Sunday, 5 February 2017

KAIJAGE: TANZANIA YA VIWANDA HAITAWEZEKANA KAMA MASHAURI YANACHUKUA MREFU KUMALIZIKA




Mwenyekiti wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) Rwezaula Kaijage akisoma hotuba iliyoandaliwa na Mawakili wa kujitegemea Kanda ya Mahakama Kuu ya Iringa katika maadhimisho ya Siku ya Sheria nchini yaliofanyika kwenye viwanja vya makahama kuu ya Iringa juzi. (Picha na Friday Simbaya)


Na Friday Simbaya, Iringa

Jaji Mfawidhi, Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Iringa, Mheshimiwa Jaji Shanghali amesema Kanda ya Mahakama Kuu Iringa ambayo inajumuisha mkoa wa Njombe kwa sasa wana mashauri 1,777. 

Alisema kuwa Kati ya mashauri hayo, wanayo mashauri 211 tu yenye umri zaidi ya miaka miwili (2) ambayo kati yake ni mashauri 123 ya Jinai (Mauaji) na mashauri 87 ya Madai. 

Jaji Shanghali alisema hayo jana wakati wa sherehe za sheria nchini zilizofanyika katika viwanja vya Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Iringa.

Alisema kuwa katika mashauri mengine yote 1,566 yana umri chini ya miaka miwili (2).

“Takwimu zinaonyesha kuwa ni asilimia nane (8%) tu ya mashauri ya muda mrefu yaliyobaki kwa nchi nzima, ” alisema Jaji Shanghali. 

Aliongeza kuwa wajibu wa Mahakama ni kutekeleza jukumu lake la utoaji haki kwa wakati na Mashauri yasikilizwe na kupatiwa ufumbuzi kwa wakati bila kuchelewa. 

Naye Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Amina Masenza alisema kuwa haki ikitolewa kwa wakati wananchi watafanya shughuli zao za maendeleo wakiwa huru na kwa ufanisi. 

“Haki ikinyimwa maendeleo hayawezi kupatikana kwa kuwa wananchi hawatakuwa huru kufanya shughuli zao kikamilifu na hivyo kudidimiza kasi ya maendeleo,” alisema Masenza. 

Alisema kuwa Ibara ya 11, ya Katiba ya Jumhuri ya Muungano wa Tanzania inampa haki kila mwananchi kufanya kazi kwa bidii na kwamba kila mtu ataishi kwa jasho lake. 

Masenza alisema kuwa Mahakama ni mamlaka ya utoaji haki kikatiba na ili kuharakisha ukuaji wa uchumi na kuomba ijitahidi kwa kadri iwezavyo kuharakisha kutoa haki ili kuchochea kasi ya maendeleo kwa wananchi. 

“Tumeshuhudia mlundikano wa mashauri katika Mahakama, Upelelezi kuchukua muda mrefu, mlundikano wa watuhumiwa katika mahabusu, mashauri kuchukua muda mrefu bila sababu za msingi, masharti magumu ya dhamana,” alisema Masenza. 

Mkuu wa Mkoa huyo aliviomba vyombo vyote vinavyohusika katika utoaji wa haki (polisi, Waheshimiwa Majaji, Mawakili wa Serikali na wa kujitegemea, Viongozi wa Serikali, Watumishi wote wa Mahakama washirikiane kwa pamoja katika kutoa haki ili kuchochea maendeleo).

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Mawakili wa kujitegemea Kanda ya Mahakama Kuu Iringa Rwezaula Kaijage akisoma hotuba yake alisema kuwa wananchi wakiwemo Watuhumiwa na Mashahidi wasipoteze muda mwingi Mahakamani wakati shughuli zao za kilimo, biashara na uchumi zimesimama. 

Alisema kuwa Mahakama ya Tanzania kwa kushirikiana na wadau wake wachukua hatua kadhaa kuhakikisha kuwa mashauri hayakai Mahakamani kwa muda mrefu. 

Kaijage alisema kuwa hali hiyo, wananchi wanapokuwa Mahakamani, wanategemea na wanatamani mashauri yao yasikilizwe na kutolewa uamuzi mapema ili mashauri yakiishamalizika, waendelee na shughuli za kujenga uchumi.

Alisema kuwa Tanzania ya viwanda haitawezekana kama mashauri yatachukua miezi na hata miaka bila kumalizika yakiwafanya wahusika na mashaidi wao kufika mahakamani kila mara ili hali wakiacha shughuli zao za uchumi. 

“Katika Mkoa wetu wa Iringa, tunao mfano mzuri wa Wilaya ya Kilolo ambayo ina Mahakama ya Wilaya, lakini haina gereza na ofisi ya mkuu wa polisi wa wilaya hiyo iko kilomita karibu sabini toka makao makuu ya wilaya,” alisema. 

Alisema kuwa hali hii imeifanya wilaya hiyo ipange kusikiliza mashauri ya jinai kwa siku mbili katika juma na hii ni kutokana na uwezo mdogo wa mkuu wa polisi wa wilaya kusafirisha mahabusu kutoka gereza la Iringa mjini hadi Kilolo. 

Kila siku ya mashauri hayo, mwendesha mashtaka analazimika kusafiri kutoka Mbigili, kuja Iringa mjini, kuwachukua mahabusu na kuwapeleka Kilolo. 

“Baada ya mashauri safari hiyo inajirudia. Tumeshuhudia mara nyingine mkuu wa polisi akishindwa kupata usafiri wa kuwafikisha mahabusu mahakamani wakati mashahidi wamekwishaandaliwa,” alisema Kaijage.

Hata hivyo, alisema kuwa Mabishano ya kisheria miongoni mwa mawakili wanaowatetea wadaawa au watuhumiwa; ama miongoni mwa mawakili wa kujitegemea na waendesha mashitaka ndio sababu mojawapo inayochelewesha haki kutolewa kwa wakati. 

Wakati mwingine suala hili linachelewesha haki kutolewa mapema kwa sababu ya wahusika kutokuwa makini na wakati mwingine kuwa wabishi hata wanapokuwa wameishaoneshwa ukweli. 

Wakati kama huo, Mahakama hulazimika kuingia katika kusikiliza kesi ndogo ndani ya kesi ya msingi jambo ambalo huchelewesha maamuzi

Pia alisema kuwa ucheleweshwaji wa kuanza kutumika sheria ya kuwaruhusu mawakili kuwatetea wateja wao kwenye Mahakama za Mwanzo ni sababu nyingine inayofanya mashauri kurundikana mahakamani pamoja na mahabusu. 

Hivi sasa mahakama za mwanzo zina mahakimu waliohitimu shahada ya sheria na kuajiriwa katika kada ya Mahakimu Wakazi na baadhi yao wana shahada za uzamili na hivyo bila ya shaka wana uwezo mkubwa. 

Alisema kuwa Kuendelea kuwazuia mawakili kufanya kazi katika mahakama za mwanzo kunasababisha mashauri ambayo yangemalizika katika hatua hiyo, kuendelea kwenye mahakama za juu kwa njia ya rufani au marejeo na hivyo kuwafanya wahusika waendelee kujenga vibanda mahakamani. 

“Tunaomba Bunge liingilie kati mapema ili kunusuru hali hii…,” alisema Kaijage.

Mwisho









TLS: INDUSTRIALIZATION DRIVE WILL NOT BE ATTAINED IF THE COURT PROCEEDINGS WILL TAKE LONG TIME TO FINISH



Jaji Mfawidhi, Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Iringa, Jaji Mary Shanghali akiteta neno na Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Christopher Ole Sendeka na Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Richard Kasesela katika maadhimisho ya Siku ya Sheria nchini yaliofanyika kwenye viwanja vya Makahama Kuu ya Iringa juzi. (Picha na Friday Simbaya)





Mwenyekiti wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) Rwezaula Kaijage akisoma hotuba iliyoandaliwa na Mawakili wa kujitegemea Kanda ya Mahakama Kuu ya Iringa katika maadhimisho ya Siku ya Sheria nchini yaliofanyika kwenye viwanja vya makahama kuu ya Iringa juzi. (Picha na Friday Simbaya)



IRINGA: THE Chairman of Tanzania Law Society (TLS) Iringa Chapter, Rwezaula Kaijage says Tanzania will not accelerate in industrialization efforts when court proceedings take months and even years to finish. 


Kaijage made the appeal on Thursday during a law day ceremony held at Iringa zone High Court grounds in Iringa Region. 


He said that Tanzania's industrialization drive will not be possible if proceedings will take months and even years without finishing, which their perpetrators and witnesses come to court every time and stop their economy activities. 


He said defendants and witnesses waste much time in court when their farming activities, trade and economic is standing.


He said that to Tanzania judiciary in collaboration with its partners should take several steps to ensure that the court proceedings should not take a long time to finish, hence economic growth.


"In our region of Iringa, we have a good example of Kilolo District, it has a District Court but it does not have the prison and OCD’s head office of the district police is almost seventy kilometers from the district headquarters," he said.


He said that this situation has made the district to organize for listening criminal proceedings for two days in a week and this is due to the limited capacity of the district police chief of transporting inmates from prison to Kilolo in Iringa.


“We have seen once the chief of police was unable to find transportation to bring detainees to court when witnesses have been prepared, "said Kaijage.


However, he said that the legal argument among the parties or lawyers who defended suspects; either among independent lawyers and prosecutors is one of the reasons given for a slow dispensing of legal rights 


He also said that a delay in the entry into force of the law to allow lawyers to defend their clients in primary courts is another reason why the heavy backlog in court cases.


Currently the primary court magistrates who have graduated with a degree in law and a cadre of judges employed some of them have master's degrees and it will certainly have great potential.


He said that lawyers continue to prevent them from working in the lower courts which causes court cases to piled up thus make the characters continue to build huts at court.


Judge in Charge, High Court of Tanzania's Iringa Region, Judge Mary Shanghali said Iringa High Court which comprises Njombe region are now 1,777 cases.


She said that Out of these cases, they have only 211 cases a year more than two (2) which is between 123 Criminal proceedings (murder) and 87 cases of assertions.


Judge Shanghali said this yesterday during a ceremony on law day held at High Court of Tanzania's Iringa zone grounds. She said that in all other cases 1,566 are under the age of two years (2).


"Statistics show that eight percent (8%) of long outstanding cases for the whole country," said Judge Shanghali.


She added that the court is obliged to carry out its role of justice at the time and counsel heard and resolved in time without delay.


The Tanzania judiciary has been organizing “Law Day” every year where they bring together judicial stakeholders to provide legal education and legal aid services to the community and to observe the start of the court calendar.


On her part, Iringa Regional Commissioner (RC), Amina Masenza said that the rights given to citizens when they make their development activities are free and efficiently.


"If right is delayed, development cannot be achieved because the country will not be free to carry out their activities fully and thus diminish the pace of development," said Masenza.


She said that Article 11 of the Constitution of the United Republic of Tanzania gives every citizen the right to work hard and that everyone will live with his sweat.


RC said that the Court is the constitutional authority of the administration of justice and to foster economic growth and strive to apply its best to speed up as much as the right to promote the rapid development in the country.


"We have seen the backlog of cases in court, Detective take long, the backlog of suspects in custody, proceedings take a long time without reasonable grounds, stringent bail," said Masenza.


Regional Commissioner asked for all entities involved in the administration of justice (police, Judges, lawyers and, Government Officials, All staff cooperate with the Court in order to stimulate the development rights).


Saturday, 4 February 2017

MISA-TAN YAWAKUTANISHA WABUNGE NA WANAHABARI...




Mhariri Mtendaji wa The Guardian Ltd, Jesse Kwayu akiwasilisha mada kuhusu namna ya kufanya mahusiano ya kikazi kati ya bunge na wanahabari kwa baadhi ya wabunge, wahariri na waandishi wa habari katika ukumbi wa Hazina Ndogo mjini Dodoma. Picha na Geofrey Adroph




Afisa Habari na Utafiti wa MISA-Tanzania, Sengiyumva Gasirigwa akizungumza jambo mbele ya baadhi ya wabunge pamoja na baadhi ya wahariri na waandishi wa habari waliofika katika semina ili kujadili jinsi ya kutengeneza mahusiano ya kikazi kati ya Bunge na wanahabari yatakayoleta ukaribu kwa pande zote.









Baadhi ya wabunge wakichangia mada kuhusu kutengeneza mahusiano ya kikazi kati ya Bunge(wabunge) na wanahabari pamoja na kutoa maoni yao ili kuboresha utoaji wa habari kwa wananchi boila kujali itikadiza kivyama.


Mhariri Mtendaji wa The Guardian Ltd, Jesse Kwayu akijibu maswali kutoka kwa wabunge katika mkutano uliowakutanisha wabunge, wahariri na waabdishi wa habari katika ukumbi wa Hazina Ndogo mjini Dodoma leo.



Mhariri mtendaji wa Jamhuri Media, Deodatus Balile akitolea ufafanuzi baadhi ya maswali yaliyoulizwa na waandishi pamoja na wabunge walioudhuria mkutano huo uliofanyika katika ukumbi wa Hazina ndogo mjini Dodoma. 



Mmoja wa waandishi wa habari akitoa changamoto anazozipata kwenye kazi zake za kila siku za kuripoti habari mbalimbali







Baadhi ya wabunge, wahariri na waandishi wa habari wakiwakwenye mkutano 



Taasisi ya Vyombo vya Habari Kusini mwa Afrika (MISA) tawi la Tanzania kwa kushirikiana na Wakfu wa Taasisi Huru za Uwazi Afrika (OSIEA) wamewakutanisha wabunge pamoja na waandishi wa habari leo katika ukumbi wa Hazina Ndogo mjini Dodoma. 

Mkutano huu ulikuwa na lengo la kuwajengea Wabunge na Wanahabari uhusiano mzuri katika utendaji wao wa kazi. Bunge na Vyombo vya Habari ni Mihimili miwili ya dola (Mmoja ukiwa Rasmi na mwingine usio Rasmi) inayotegemeana sana katika utendaji wake wa kazi.


Kutokana na kazi kubwa ya Bunge ambayo ni kutunga sheria na kuwakilisha Umma katika mijadala mbalimbali ya maendeleo katika ngazi za Taifa na Jimbo lazima kutumia vyombo vya Habari kwenye kazi ya kutafsiri mipango na mikakati mbalimbali inayofanywa na Bunge katika lugha ambayo mpiga kura/mwananchi wa kawaida anaweza kuelewa. Lengo kuu likiwa ni kuharakisha maendeleo ya mtu mmoja mmoja na jamii nzima.


Katika siku za karibuni kumetokea changamoto mbalimbali katika utendaji kazi wa muhimili huu rasmi na muhimili huu usiokuwa rasmi, na hasa kutoaminiana na kushutumiana kwa namna moja ama nyingine. Kutokana na changamoto hizo hakuna budi kwawaandishi wa habari paamoja ili kujadili changamoto na kuja na suluhisho la changamoto hizo.


Semina hiyo imeshirikisha watu 55 ikiwa ni pamoja na wabunge mbalimbali toka vyama vyote, Wahariri wa vyombo Habari vilivyoko Dodoma na Bureau Chiefs wa vyombo vya Umma na Binafsi vilivyopo Dodoma.


MAGARI MANNE YAGONGANA BARABARA YA NYERERE ENEO LA MTAVA JIJINI DAR ES SALAAM




Wananchi wakimuangalia dereva wa teksi aliyejeruhiwa baada ya gari lake lenye namba za usajili T 625 AWS kugongana na gari dogo lenye namba usajili T 214 CFX wakati likiingia barabara ya Nyerere likitokea Jengo la Kibiashara la Quality Centre Dar es Salaam leo asubuhi.



Mwonekano wa Teksi hiyo namba T 625 baada ya kugongana.



Wananchi wakiangalia ajali hiyo.


Wananchi wakiangalia gari dogo aina ya Toyota Corolla lenye namba T 214 CFX baada ya kuyagonga magari namba T 741 DEK na T 596 BCG katika eneo hilo la Mtava.



Askari wa Usalama Barabarani akipima ajali hiyo.



Gari dogo aina ya Toyota Corolla lenye namba T 214 CFX likiwa eneo la ajali kabla ya kuondolewa.






Na Dotto Mwaibale

DEREVA wa gari dogo teksi yenye namba za usajili T 625 AWS amenusurika kufa baada ya gari lake alilokuwa akiliendesha kutoka mjini akielekea Uwanja wa Ndege kugongana na gari dogo lenye namba T 214 CFX aina ya Corolla lililokuwa likiingia Barabara ya Nyerere likitokea Jengo la Biashara la Quality Centre eneo la Mtava jijini Dar es Salaam leo asubuhi.


Mashuhuda wa ajali hiyo wakizungumza na waandishi wa habari eneo la ajali walisema ajali hiyo ilisababishwa na gari hilo dogo aina ya Corolla lililokuwa likiingia barabara ya Nyerere bila kuchukua tahadhari.


"Chanzo cha ajali hii ni gari hilo dogo aina ya corolla ambalo liliingia barabara ya Nyerere bila ya dereva wake kuchukua tahadhari na kama dereva wa gari namba T 625 AWS angekuwa katika mwendo wa kawaida madhara yake yasingekuwa makubwa kiasi hicho" alisema shuhuda aliyejitambulisha kwa jina la Mlugulu.


Mlugulu alisema baada ya magari hayo kugongana gari hilo aina ya Corolla liligeuka na kwenda kuyagonga magari mengine namba T 596 BCG na T 741 DEK yaliyokuwa yamesimama yakisubiri kuingia upande ambao lipo Jengo la Kibiashara la Quality Centre.


Katika ajali hiyo gari namba T 625 AWS liliacha njia na kuhamia upande wa pili wa barabara ya kutoka Tazara kwenda mjini.


Baada ya ajali askari wa usalama barabarani walifika na kupima ajali hiyo na kuchukua maelezo ya madereva wote wanne ambapo magari mawili T 214 CFX na T 625 AWS yakiondolewa na magari ya kukokota magari mabovu (Breck Down) na kupelekwa kituo cha Polisi cha Chang'ombe Temeke jijini Dar es Salaam kwa hatua zingine za kisheria.

Friday, 3 February 2017

Improving Economic Opportunities For Youth Through Agriculture


By Friday Simbaya, Kilombero

The agriculture sector in Tanzania struggles to attract younger generations. For many youth (ages 18-35), farming fails to offer profitable economic opportunities and attractive environments in which to live and work, says Thomas Carr Chief of Party, NAFAKA.

He said that cultural traditions that grant land control primarily to the patriarch further limit access by younger family members, which has also contributed to the migration of younger generations to urban centers where they perceive the quality of life and earning potential to be better.

The NAFAKA Chief of Party, Carr said recently that Tanzanian Staples Value Chain (NAFAKA) is aimed improving the impact this generational shift could have on the future of Tanzanian agriculture, the USAID Feed the Future Initiative has been working with rural youth groups to create new economic opportunities in the agriculture sector.

He said providing services to farmers, such as weeding and spraying, not only further enhances the productivity of the entire agriculture sector but also creates new jobs well suited for younger generations. 

By facilitating training to youth groups on Good Agricultural Practices (GAP) like land preparation, proper planting and spacing, crop management, and post-harvest handling, the project has initiated renewed interest in agriculture and provided youth with important techniques that benefit the entire sector.

At least seventeen (17) youth groups have already been formed with a total of 220 members. Presently, forty-three of those members (51% female) have begun offering services to farmer customers.

One such group that has benefited from training is Huduma Youth Group in Mlimba (Kilombero District). 

The group’s 10 members (50% female) have already generated a total of $1,280 working as agricultural service providers within their community.

Carr said that members are hired to perform spraying services, transplanting, direct seeding, and weeding activities. 

The group invested 70% of its profit into the purchase of one acre of shared land, four spraying pumps, and three dribblers and collectively decided to divide the remaining 30% among themselves for individual use. 

Currently, the group has 21 regular clients and has delivered services on 50 total acres of land. The group has also established a group development fund worth $163 to manage personal emergencies or natural disasters.

Ester Oscar Kiyule, chairperson of Huduma Youth Group, explained, “Working as a group has helped many of our members believe that they can be someone reliable to many. I am very excited that I am role model for other youth in our community.”

Through this initiative, a wider range of economic opportunities in the agriculture sector are being developed, creating jobs for youth in rural areas, establishing linkages that strengthen agricultural value chains across, and sustaining the future of the agriculture sector in Tanzania.

The NAFAKA Staples Value Chain Activity is a six-year Task Order issued by USAID under the Tanzania Feed the Future (FtF) Initiative and administered by ACDI/VOCA. 

NAFAKA integrates agricultural, gender, environmental, and nutritional development efforts to improve smallholder farmer productivity and profitability within the rice and maize value chains in Morogoro (Kilombero and Mvomero districts), Dodoma (Kongwa district), Manyara (Kiteto district), Mbeya (Mbozi, Mbeya Rural, Mbarali, and Rungwe districts), and Iringa (Iringa Rural and Kilolo districts) on the mainland, as well as Pemba and Unguja in Zanzibar. 

NAFAKA’s goal is to sustainably reduce poverty and food insecurity by increasing incomes for smallholder farmers, including men, women, and

The program is part of Feed the Future, the US government’s global hunger and food security initiative to break the cycle of hunger and poverty in the developing world. 

Feed the Future is focusing on the Southern Agricultural Growth Corridor (SAGCOT), a region the Tanzanian government has identified as the most conducive for agricultural growth.

End



WATOTO WAITAKA SERIKALI KUTUNGA SHERIA KALI ...

Na Friday Simbaya, Mufindi  Wanafunzi wa shule za msingi na sekondari wilayani Mufindi mkoani Iringa wameiomba serikali kwa kush...