Friday, 9 June 2017

RC ANNA MNGWIRA ATEMBELEA FAMILIA YA DKT NDESAMBURO,AZUNGUMZA NA WANACCM



Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro,Anna Mngwira akizungumza na baadhi ya viongozi wa Chama cha Mapinduzi alipotembelea ofisi za chama hicho kujitamburisha .kushoto kwake ni Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi mkoa wa Kilimanjaro Idd Juma ,na anayefuatia ni Katibu tawala mkoa wa Kilimanjaro Mhandisi,Aisha Amour.


Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Manispaa ya Moshi,Elizabeth Minde (katikati) akifurahia jambo wakati Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Anna Mngwira (hayupo pichani) alipokutana na uongozi wa chama hicho katika ofisi za CCM-Mkoa wa Kilimanjaro.



Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Kilimanjaro ,Idd Juma akitoa neon la shukrani mara baada ya Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro ,Anna Mngwira kutembelea ofisi za chama hicho.


Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Anna Mngwira akitoka ofisi za Chama cha Mapinduzi mkoa wa Kilimanjaro mara baada ya kuonana na viongozi wa chama hicho.


Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro ,Anna mngwira akisalimaiana na Katibu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) mkoa wa Kilimanjaro alipofika nyumbani kwa Marehemu Dkt Philemoni Ndesamburo kutoa pole kwa familia.


Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro ,Anna Mngwira akisalimiana na mtoto wa Marehemu Dkt Philemoni Ndesamburo ,Sindato Ndesamburo alipotembelea nyumbani kwa marehemu kutoa pole kwa familia.


Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro,Anna Mngwira akitia saini katika kitabu cha waombolezaji mara baada ya kufika nyumbani kwa Marehemu Dkt Ndesamburo kutoa salamu za pole kwa familia.


Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro ,Anna mngwira akizungumza jambo na mjane wa Marehemu Dkt Ndesamburo ,Ndehorio Ndesamburo alipofika nyumbani kutoa salamu za pole kwa familia.



Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro,akitembelea kaburi ulipolazwa mwili wa marehemu Dkt Philemoni Ndesamburo alipofika nyumbani kutoa salamu za pole kwa familia.


Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro,Anna Mngwira akiongoza sala katika kaburi la marehemu Dkt Philemon Ndesamburo.


Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Anna Mngwira akimpa mkono wa pole Mbunge wa viti maalumu na mtoto wa marehemu Dkt Ndesamburo ,Lucy Owenya alipofika kutoa salamu za pole kwa familia y marehemu.



Mbunge wa Viti Maalum Chadema mkoa wa Kilimanjaro,Lucy Owenya akizungumza jambo na mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro,Anna Mngwira alipofika kutoa salamu za pole kwa familia.


Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro,Anna Mngwira akisalimiana na wananchi katika neo la Kwa Alphonce wakati akiwa njiani akitoka kutoa salamu za pole kwa familia ya Dkt Ndesamburo.



Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro,Anna Mngwira akiwa katika picha ya pamoja na wananchi alipowasalimia katika eneo la Kwa Alphonce mjini Moshi.


Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro akizungumza na mmoja wa wakazi wa mkoa wa Kilimanjaro aliposhuka kwenye gari kuwasalimia.




Na Dixon Busagaga wa Busagaga's Orijino Blog.


Thursday, 8 June 2017

HABARI KUHUSU UTAMBUZI NA USAJILI WA WAKAZI WA MANISPAA YA IRINGA


Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa kushirikiana na Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA), na Halmashauri ya Manispaa ya Iringa tumeanza zoezi la Kutambua na Kusajili wakazi wa Manispaa ya Iringa.
Zoezi limeanza tarehe 07/06/2017 na linatarajiwa kukamilika tarehe 05/07/2017. Zoezi linaanza saa 1 asubuhi hadi saa 11 Jioni. Zoezi litafanyika katika Vituo vya Usajili vilivyopo katika Kata zote 18 za Manispaa ya Iringa kwa mujibu wa Ratiba ilivyopangwa kila Kata imepangiwa siku 3 za usajili.   

Zoezi za usajili litahusisha wananchi wote raia wa Tanzania wenye umri wa miaka 18 na kuendelea.

Vitu vya Msingi anavyotakiwa kwenda navyo Mwananchi Raia wa Tanzania katika kituo cha usajili ni:-

1.   Nyaraka halisi (original) na vivuli vya kuthibitisha uraia na umri wa Mhusika,
2.   Cheti cha Kuzaliwa,
3.   Pasi ya Kusafiria,
4.   Vyeti vya Elimu ya Msingi na Sekondari,
5.   Leseni ya Udereva,
6.   Kitambulisho cha Bima ya Afya,
7.   Kitambulisho cha Mpiga kura.

Kwa kuwa zoezi hili linahusisha upigaji wa Picha, kwa ajili ya ubora wa picha, Tunaelekeza yafuatayo kwa wananchi:-
· kutovaa nguo Nyeupe, Kijivu, Bluu mpauko, Pinki, nguo zenye kung’aa sana, Jezi, nguo zenye nembo, kofia aina yeyote ama kupaka Hina mikononi.

Matarajio katika Halmashauri ya Manispaa ya Iringa ni kusajili wakazi 130,000 kwa ajili ya Vitambulisho vya Taifa.

Mwananchi jitokeze Usajiliwe ili Upate Kitambulisho cha Taifa kwa Maendeleo yako na Taifa kwa Ujumla
Imetolewa na:

Dennis Gondwe,
Afisa Habari- Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
IRINGA8/6/2017 

RATIBA YA USAJILI KATIKA KATA NI KAMA IFUATAVYO:
SN
JINA LA KATA
TAREHE ZA USAJILI
1
KITWIRU
7-9/6/2017
2
RUAHA
7-9/6/2017
3
IGUMBILO
10-12/6/2017
4
MSHINDO
10-12/6/2017
5
KITANZINI
10-12/6/2017
6
MIVINJENI
10-12/6/2017
7
MLANDEGE
13-15/6/2017
8
KWAKILOSA
13-15/6/2017
9
ILALA
13-15/6/2017
10
MWANGATA
18-20/6/2017
11
ISAKALILO
18-20/6/2017
12
MKWAWA
21-23/6/2017
13
MAKORONGONI
24-26/6/2017
14
GANGILONGA
24-26/6/2017
15
KIHESA
27-29/6/2017
16
MTWIVILA
30/6-02/7/2017
17
MKIMBIZI
30/6-02/7/2017
18
NDULI
3-5/7/2017


Monday, 5 June 2017

MBUNGE CHUMI AKABIDHI VITANDA 35 SHULE YA ISALAVANU



Mbunge wa Jimbo la Mafinga Mjini Cosato Chumi (kushoto) kwa kushirikiana na wadau wake amekabidhi vitanda 35 ‘double decked’ vyenye thamani ya shilingi milioni sita na nusu (6.5m/-) kwa wanafunzi wa shule ya Sekondari ya Isalavanu wilayani Mufindi, mkoani Iringa jana. Shule hiyo ilikuwa vitanda vitano tu na kupelekea wanafunzi hao kutandika magodoro chini. 

MAGAZETI LEO JUMANNE JUNI 6
































WATOTO WAITAKA SERIKALI KUTUNGA SHERIA KALI ...

Na Friday Simbaya, Mufindi  Wanafunzi wa shule za msingi na sekondari wilayani Mufindi mkoani Iringa wameiomba serikali kwa kush...