mkunda, has today arrived in Iringa Region for an official working visit.

During his visit, General Mkunda held talks with the Iringa Regional Commissioner, Comrade Kheri James, alongside members of the Regional Security Committee, where they discussed various matters related to the safety and security of the public.




 

TRA YAZINDUA DAWATI MAALUM LA UWEZESHAJI BIASHARA IRINGA


 Katika jitihada za kuboresha mazingira ya biashara na kuhamasisha ulipaji kodi kwa hiari, Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) mkoa wa Iringa imezindua rasmi Dawati Maalum la Uwezeshaji Biashara. Hatua hii ni sehemu ya mkakati mpana wa kuimarisha ushirikiano kati ya serikali na sekta binafsi.

Akizungumza wakati wa uzinduzi uliofanyika katika viwanja vya Garden, Halmashauri ya Manispaa ya Iringa mnamo 9 Septemba 2025, Meneja wa TRA mkoa wa Iringa, Bw. Peter Jackson, alisema dawati hilo litatoa huduma mbalimbali ikiwemo elimu ya kodi, ushauri wa kisheria pamoja na msaada katika kutatua changamoto zinazowakabili wafanyabiashara katika ngazi zote.

“Dawati hili siyo tu sehemu ya kupata taarifa, bali ni jukwaa la mazungumzo ya moja kwa moja kati ya wafanyabiashara na TRA. Lengo letu ni kukuza uelewa wa pande zote na kuendeleza utamaduni wa ulipaji kodi kwa hiari,” alieleza Jackson.

Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Bw. Benjamin Sitta, aliwahimiza wafanyabiashara kulitumia vyema dawati hilo, akibainisha kuwa serikali ipo tayari kusikiliza na kushughulikia changamoto zao, lakini pia inatarajia ushirikiano katika kutimiza wajibu wa kulipa kodi.

Uzinduzi huo uliongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Bw. Kheri James, ambaye aliipongeza TRA kwa kuanzisha mbinu bunifu ya kuwasogezea karibu walipakodi huduma. Alisema hatua hiyo ni sehemu ya mkakati wa kitaifa wa kuboresha urahisi wa kufanya biashara nchini Tanzania.

Aidha, Bw. James aliwataka wananchi kudai risiti kila wanaponunua bidhaa au huduma, akisema utaratibu huo unaleta uwazi katika mapato na kuchangia maendeleo ya taifa.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Shirikisho la Wafanyabiashara Wadogo Tanzania (SHIUMA) mkoani Iringa, Bw. Kessy Ndandu, alisema uzinduzi wa dawati hilo ni hatua mpya kwa wafanyabiashara wadogo kwani utawasaidia kupata uelewa wa haki na wajibu wao wa kikodi, sambamba na mbinu za kukuza biashara zao kwa kuzingatia sheria.

Hafla hiyo ilihudhuriwa na viongozi wa serikali, wawakilishi wa taasisi za umma na binafsi, vyama vya wafanyabiashara, viongozi wa masoko pamoja na wakazi kutoka maeneo mbalimbali ya mkoa wa Iringa.

MKUU WA MAJESHI YA ULINZI NCHINI AWASILI MKOANI IRINGA

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi wa Wananchi wa Tanzania (JWTZ), Jenerali Jacob John Mkunda, amewasili mkoani Iringa leo kwa ziara ya kikazi.  ...