Saturday, 25 July 2015

UWT CCM MKOA WA IRINGA WACHAGUANA


Rose Tweve

Ritta Kabati

Lediana Mng'ong'o

wajumbe

Zainabu Mwamwindi

wagombea

UMOJA wa Wanawake wa Tanzania (UWT) mkoa wa Iringa umekataa kumuongezea kipindi kingine cha miaka mitano bungeni, Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Iringa, Lediana Mng’ong’o (58) katika mkutano wake wa kura za maoni uliofanyika juzi, mjini Iringa.


Mng’ong’o ambaye pia alikuwa mmoja wa wenyeviti wa bunge la 10 linalomazima muda wake amekuwa mbunge wa viti maalumu mkoa wa Iringa kwa miaka 15.

Friday, 24 July 2015

Kibiki aikumbuka Lipuli, asema ni agenda yake akipata Ubunge




NA MWANDISHI WETU, IRINGA

MGOMBEA wa nafasi ya Ubunge kwa tiketi ya CCM, Mwanahabari Frank Kibiki ameahidi kushirikiana na wadau wa soka kupandisha daraja timu ya soka ya Lipuli ya mjini Iringa iwapo atapewa ridhaa ya kupeperusha bendera ya CCM katika uchaguzi mkuu ujao.

BHALALUSESA ASISITIZA UMUHIMU WA UMAHIRI KATIKA TEHAMA



Kiongozi wa kitaifa wa mradi wa CFIT, Prof. Ralph Masenge akimkaribisha mgeni rasmi Kaimu Kamishina wa Elimu, Benjamin Kulwa (hayupo pichani) kufungua kongamano linalohusu upitiaji wa waraka wa mafunzo ya Tehama kwa wakufunzi wa vyuo vya ualimu linalofanyika mjini Bagamoyo.


Kaimu Kamishina wa Elimu, Benjamin Kulwa akisoma hotuba kwa niaba ya Kamishina wa Elimu, Profesa Eustella Bhalusesa wakati akifungua rasmi kongamano linalohusu upitiaji wa waraka wa mafunzo ya Tehama kwa wakufunzi wa vyuo vya ualimu linalofanyika mjini Bagamoyo. Kulia ni Ofisa Miradi ya Mawasiliano, Habari na Tehama wa Shirika la Kimataifa la Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) nchini, Al Amin Yusuph.

Na Mwandishi wetu, Bagamoyo

KAMISHINA wa Elimu, Profesa Eustella Bhalalusesa amesisitiza haja ya kuhakikisha kwamba viwango vya umahiri vya Tehama kwa wakufunzi wa vyuo vya ualimu nchini vinakua vya juu kukidhi haja ya matumizi ya kufundishia na kujifunza nchini.

Alitoa kauli hiyo mjini hapa wakati akifungua kongamano linalohusu upitiaji wa waraka wa mafunzo ya Tehama kwa wakufunzi wa vyuo vya ualimu.

Thursday, 23 July 2015

KUMEKUCHA WATIA NIA WASHUTUMIANA KWA RUSHWA JIMBO LA IRINGA MJINI


Watia nia Jimbo la Iringa Mjini kushoto ni Peter Mwanilwa, Micheal Mlowe, Mahamudu Madenge, Dk. Yahaya Msigwa, Frank Kibiki na Frederick Mwakalebela wakati wakiongea na waandishi wa habari kuhusu ukiukwaji wa kanunu za uchaguzi wa CCM.





Madenge (katikati) akisoma kanunni hizo kwa wanahabari

WAKATI Joto la uchaguzi likishuka na kupanda mkoani Iringa kada wa chama chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Iringa ambaye pia ni Mwenyekiti wa CCM Mkoa huo na mtia nia kugombea ubunge wa jimbo la Iringa Mjini kwa tiketi ya chama cha mapinduzi CCM, Jesca Msambatavangu ametuhumiwa na makada wenzake wa chama hicho kwa kutoa rushwa kinyume na matakwa ya maadili na kanuni ya chama hicho.

Msambatavangu ametuhumiwa na makada wenzake 11 kati ya 13 ambao wameomba ridhaa ya kuwania kugombea ubunge jimbo la Iringa Mjini kwa tiketi ya CCM .

TOP JOBS FOR THIS WEEK







S/No. COMPANY NAME JOB LINK



3. RELIANCE INSURANCE COMPANY TANZANIA LTD http://www.brightermonday.co.tz/jobs/branch-manager-66




7. THE INTERNATIONAL RESCUE COMMITTEE (IRC) TANZANIA http://www.brightermonday.co.tz/jobs/monitoring-evaluation-coordinator


HERE COMES WOMEN’S EMPOWERMENT SHOW, SUCCESSFUL WOMEN IN THE SPOTLIGH











Educate, Empower and Inspire is a women’s empowerment show. The aim of this show is to put successful women in the spotlight and get a glimpse as to how they are making a difference to our society and how they can inspire others to do the same.

My first guest was Dr. Trish Scanlan who runs the paediatric oncology department at Muhimbili hospital. Since her involvement in 2008, along with her dedicated team of Tanzanian doctors and nurses, the short term survival rates of children with cancer rocketed from 12% to 60%.

UN YAKANUSHA UZUSHI WA JAMII FORUM NA INDIAN OCEAN NEWSLETTER



Mratibu wa mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini Tanzania na Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Mipango ya maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Bw. Alvaro Rodriguez.

UMOJA wa Mataifa umetaka vyombo vya habari vya kitaifa na kimataifa kuhakikisha vinatoa taarifa zao kwa usahihi kuhusu maandalizi ya uchaguzi na uchaguzi wenyewe.

Kauli hiyo imetolewa na Ofisi ya Umoja wa Mataifa Dar es salaam, kufuatia taarifa iliyochapishwa na jarida moja kwamba UN inataka kujitoa katika kusaidia mandalizi ya uchaguzi nchini Tanzania.

Wednesday, 22 July 2015

Violence against journalists: finding the media’s role in reporting press freedom violations




Carolina Morais Araujo | July 15, 2015

The increasing violence against journalists around the world is worrisome. So far 33 journalists have been killed this year, for reasons directly connected to their job, the Committee to Protect Journalists (CPJ) reports.

Impunity has been the rule after most of these murders: CPJ says that 90 percent of the 370 killings of journalists in the past ten years did not result in a conviction. While international and non-governmental organizations consider new approaches to combat this problem, the role of the media in this process is rarely discussed.

It may be, though, that journalists have a role to play in protecting their own. By covering violations of press freedom and cases of violence against journalists, the media can raise awareness and perhaps make conditions safer by pressuring governments to act.

As part of its advocacy work on press freedom and safety, the Open Society Foundation’s Program on Independent Journalism commissioned research by a group of four students at Columbia University’s School of International and Public Affairs (SIPA) to analyze press coverage of journalists safety in five different regions. 

Tuesday, 21 July 2015

WATIA NIA WAKIJINADI KWA WANACHAMA KATA YA KIHESA

Dkt. Yahaya Msigwa akijinadi kwa wanachama la shule ya msingi kihesa katika jimbo la iringa mjini leo.


Frederick Mwakalebela akijinadi kwa wanachama la shule ya msingi kihesa katika jimbo la iringa mjini leo.

Addo November Mwaisongwe akijinadi kwa wanachama la shule ya msingi kihesa katika jimbo la iringa mjini leo.

Balozi mstaafu Augustine Philip Mahiga akijinadi kwa wanachama la shule ya msingi kihesa katika jimbo la iringa mjini leo.


Jesca Msambatangu akijinadi kwa wanachama la shule ya msingi kihesa katika jimbo la iringa mjini leo.

FALES KIBASA

Mgombea ubunge Iringa Mjini kupitia CCM, Peter Mwanilwa


WANACHAMA 13 wa Chama cha Mapinduzi (CCM) wanaotaka ubunge katika jimbo la Iringa Mjini wanaendelea kujinadi kwa wanachama wa chama hicho katika matawi 81 kwa kushindanisha mikakati yao ya kulikomboa jimbo hilo na kuwaletea wananchi wake maendeleo.


Kwa miaka mitano iliyopita jimbo hilo limeongozwa na Mchungaji Peter Msigwa aliyechaguliwa kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).


Mbali na kuwashirikisha wanachama wake wote, kampeni hizo ambazo tayari zimefanyika katika matawi ya kata za Nduli na Kihesa na leo Mkwawa zimewavutia pia wafuasi wa baadhi ya wagombea hao.

Monday, 20 July 2015

THE STARS BAND YAZINDULIWA RASMI SIKU YA EID MOSI NDANI YA MZALENDO PUB HUKU IKISINDIKIZWA NA BENDI YA FM ACADEMIA PAMOJA NA BARNABA




Bendi mpya ya muziki wa dansi ijulikanayo kama The Stars Band iliyo chini ya Aneth Kushaba imezinduliwa rasmi siku Jumamosi ya Julai 18, siku ya Idd-Mosi ndani ya kiota cha Mzalendo Pub, Kijitonyama jijini Dar es Salaam huku ikisindikizwa na mwanamuziki wa muziki wa kizazi kipya Barnabas pamoja na bendi ya FM Academia ‘Wazee wa Ngwasuma’. 




Mkurugenzi wa The Stars Band, Aneth Kushaba akijitambulisha kwa mashabiki wakenm pamoja na azungumza na wapenzi wa bendi mpya ya The Stars Band wakati wa uzinduzi yeye binafsi alisema hawezi kusema yaliyopita bali wapenzi wa bendi hiyo wategemee makubwa kutoka kwenye bendi hiyo iliyozinduliwa siku ya Idd Mosi ndani ya kiota cha Mzalendo Pub






Mwimbaji wa Bendi ya The Stars, Felly Kano akionesha mambo yake kwenye stage hii yote ni wakati anajitambulisha kwa mashabiki wa bendi waliofika kwenye uzinduzi wa bandi hiyo

WATOTO WAITAKA SERIKALI KUTUNGA SHERIA KALI ...

Na Friday Simbaya, Mufindi  Wanafunzi wa shule za msingi na sekondari wilayani Mufindi mkoani Iringa wameiomba serikali kwa kush...