Thursday, 3 December 2015

MRATIBU WA UN NCHINI, ALVARO RODRIGUEZ ZIARANI MKOANI SINGIDA KUKAGUA MIRADI YA SHIRIKA HILO











Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez akisalimiana na Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dk. Parseko Kone alipomtembelea na kufanya mazungumzo ofisini kwake jana mjini Singida.

Na Modewjiblog team, Singida

Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez amekutana na Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dkt. Parseko Kone ofisini kwake kwa ajili ya kubadilishana uzoefu wa utekelezaji wa miradi inayofadhiliwa na Umoja wa Mataifa mkoani humo.

Mratibu huyo yupo Mkoani hapa kwa siku mbili kukagua miradi inayofadhiliwa na Mashirika ya Umoja wa Mataifa.

Katika siku yake ya kwanza atatembelea mradi wa afya ambao unashughulikia watu wanaoishi na VVU katika kijiji cha Puma wilaya ya Ikungi. Pia atatembelea kikundi cha ufugaji nyuki kinachojihusisha na uzalishaji wa asali na utengenezaji wa mishumaa.

Aidha akiwa kijiji cha Puma atatembelea kambi waliokolazwa watu wenye ugonjwa wa Kipindupindu.

Katika ukaguzi wa miradi hiyo Mratibu huyo atapata nafasi ya kuzungumza na walengwa wa miradi hiyo ili kupata mafanikio na changamoto zilizojitokeza.

Katika siku yake ya pili na ya mwisho mkoani Singida Bw. Alvaro Rodriguez atatembelea mradi mkubwa wa ufugaji nyuki kisasa unaofadhiliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo (UNDP).

Baada ya hapo atatembelea ujenzi wa hospitali ya rufaa inayoendelea kujengwa kijiji cha Mandewa nje kidogo ya mji wa Singida.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dk. Parseko Kone alitoa Shukrani kwa Umoja wa Mataifa kwa misaada yake ya kuisaidia serikali katika kutatua kero mbalimbali za wananchi.

Hata hivyo ameomba Mashirika hayo yaendelea kusaidia katika Nyanja za upatikanaji wa ajira kwa vijana na masoko kwa wakulima.

Mratibu huyo baada ya kumaliza ziara yake mkoani Singida ataelekea mkoa wa Tabora ambapo ataanza ziara yake tarehe 3 mwezi Desemba na baada ya kumaliza mkoa wa Tabora atelekea mkoani Kigoma tarehe 4 hadi 6 nwezi Desemba.

Singida ni kati ya mikoa itakayounufaika na mpango mpya wa malengo ya maendeleo endelevu (Sustainable Development Goals-SDGs) unaotarajiwa kuanza kutekelezwa 2016-2030.



Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dk. Parseko Kone akisalimiana na Mtaalam wa Mahusiano na Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa (UN) Tanzania Hoyce Temu (kulia) aliyeambatana na Bw. Rodriguez. Aliyeketi ni Katibu Tawala wa mkoa wa Singida, Festo Kang'ombe.



Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dk. Parseko Kone (wa kwanza kulia) akiwa kwenye mazungumzo na Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez aliyeambatana na Afisa wa Mambo ya Nje kutoka Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Maulidah Hassan (wa tatu kushoto) pamoja na Mtaalam wa Mahusiano na Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa (UN) Tanzania Hoyce Temu katika ziara ya kukagua miradi mbalimbali inayofadhiliwa na Umoja wa Mataifa mkoani humo. Wa kwanza kushoto ni Mratibu wa TACAIDS mkoa wa Singida, Mdala Fedes. wengine pichani ni Katibu Tawala wa mkoa wa Singida, Festo Kang'ombe (wa kwanza kulia).



Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dk. Parseko Kone akisoma baadhi ya mambo yaliyomo kwenye kitabu cha 'Mwongozo wa wadau wa kilimo na mifugo' kilichoandaliwa na ofisini kwa Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez (hayupo pichani). Kulia ni Katibu Tawala wa mkoa wa Singida, Festo Kang'ombe.



Mtaalam wa Mahusiano na Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa (UN) Tanzania Hoyce Temu akitoa maelezo ya lengo namba 3 ambalo ni 'Afya Njema na Ustawi' wakati wa kutambulisha malengo mapya ya maendeleo endelevu (Sustainable Development Goals-SDGs) kwa Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dk. Parseko Kone walipomtembelea ofisini kwake jana.



Katibu Tawala wa mkoa wa Singida, Festo Kang'ombe akioorodhesha mambo muhimu yanayotakiwa kufanyika katika mkoa wa Singida ili kufanikisha utekelezaji wa lengo namba 3 ambalo ni 'Afya Njema na Ustawi' kati ya malengo 17 ya maendeleo endelevu (SDGs) yanayotarajiwa kuanza kutekelezwa 2016-2030. Wanaoshuhudia tukio hilo kushoto ni Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez aliyeambatana na Afisa wa Mambo ya Nje kutoka Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Maulidah Hassan.



Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dk. Parseko Kone (wa kwanza kulia), Katibu Tawala wa mkoa wa Singida, Festo Kang'ombe (wa pili kulia) pamoja na Mratibu wa TACAIDS mkoa wa Singida, Mdala Fedes (wa tatu kushoto) wakimkabidhi Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez bango hilo lenye mambo muhimu yanayotakiwa kufanyika katika mkoa wa Singida ili kufanikisha lengo namba 3 kati ya malengo 17 ya maendeleo endelevu (SDGs) aliyeambatana kwenye ziara hiyo na Afisa a Mambo ya Nje kutoka Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Maulidah Hassan (katikati kulia).



Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dk. Parseko Kone (wa pili kulia), Katibu Tawala wa mkoa wa Singida, Festo Kang'ombe (wa pili kushoto) katika picha ya pamoja na Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez (kulia) kwenye bango maalum lenye rangi mbalimbali zinazowakilisha malengo 17 ya maendeleo endelevu (SDGs) yanayotakiwa kumfikia kila mwananchi nchini kwa ajili ya utekelezaji.



Kutoka kushoto ni Mratibu wa TACAIDS mkoa wa Singida, Mdala Fedes, Katibu Tawala wa mkoa wa Singida, Festo Kang'ombe, Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dk. Parseko Kone, Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez, Katibu wa Mkuu wa Mkoa wa Singida, Bw. Sute pamoja na Afisa wa Mambo ya Nje kutoka Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Maulidah Hassan.



Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dk. Parseko Kone (katikati) akibadilishana mawazo na Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez pamoja na Ofisa kutoka Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Maulidah Hassan nje ya jengo la Ofisi ya Mkuu huyo wa mkoa.



Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez akiagana na Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dk. Parseko Kone.

......AKIWA NJIANI KUELEKEA MKOANI SINGIDA......



Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez akiwa ameambatana na Ofisa kutoka Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Maulidah Hassan (kulia) mara baada ya kusimamisha gari maeneo ya Babati mjini.



Neema Mikaeli (22)akihamaki kuona watu waliokuwa wakimsogelea (hawapo pichani) katika eneo alilokuwa akifua nguo kwenye dimbwi la maji machafu ya mvua kama yanavyoonekana pichani.

Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa nchini akiwa njiani kuelekea mkoani Singida alishtushwa kuona mkazi mmoja wa Babati mjini Neema Mikaeli (22) akifua nguo kwenye dimbwi la maji machafu ya mvua na kusimama na kuzungumza nae ambapo aligundua kuna tatizo la maji safi na salama kwa wakazi wa eneo hilo pamoja na ukataji miti ambao unapelekea kuharibu mazingira.

Katika mazungumzo ya Neema alisema kuwa kuna mabomba ya maji yaliyowekwa zaidi ya miaka 3 sasa lakini hayatoi maji na hivyo kupelekea wao kutembelea umbali mrefu ambao kuna mto na wanatumia maji ya mto huo kupikia na kunywa.

Akiongea na Mikaela alimuhakikishia kwamba Umoja wa Mataifa utazidi kufanya kazi ka ukaribu na serikali ya Tanzania sambamba na kukabiliana na changamoto za mabadiliko ya tabianchi.



Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez, Ofisa kutoka Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Maulidah Hassan pamoja na Mtaalam wa Mahusiano na Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa (UN) Tanzania Hoyce Temu wakizungumza na Mkazi huyo wa wilaya ya Babati mjini mkoani Manyara, Neema Mikaeli (22) aliyekuwa akifua nguo zake kwenye dimbwi hilo kutokana na kukosekana kwa maji katika eneo lao.



Haya ndio maji ambayo hata sabuni ya unga haikolei yaliyokutwa yakitumiwa na Neema Mikaeli (22) (hayupo pichani) kufulia nguo zake.



Neema Mikaeli (22) akiwa kwenye eneo la dimbi la maji ya mvua akiendelea kufanya usafi wa nguo zake.

MELI MPYA YA MV MAPINDUZI YAWASILI KATIKA BANDARI YA ZANZIBAR, IMETOKA KOREA





Meli Mpya ya MV Mapinduzi Ikiwasili katika Bandari ya Zanzibar Ikitokea Nchini Korea Ilikotengenezwa.


Meli Mpya ya MV Mapinduzi 2 ikiwasili Zanzibar ikitokea Nchini Korea

Meli Mpya ya MV Mapinduzi ikiwasili katika bandari ya Zanzibar ikitokea Nchini Korea baada ya kukamilika kwa Uundaji wake uliochukua miezi 18, ikiwa katika bahari ya Zanzibar ikielekea katika bandari kwa ajili ya ufungaji wa gati katika bandari ya Malindi Zanzibar.

Wananchi wa Zanzibar wakiipokea Meli yao Mpya ya MV Mapinduzo 2 wakiwa katika bustani ya Forodhani Zanzibar.

Wananchi wa Zanzibar wakichukua picha kupitia simu zao Meli Mpya ya MV Mapinduzi wakati ikiwasili Zanzibar katika bandari ya Zanzibar

Meli Mpya ya Mv Mapinduzi 2 ikiwa katika bahari ya Zanzibar.

Wananchi wa Zanzibar wakiwa katika bustani ya forodhani wakiipokea Meli yao Mpya ya MV Mapinduzi 2 ikiwasili Zanzibar ikitokea Nchini Korea ilioundwa meli hiyo.

Wananchi wa Zanzibar wakichukua picha kupitia simu zao Meli Mpya ya MV Mapinduzi wakati ikiwasili Zanzibar katika bandari ya Zanzibar, wakiwa katika bustani ya forodhani Zanzibar

Wananchi wakiwa katika Bandari Kuu ya Malindi Zanzibar wakiipokea Meli yao Mpya ya MV Mapinduzi ilipokuwa ikifunga gati katika bandari hiyo ya Zanzibar.

Wafanyakazi wa Shirika la Meli Zanzibar wakipiga picha Meli Mpya ya Mv Mapinduzi kupitia simu zao kwa ajili ya kumbukumbu kwa kuja kwa Meli hiyo Mpya.

MV Mapinduzi ikiwa katika Bandari ya Zanzibar ambayo ina uwezo wa kuchukua Abiria na Mizigo na Magari.

Waziri wa Fedha Zanzibar Mhe Omar Yussuf Mzee akiwapungia mikono Wananchi waliofika katika Bandari ya Malindi Zanzibar ikifunga Gati akiwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Miundombinu na Mawasiliano Dk Juma Malik.

Mwananchi wa Zanzibar akiwa na simu yake baada ya kuchukua picha ya Meli ya Mv Mapinduzi 2 na kuwatumia Wananchi kupitia simu yake.




Wafanyakazi wa Shirika la Meli Zanzibar na wa Shirika la Bandari Zanzibar wakishangilia Meli Mpya ya MV Mapinduzi wakati ikiwasili katika bandari ya Malindi ikifunga Gati
Wafanyakazi wa Shirika la Meli Zanzibar na wa Shirika la Bandari Zanzibar wakishangilia Meli Mpya ya MV Mapinduzi wakati ikiwasili katika bandari ya Malindi ikifunga Gati


Wananchi wakiwa katika Bandari ya Zanzibar wakiipokea Meli ya Mv Mapinduzi 2 katika bandari ya Zanzibar.

Meli Mpya ya MV Mapinduzi 2 ikiwa katika bandari ya Malindi baada ya kufunga gati katika bandari hiyo ya Zanzibar.

Wafanyakazi wa Shirika la Mandari wakiwa katika Bandari ya Zanzibar wakipokea Meli Mpya ya Mv Mapinduzi 2

Waandishi wa habari wa Zanzibar na Viongozi wa Shirikala la Meli Zanzibar wakiwa katika Meli ya Mv Mapinduzi 2 wakitokea katika kisiwa cha Chumbe kuipokea meli hiyo ikitokea Nchini Korea ilikoundwa Meli hiyo. Imetayarishwa na OthmanMapara.Blogspot.
Zanzinews.com.

UN, SERIKALI ZATAKA VIJANA KUONGOZA KATIKA KUKABILI MABADILIKO TABIA NCHI SINGIDA



Mkuu wa wilaya ya Ikungi, Chigulu Charles akitoa neno la ukaribisho kwa Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez aliyeambatana na Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dkt. Parseko Kone katika ziara ya kukagua miradi inayofadhiliwa na Mashirika ya Umoja wa Mataifa mkoani Singida.

Na Modewjiblog team, Singida

MRATIBU wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi mkazi wa Shirika la Mipango ya Maendeleola umoja huo (UNDP) Bw.Alvaro Rodriguez, amezuru mradi wa ufugaji nyuki uliopo Ikungi mkoani Singida.

Katika Ziara hiyo kwenye mradi unaofadhiliwa na UNDP, Mratibu huyo aliambatana na Mkuu wa mkoa wa Singida Dk. Parseko Kone, na Ofisa wa Mambo ya Nje kutoka Kitengo cha Ushirikiano wa Kimataifa wizara ya Mambo ya Nchi za Nje, Bi. Maulidah Hassan.

Viongozi hao walifika katika mradi huo kuangalia mafanikio ya mradi huo unaotekelezwa chini ya mpango wa miaka mitano wa Msaada wa Maendeleo wa Umoja wa Mataifa, (UNDAP).

Mradi huo uliofadhiliwa na UNDP kwa thamani ya Shilingi milioni 224 umewanufaisha wafugaji 2,000 huku wanawake wakiwa ni 1,100.

Mradi huo ulianza kutekelezwa kuanzia mwaka 2013 na 2014 umelenga kuendeleza shughuli za ufugaji nyuki wilayani Ikungi.

Aidha mradi huo umelenga kupunguza umaskini kutunza mazingira kwa njia ya uragibishi na kufunza wananchi kuhusu suala la ufugaji nyuki na utunzaji wa mazingira.

Kutokana na mradi huo, fursa za ajira zilitengenezwa, hasa vijana wa kijijini, kuwepo na eneo la kisasa la kutengeneza mizinga ya nyuki na uchomaji moto uliokuwa unafanywa katika misitu ukapungua sana.

Akizungumza katika eneo la mradi Bw. Rodriguez, aliusifu utawala wa mkoa wa Singida kwa kufanyakazi na UNDP kwa lengo la kujenga uwezo kwa wananchi na wakati huo huo kutunza mazingira.



Mwakilishi wa Mratibu Mkuu wa Taasisi ya Kijamii ya Fursa za Kimaendeleo (Fu-DI) ya wilayani Ikungi, inayosimamia mradi wa ufugaji nyuki kisasa, Boniface Mathew akitoa maelezo ya mradi kwa Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez. Pamoja na mambo mengine Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa UNDP limeshiriki katika ufadhili wa utengenezaji wa mizinga bora pamoja na kutoa semina mbalimbali kwa wafugaji nyuki uliogharimu kiasi cha Shilingi milioni 224 hadi sasa.

“Ninafuraha sana kuona matokeo mema ya mradi huu; ni lengo letu kutunza mazingira huku tukifaidika na uhifadhi huo. Mafanikio haya yanastahili kuigwa na wengine,” alisema Rodriguez akiongeza kuwa wanawake walifaidika sana na mradi huu kiasi cha kustahili kufanyiwa kazi katika eneo jingine.

Mkuu wa mkoa wa Singida Dk. Parseko Kone alisema mradi wa UNDP una matokeo yenye tija kubwa na kuwataka waliofadhiliwa kutumika kufunza jamii nyingine umuhimu wa ufugaji na hifadhi ya misitu.

“leo tunashuhudia ufugaji nyuki wa kisasa ambao umebadilisha sekta ya ufugaji nyuki, tija katika ufugaji huu imeongezeka maradufu. Hiyo imesaidia kaya zaidi ya 1000 kupata kipato cha kukabiliana na umaskini.” Alisema Mkuu wa mkoa.

Aidha alisema kwamba wafugaji nyuki wameweza kuwa pamoja na kujipatia asali na mazao mengine kutokana na shughuli ya ufugaji nyuki kama nta, sumu ya nyuki, uchavuaji na kadhalika.



Mwakilishi wa Mratibu Mkuu wa Taasisi ya Kijamii ya Fursa za Kimaendeleo (Fu-DI) ya wilayani Ikungi, Boniface Mathew (kulia) akikabidhi taarifa ya mradi kwa Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez.

Kutokana na shughuli hizo za ufugaji zaidi ya fursa 2,500 za ajira zilitengenezwa.nafasi hizo ni kama za mfugaji, wachongaji mizinga, wauza asali, wasafirishaji na wachakati wa asali.

Wilaya ya Ikungi imejaliwa kuwa na misitu ya Miombo na Minanga ambayo ni chanzo kizuri cha chavua.

Mradi wa ufugaji nyuki Ikungi umelenga kufungua njia zote za uzalishaji asali na kupiga vita umaskini kwa kuanzisha fursa za ajira za kujitegemea.

Mwakilishi huyo wa UNDP na Mkuu wa mkoa pia walitembelea hospitali ya rufaa ya mkoa ambayo ipo katika awamu ya mwisho ya ujenzi.

Itakuwa ni moja ya hospitali kubwa itakayohudumia mikoa mitano katika ukanda wa kati.

Katika mazungumzo yake Mratibu wa UN alimpongeza Mkuu wa mkoa kwa juhudi zake za kuhudumia wanawake waume na watoto wa Tanzania.



Baadhi ya mizinga ya kisasa iliyofadhiliwa na UNDP ikiwa kwenye karakana ya kutengeneza mizinga ya nyuki tayari kugawiwa kwa vikundi mbalimbali vya wanawake na vijana iliyopo kwenye Taasisi ya Kijamii ya Fursa za Kimaendeleo (Fu-DI) ya wilayani Ikungi.



Mwakilishi wa Mratibu Mkuu wa Taasisi ya Kijamii ya Fursa za Kimaendeleo (Fu-DI) ya wilayani Ikungi, Boniface Mathew akimwonyesha mizinga ya kisasa ya ufugaji nyuki Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez (katikati). Kushoto ni “Programme Assistant- Global Environmental Facility Small Grant”, UNDP, Stella Zaa.



Malengo ya maendeleo endelevu sasa yamewafikia wafugaji wa nyuki Singida na waratibu wa miradi ya wafugaji wa nyuki Singida. Pichani ni Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez katika karakana ya kutengenezea mizinga ya kisasa.



Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez akisalimiana na wanakikundi cha Uaminifu kinachojihusisha na ufugaji nyuki kwa njia ya kisasa mara baada ya kuwasili kukagua shamba darasa la kuzalisha makundi ya nyuki lilipo katika kijiji cha Mahambe tarafa ya Ikungi mkoani Singida.



Mwakilishi wa Mratibu Mkuu wa Taasisi ya Kijamii ya Fursa za Kimaendeleo (Fu-DI) ya wilayani Ikungi, Boniface Mathew akijiandaa kumvisha nguo maalum Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dkt. Parseko Kone kabla ya kuingia kwenye shamba darasa la kuzalisha makundi ya nyuki lilipo katika kijiji cha Mahambe tarafa ya Ikungi mkoani Singida.



Mwanakikundi cha Uaminifu kinachojihusisha na ufugaji nyuki kwa njia ya kisasa, Juma Simbu, akitoa taarifa ya kikundi kwa Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez aliyeambatana na Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dkt. Parseko Kone ambapo alisema mradi wa ufugaji utawatoa kwenye lindi la umaskini, japokuwa wanakabiliwa na changamoto kadhaa.



Mwanakikundi cha Uaminifu kinachojihusisha na ufugaji nyuki kwa njia ya kisasa, Juma Simbu akikabidhi taarifa ya kikundi kwa Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez.



Sehemu ya eneo la shamba darasa la kuzalisha makundi ya nyuki lilipo katika kijiji cha Mahambe tarafa ya Ikungi mkoani Singida.



Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez akisaidiana na wanakikundi cha Uaminifu kinachojihusisha na ufugaji nyuki kwa njia ya kisasa kupandisha moja kati ya mizinga iliyofadhiliwa na UNDP katika shamba darasa la kuzalisha makundi ya nyuki lilipo katika kijiji cha Mahambe tarafa ya Ikungi mkoani Singida.



Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dkt. Parseko Kone wakipandisha moja kati ya mizinga iliyofadhiliwa na UNDP kwenye shamba hilo.Kwa matukio zaidi bofya hapa





Wednesday, 2 December 2015

UN, SERIKALI WASHUKURU WAKAZI WA SINGIDA KUJIMILIKISHA MIRADI YA MAENDELEO



Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez akisalimiana na mmoja wa watendaji wa wilaya ya Ikungi mkoani Singida mara tu alipowasili kijiji cha Puma kukagua mradi wa ufugaji kuku wa kusaidia watu wanaoishi na VVU unaofadhiliwa na Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) kupitia TACAIDS. Wa pili kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dkt. Parseko Kone.

Na Modewjiblog team, Singida

MRATIBU Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja huo (UNDP), Bw.Alvaro Rodriguez ameipongeza serikali ya Tanzania kwa kuweka mazingira yanayofanikisha miradi mbalimbali ya maendeleo endelevu.

Mratibu huyo alitoa wito huo wakati alipofanya ziara ya siku mbili mkoani Singida kukagua miradi inayofadhiliwa na Umoja wa Mataifa.

Baada ya kuona mafanikio katika miradi hiyo Bw. Rodriguez, alisifu pia jamii ya Singida kwa kujitoa kuhakikisha kwamba wanafanikisha miradi hiyo kwa kuifanya kuwa miradi yao.

Katika ziara hiyo ambapo pia Mkuu wa Mkoa wa Singida Dk. Parseko Kone na Afisa wa Mambo ya Nje kutoka Kitengo cha ushirikiano wa kimataifa Wizara ya Mambo ya Nchi za Nje, Bi. Maulidah Hassan walikuwepo, Mratibu alitembelea kituo cha watu wanaoishi na Virusi vya Ukimwi; Kituo cha kutibu kipindupindu na Ushirika wa wajasiriamali vijana.

Miradi hiyo inafadhiliwa na Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Shirika la Afya Duniani (WHO), Shirika la Kazi Duniani (ILO) na Shirika la Umoja wa Mataifa la Kupambana na Ukimwi (UNAIDS).

UNAIDS ni mshirika wa karibu wa serikali ya Tanzania katika mapambano dhidi ya UKIMWI kupitia mashirika ya TACAIDS na ZAC.


Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dkt. Parseko Kone akiteta jambo na Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez mara baada ya kuwasili kwenye kijiji cha Puma kukagua mradi wa kikundi cha ufugaji kuku kwa watu wanaoishi na VVU.

Mashirika ya TACAIDS na ZAC yanatambulika kitaifa na kimataifa kutokana na shughuli zake za kuhudumia umma wa Tanzania.

Miradi hiyo imewezesha vijana wengi kuwa wajasiriamali, kudhibiti Kipindupindu na kuongeza uelewa wa UKIMWI.

Alisema kwamba maendeleo endelevu yanahusisha serikali na jamii kuangalia changamoto zinazokabili jamii na kuzitafutia ufumbuzi kwa kuoanisha na malengo ya maendeleo endelevu SDGs.

Miradi hiyo iliyopo Singida inatekelezwa chini ya mpango wa msaada wa maendeleo wa Umoja wa Mataifa,(UNDAP).

Mashirika ya Umoja wa Mataifa yamekuwa yakifanywa shughuli mbalimbali za kusaidia wananchi wa Tanzania waume, wake na watoto kupitia mpango wa msaada wa maendeleo wa Umoja wa Mataifa,(UNDAP) wa mwaka 2011-2016.

Naye Mkuu wa mkoa wa Singida, Dk Kone akisisitiza umuhimu wa wananchi kujimilikisha miradi hiyo, amewaambia Umoja wa Mataifa kwamba kwamba wananchi wa mkoa huo wataendelea kujimilikisha miradi hiyo na kuifanya ya kwao ili kuharakisha maendeleo endelevu.


Mkuu wa wilaya ya Ikungi mkoani Singida, Chigulu Charles (wa kwanza kulia) akitoa taarifa yake ya mapambano dhidi ya maambukizi mapya ya Virusi vinavyosababisha ugonjwa wa UKIMWI wilayani humo. Wa tatu kushoto,ni Mratibu mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez na wa pili kushoto ni Mkuu wa mkoa wa Singida, Dk.Parseko Kone.

Alisema maelfu ya wananchi wa Singida wamenufaika na miradi ya maendeleo inayofadhiliwa na Umoja wa Mataifa kupitia mashirika yake yaliyopo hapa nchini .

Aidha alitaka Mashirika hayo kuendelea kusaidia miradi mbalimbali na hasa wakati Mpango wa pili wa Msaada wa maendeleo (UNDAP II) unapokaribia kuanza mwakani, sanjari na mpango wa maendeleo wa taifa Julai 2016.

Alisema Singida imesonga mbele katika maendeleo katika siku za karibuni lakini bado inahitaji msaada wa mashirika ya Umoja wa Mataifa kuendelea kuhifadhi mafanikio na kuyaboresha.


Mhudumu wa watu wanaoishi na VVU kata ya Puma tarafa ya Ihanja wilaya ya Ikungi, Kelvin Mwiru, akitoa taarifa yake juu ya majukumu ya kuhudumia watu 150 wanaoishi na VVU katika vijiji vya kata ya Puma na vijijini jirani.Mhudumu huyo ameiomba halmashauri ya wilaya ya Ikungi na wadau wengine kumtambua na kumpa ushirikiano katika kazi hiyo ngumu ya kujitolea kuwahudumia watu wanaoishi na VVU ambao wanaongezeka kila kukicha.


Mratibu mkzi wa mashirka ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez (anayengalia kamera) akitoa nasaha zake mbele ya kikundi cha ufugaji kuku cha Upendo cha watu wanaoishi na VVU na wananchi kwa ujumla wa kijiji cha Puma wilaya ya Ikungi.Mwenye suti ya bluu, ni Mkuu wa mkoa wa Singida, Dkt. Parseko Kone.


Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez na Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dkt. Parseko Kone wakiangalia baadhi ya kuku wa mayai walipotembelea kikundi cha ufugaji kuku cha Upendo cha watu wanaoishi na VVU na wananchi kwa ujumla wa kijiji cha Puma wilaya ya Ikungi.


Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez (kushoto) Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dkt. Parseko Kone (kulia) pamoja na Afisa wa Mambo ya Nje kutoka Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Maulidah Hassan (katikati) wakitazama mayai yanayototolewa na kuku hao.


Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez, Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dkt. Parseko Kone, Mkuu wa wilaya ya Ikungi, Chigulu Charles (kulia), Afisa wa Mambo ya Nje kutoka Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Maulidah Hassan na Mratibu wa TACAIDS mkoa wa Singida, Mdala Fedes katika picha ya pamoja na baadhi ya wanakikundi cha ufugaji kuku cha Upendo cha watu wanaoishi na VVU.


Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dkt. Parseko Kone akiondoka katika kijiji cha Puma kuelekea kijiji cha Mandewa kilichopo Singida mjini.


Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez akisalimiana na Mganga mfawidhi wa manispaa ya Singida, Dk. John Mwombeki baada ya kuwasili kwenye kambi ya muda ya wagonjwa wa Kipindupindu iliyopo katika kijiji cha Mandewa nje kidogo ya mji wa Singida akiwa amefuatana na Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dkt. Parseko Kone.


Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez akiingia kwenye kambi ya muda ya wagonjwa wa kipindupindu.


Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez akisaini kitabu cha wageni katika kambi ya wagonjwa wa Kipindupindu.


Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez akiwaeleza jambo mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dkt. Parseko Kone (kushoto) na Afisa kutoka Shirika la Afya (WHO) kanda ya Dodoma, Dk. Cyrialis Mutabuzi (kulia) pamoja na Mtaalam wa Mahusiano na Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa (UN) Tanzania Hoyce Temu (wa pili kushoto).


Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dkt. Parseko Kone akizungumza na mgonjwa wa kipindupindu kutoka kijiji cha Mtavila wilaya ya Ikungi, Jumanne Shaban. Dkt. Kone amemuagiza akirudi kijijini akawe Balozi mzuri wa mapambano dhidi ya kipindupindu.WHO inasaidia uendeshaji wa vituo hivi pamoja na tiba.

WATOTO WAITAKA SERIKALI KUTUNGA SHERIA KALI ...

Na Friday Simbaya, Mufindi  Wanafunzi wa shule za msingi na sekondari wilayani Mufindi mkoani Iringa wameiomba serikali kwa kush...