Monday, 9 May 2016

UVUNJAJI WA SHERIA



Pamoja kwamba kuna kibao kinachokataza kutofanya  shughuli zozote zile katika ofisi ya maliasili na utalii,  wananchi hao walikutwa wakutenganeza gari eneo hilo bila kujali ilani ya kibao kama mpigapicha wetu alivyowakuta wakifanya shughuli katika Mtaa ya Ujasili (Ujasili Road) Mlangege Gereji Manisapaa ya Iringa, mkoani Iringa.

AZANIA BENKI YASHEREHEKEA SIKU YA MAMA KWA KUGAWA DAWA NA VIFAA VYA USAFI HOSPITALI YA AMANA


Mkurugenzi wa Mikakati na Biashara wa Benki ya Azania, Mwanahiba Mzee (kulia), kwa niaba ya mkurugenzi mkuu wa benki hiyo, akimkabidhi kiongozi wa wagonjwa wa ndani wa Hospitali ya Rufaa ya Amana, Francis Yango (kushoto), dawa na vifaa vya usafi vyenye thamani ya sh.milioni 5 vilivyotolewa na benki hiyo ikiwa ni kuadhimisha siku ya wanawake Dar es Salaam leo asubuhi. Wapili kulia ni Muuguzi wa zamu,Getrude Massawe na Antusa Lasway.

Wafanyakazi wa benki ya Azania wakiwa mbele ya vifaa na dawa walivyotoa msaada kwa Hospitali hiyo.
Hapa ni furaha tupu kabla ya kukabidhi msaada huo.




Mwonekano wa maboksi yenye msaada huo baada ya kupokelewa.
Vifaa hivyo vikipelekwa kwa walengwa.
Mkurugenzi wa Mikakati na Biashara wa Benki ya Azania, Mwanahiba Mzee (kushoto), akimkabidhi dawa za meno na sabuni, Judith Kimei katika wodi ya wazazi. Kulia ni Muuguzi wa zamu Antusa Lasway.

Ofisa wa benki hiyo, Neema Tumsifu akimjulia hali mtoto aliyezaliwa katika wodi hiyo.
Ofisa wa benki hiyo, Valentina Chesama akimjulia hali mtoto aliyezaliwa katika wodi hiyo.

Wafanyakazi hao wa Bebki ya Azania wakiondoka Hospitalini hapo baada ya kukabidhi msaada huo.




BENKI ya Azania imetoa msaada wa dawa na vifaa vya usafi vyenye thamani ya sh. milioni 5 katika Hospitali ya Rufaa ya Amana Ilala Jijini Dar es Salaam ikiwa ni maadhimisho ya siku ya wanawake duniani.

Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa benki hiyo wakati wa kukabidhi msaada huo Dar es Salaam leo asubuhi, Mkurugenzi wa Mikakati na Biashara, Mwanahiba Mzee alisema kila mara benki hiyo imejiwekea utaratibu wa kusaidia jamii kulingana na ratiba yao ambapo mwaka huu waliona ni vema msaada huo waupeleke Hospitali hiyo.

Alisema mwaka katika kusherehekea sikukuu ya wanawake waliona ni vema kutoa msaada hasa katika wodi ya wajawazito ukizingia kuwa sikukuu hiyo inawahusu.

"Tumetoa msaada wa dawa mbalimbali kama dettol, spiritis, mabomba ya sindano, micoprostol, vitamini k na nyingine nyingi pamoja na vifaa vya usafi kama vile mifagio, sabuni na dawa za mswaki" alisema Mzee.

Kiongozi wa wagonjwa wa ndani wa Hospitali hiyo, Francis Yango akizungumza wakati wa kupokea msaada huo kwa niaba ya Mganga Mkuu, Shadrack Shimwela aliishukuru benki hiyo na kuwataka wadau wengine kujitokeza kusaidia.


"Tunawashukuru sana Azania Bank Ltd kwa msaada wenu lakini tunawaomba muende mbele zaidi kama mtaweza mtujengee walau wodi ambayo itaingiza walau vitanda 30 na wodi hiyo muandike jina la benki yenu kwani changamoto kubwa tulionayo kwa sasa licha ya kuwa na vitanda vya kutosha tuna uhaba wa wodi" alisema Yango.

HATIMAYE CHAMA CHA ADC CHAFANYA MKUTANO MKUU,MSAJILI AWAMWAGIA PONGEZI


Waziri wa kilimo wa serikali ya mapinduzi ya Zanzibar amnbaye ni mlezi wa chama cha ALLIANCE FOR DEMOCRATIC CHANGE -ADC nchini Tanzania Mh HAMAD RASHID akihutubia wajumbe wa mkutano mkuu wa chama hicho unaofanyika Jijini Dar es salaam leo(Picha na EXAUD MTEI)

Baada ya chama cha ALIANCE FOR DEMOCTARIC CHANGE –ADC kuingia katika migogoro ya kiuongozi ndani ya chama hicho siku za hivi karibuni Hatimaye hali ya Amani imerejea ambapo chama hicho leo kimeingia katika mkutano mkuu uliowakutanisha wajumbe mbalimbali kutoka kila kona ya nchi.


Katika mkutano ambao umehudhuriwa na viongozi wakuu wa chama hicho akiwemo waziri wa kilimo wa serikali ya Zanzibar ambaye alikuwa mgombea Urais wa Zanzibar kwa tiketi ya chama hicho ambaye pia ndiye mlezi wa chama Mh HAMAD Rashid,viongozi kutoka ofisi ya msajili wa vyama vya siasa na wajumbe mbalimbali wa chama hicho.
Makamu mwenyekiti wa ADC Mama ADELA STOLIC akihutubia wakati akifungua mkutano huo Mkuu mapema leo

Akizngumza wakati wa Ufunguzi wa mkutano huo HAMAD RASHID amesema kuwa chama cha ADC ni chama ambacho kimeanzishwa kwa ajili ya kuwasaidia watanzania,kikiwa na itikadi zake,sera zake na mipango yake hivyo hakipo tayari kufwata sera za chama kingine chochote nchini na swala la kushiriki chaguzi mbalimbali ni moja kati ya sera zao hivyo hawapo tayari kususia uchaguzi wa aina yoyote kwani ndio njia pekee ya kupata viongozi wa nchi.
Msajili Msaidizi wa vyama vya siasa nchini A SISTY LEORNAD NYAHOZI akitoa hotuba fupi kwa niaba ya msajili wa vyama vya siasa nchini 

Ameleza kuwa chama chake kimeanza mipango kabambe ya kujiimarisha Zaidi kwa lengo la kuwaletea mabadiliko ya kweli watanzania baada ya wapinzani wao waliokuwa wakiongoza serikali iliyopita na sasa hawapo kushindwa kufanya hivyo kwa miaka yote iliyopita hivyo amewataka watanzania kuanza kukiamini chama cha ADC kwani ndio dira pekee ya mabadiliko kwa watanzania kwa sasa.
Akizungumzia kuhusu upatikanaji wa viongozi wa chama hicho mara baada ya kuondolewa kwa aliyekuwa mwenyekiti wa chama kiongozi huyo amewataka wanachama wa chama hicho wakae tayari kwa kuwa siku yoyote chama kitaitisha uchaguzi wa kupata viongozi wapya.

Naye msajili msaidizi wa vyama vya siasa nchini Mh SISTY LEORNAD NYAHOZI akizungumza katika mkutano huo amekipongeza chama hicho kwa kukubali kuingia katika uchaguzi wa marudio Visiwani Zanzibar ambapo walishika nafasi ya pili kwa kupata asilimia 3 jambo ambalo amesema ni ukomavu wa kisiasa kwa chama kichanga kama hicho kushiriki uchaguzi mkubwa kama ule na kupata mafanikio hayo.

Aidha amesema kuwa chama hicho kimeonyesha ukomavu Zaidi baada ya kutokea mtafaruku na aliyekuwa mwenyekiti wa chama hicho na kufanikiwa kulimaliza kidemocrasia jambo ambalo amesema linafaa kuigwa na vyama vingine vya siasa nchini.
Chama hicho kilijikuta katika migogoro iliyosababisha hadi kutimuliwa kwa aliyekuwa mwenyekiti wake SAID MIRAAJ kwa kile kiliichoitwa kukiuka matakwa katiba ya chama ambapo ilielezwa kuwa mwenyekiti huyo alipinga kitendo cha viongozi wa chama kuingia katika uchaguzi wa Zanzibar wa marudio jambo ambalo alilipinga na kusababisha mtafaruku baina yake na aliyekuwa mgombea wa chama hicho visiwani Zanzibar ambaye kwa sasa ni waziri HAMAD RASHID

TIGO YASHIRIKIANA NA MADEREVA WA BODABODA UKEREWE



Mkuu wa Wilaya ya Ukerewe Joseph Mkirikiti,akihutubia madereva bodaboda wa wilaya yake jana wakati wa uzinduzi wa ushirikiano wa madereva hao na mtandao wa Tigo kwa ajili ya utendaji wao wa kutoa huduma ya usafiri ,Wa pili toka kulia ni Mkurugenzi wa Tigo Kanda ya ziwa, Ali Maswanya na Mkurugenzi wa Mikakati wa Tigo Kobbina Awuah(kulia)


Mkurugenzi wa Kanda ya ziwa wa mtandao wa Tigo Ali Maswanya, akizungumza wakati wa kuzindua ushirikiano wao na madereva Bodaboda Wilaya ya Ukerewe jana, kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Ukerewe Joseph Mkirikiti na Mkurugenzi wa Mikakati wa Tigo Kobbina Awuah(kulia)



Madereva Bodaboda Wilaya ya Ukerewe Mkoani Mwanza,wakinyoosha mikono juu kuashilia kuzinduliwa kwa umoja wao na Mtandao wa Tigo,kwenye hafla iliyofanyika 



Baadhi ya bodaboda zikiwa nje ya eneo hilo la ukumbi wa Mmikutano Ukewe.


Sunday, 8 May 2016

MATUMIZI BORA YA ARDHI YA KIJIJI NDIO TIBA YA MIGOGORO YA ARDHI NCHINI

Wajumbe wa PLUP na VLUMC wakichukua jira za ardhi kwa kutumia GPS

Picha ya pamoja ya wajumbe wa kamati ya ardhi (VLUMC), halmashauri ya kijiji cha Mbweleli (VC) na  timu ya PLUP.


Mwakilishi kutoka shirika la WWF Ebrania Mlimbila akitoa neno la shukrani kwa wajumbe kamati ya ardhi (VLUMC) na wale wa halmashauri ya cha Mbweleli, kata ya Migoli, tarafa ya Ismani baada kumalizika kwa mafunzo ya matumizi bora ya ardhi. Kushoto ni mwezeshahaji (PLUP) Godfry Mwanga ambaye pia ni rasimu ramani (Cartographer) kutoka Halmamshauri ya Wilaya ya Iringa, mkoani Iringa.



Washiriki wa Mafunzo ya Matumizi bora ya ardhi ya kijiji (VLUP) ambao wanaunda kamati ya usimamizi wa ardhi (VLUMC) na halmashauri ya kijiji cha Mbweleli kata ya Migoli , tarafa ya Ismani wilayani Iringa, mkoani Iringa wakichangamsha Miili yao wakati wa mafunzo hayo ya kuwajengea uwezo. Mafunzo hayo ya mpango wa matumizi bora ya ardhi ya kijiji wa miaka kumi (2016-2026) yamefadhiliwa na shirika la WWF kupitia program ya maji Ruaha (RWP) kwa kushirikiana na halmashauri ya wilaya ya Iringa.


Sadiq Khan's London mayoral win gives Jeremy Corbyn reason to be cheerful

Election of first Muslim mayor of major western capital promises to offset big losses in Scotland as SNP maintains grip on Holyrood




Sadiq Khan’s election as London mayor in the early hours of Saturday handed a boost to Labour leader Jeremy Corbyn at the end of a difficult day in which Labour held ground in England but endured a disastrous defeat in its former heartland of Scotland.

Khan’s landslide victory over his rival, Conservative Zac Goldsmith, in which he secured more than 1.3m votes made him the first Muslim mayor of a major western capital, and gave Labour the keys to City Hall after eight years of Conservative control, following a bitterly fought and controversial campaign.

UK elections: Sadiq Khan confirmed as London mayor
• Khan beats Goldsmith in London
• Scottish Labour beaten to third place after Tory surge


As the votes were being counted, senior Tories and even Goldsmith’s own sistercriticised his team’s strategy, which included repeated claims from the candidate himself and David Cameron that Khan had shown bad judgment by sharing platforms with alleged extremists.

The former Conservative party chairman Sayeeda Warsi attacked the Goldsmith campaign on Twitter, claiming: “Our appalling dog whistle campaign for #LondonMayor2016 lost us the election, our reputation & credibility on issues of race and religion.”

Steve Hilton, Cameron’s former director of strategy who was part of an effort to “detoxify” the Tories, told BBC Newsnight that Goldsmith had brought back the “nasty party label to the Conservative party”.

Speaking after finally being declared winner after midnight, Khan said that he grew up on a council estate and “never dreamt that someone like me could be elected as mayor of London”.



He highlighted his positive campaign before making a pointed attack on Goldsmith. “I am so glad that London has chosen hope over fear and unity over division. The politics of fear is simply not welcome in our city.”

Goldsmith thanked his team and admitted he was disappointed but failed to address the accusations.

The row could be uncomfortable for the prime minister, who used the line of attack more than once in the House of Commons.

 
Zac Goldsmith’s campaign has been attacked by senior Tories. Photograph: Andrew Parsons/i-Images

Jemima Goldsmith questioned the tactics, saying they did not reflect the “eco-friendly, independent-minded politician with integrity” she knew her brother to be.

But underlining the hostility the new mayor could face once he takes up office, the candidate for Britain First, Paul Golding, turned his back in protest as Khan made his acceptance speech at City Hall. “Britain has an extremist mayor!” shouted a member of Golding’s team.

Corbyn congratulated Khan at the end of a day of results across the UK that were not bad enough to trigger a coup against the Labour leader. He said he had defied the critics to hang on across England, where the party retained councils such as Crawley and Plymouth and had suffered a lower net loss than expected, of two dozen councillors.

“All across England last night we were getting predictions that Labour was going to lose councils. We didn’t, we hung on and we grew support in a lot of places,” Corbyn said in a defiant speech to activists in Sheffield.

In Scotland, however, Labour was pushed into third place by the Conservatives in a crushing defeat for a party that once dominated the political landscape north of the border. Corbyn said: “We are going to walk hand-in-hand with our party in Scotland to build that support once again.”

The leader’s positive take on the election results contrasted with a more cautious response from a series of shadow cabinet members who said that Labour had a long way to go before it was on track for a 2020 majority.

The shadow leader of the House, Chris Bryant, said Labour was not “match ready”, while the shadow Scottish secretary, Ian Murray, claimed that people did not see Corbyn’s Labour as a “credible party of future government”.

We nominated Jeremy Corbyn for the leadership. Now we regret it
Jo Cox and Neil Coyle


Other seized on the predictions of psephologists who said it was extremely unusual for a party in opposition to lose council seats at this stage of the electoral cycle.

Jo Cox and Neil Coyle, two new MPs who nominated Corbyn, wrote in the Guardian that they regretted their decision, warning that “weak leadership” risked keeping their party out of power until 2030.

Cameron hailed the Scottish result, saying he would not have believed it possible two years ago. He accused Labour of losing touch with working people by being “obsessed with their leftwing causes and unworkable economic policies”.

FacebookTwitterPinterest Scottish Conservative leader Ruth Davidson stands with Edinburgh Castle in the background. Photograph: Danny Lawson/PA

Dubbed “Super Thursday”, the day of elections across the UK saw:

• Labour achieving 31% of the vote share, just ahead of the Conservatives on 30%, according to a BBC forecast, based on how people had voted in England.

• The SNP losing its overall majority in the Scottish parliament but easily remaining the largest party with 63 seats, ahead of the Conservatives with 31 seats and Labour with 24.

• Labour remaining the dominant party in Wales, winning 29 out of 60 seats, but losing its minister Leighton Andrews to the Plaid Cymru leader, Leanne Wood. Ukip also won seven seats in Wales.

The polling analyst John Curtice suggested the results would translate into 301 Tory MPs in a general election, short of a majority, with Labour on 253.

The Liberal Democrats made progress, taking control of Watford council and gaining seats elsewhere in the country.

But the main focus of the day was on Labour’s performance, after a week in which Corbyn had been plunged into controversy over antisemitism claims that resulted in a series of suspensions, including Ken Livingstone.

The Labour leader’s allies hailed the outcome, with the shadow chancellor, John McDonnell, and the shadow communities secretary, Jon Trickett, calling on critics of the leadership to “put up or shut up”.

MAGAZETINI LEO JUMAPILI

Friday, 6 May 2016

TRA YAAZIMISHA SHEREHE ZA KODI JIJINI DAR



Mkurugenzi wa Rasilimali Watu na Utawala wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Bw. Victor Kimaro (wa kwanza kushoto) akizugumza na wadau mbalimbali (hawapo pichani) juu ya uwezo wao wa kumudu ukusanyaji wa kodi vizuri ili waweze kufanikisha vizuri malengo waliyo jiwekea mwaka huu. 




Pia aliwashukuru (ITA) kwa kujitolea kutoa elimu kwa wawekezaji wote wanaofika hapa nchini iliwaweze kulipa kodi wanapo wekekeza hapa nchini. alizungumza hayo Siku ya maadhimisho ya sherehe ya siku ya kodi zilizofanyika kwenye ukumbi wa mikutano (TRA) Mwenge jijini Dar es
Salaam 2016

Mdau akifafanua jambo kwenye sherehe ya siku ya kodi zilizofanyika kwenye ukumbi wa mikutano (TRA) Mwenge jijini Dar es Salaam 2016.









Thursday, 5 May 2016

TRA YAWAANDALIA ZAWADI NONO WAANDISHI WA HABARI WALIOSHINDA TUZO YA UANDISHI WA KODI NA MAKUSANYO YA MAPATO


Pichani ni Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipakodi Bw. Richard Kayombo, kwa niaba ya Kamishna Mkuu wa TRA (Kushoto) akimkabidhi tuzo pamoja na cheti mshindi wa kwanza wa tuzo ya Uandishi wa habari za Kodi na Makusanyo ya Mapato ya Serikali kwa mwaka 2015 Bi. Valeria Mwalongo katika sherehe za kutunuku waandishi bora wa mwaka zilizofanyika katika Ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam tarehe 29 Aprili 2016

Mshindi wa pili wa tuzo ya Uandishi wa habari za Kodi na Makusanyo ya Mapato ya Serikali mwaka 2015 Bw. Nuru Hassan (kulia) akipokea cheti kutoka kwa Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipakodi Bw. Richard Kayombo (kushoto) aliyemuwakilisha Kamishna Mkuu wa TRA katika sherehe zilizofanyika katika ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam tarehe 29 Aprili 2016


Kwa mara ya kwanza katika historia ya Tuzo za Umahiri katika Uandishi wa Habari, ambazo hutolewa na Baraza la Habari Tanzania (MCT), waandishi wawili wameshinda tuzo ya Uandishi wa Kodi na Makusanyo ya Mapato ya Serikali kwa mwaka 2015,


Waandishi hao wawili, Valeria Mwalongo, mwandishi wa Redio Tumaini aliyeshika nafasi ya kwanza na Bw. Nuru Hassan kutoka Afya Redio aliyeshika nafasi ya pili katika kinyang’anyiro hicho ni washiriki na washindi wa kwanza kupata tuzo hiyo ambayo imeingizwa kwa mara ya kwanza kwa kazi za mwaka 2015.


Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipakodi kutoka TRA Bw. Richard Kayombo alitoa tuzo hiyo kwa waandishi hao kwa niaba ya Kamishna Mkuu wa TRA katika Ukumbi wa Mlimani City Dar es Salaam ambako sherehe za kutunuku Zawadi zilifanyika.


Kutokana na ushindi huo Bw. Richard Kayombo amesema TRA itatoa donge nono kwa waandishi wa habari watakaoshiriki na kushinda katika kundi la uandishi wa habari za kodi na ukusanyaji wa mapato. Mshindi wa kwanza wa 2015 Bi. Valeria Mwalongo atajipatia kompyuta mpakato na wapili Bw. Nuru Hassan atajipatia simu aina ya Samsung mbali na kupata tuzo na vyeti kutoka MCT.


“Mamlaka ya Mapato Tanzania imedhamiria kuwajengea uwezo zaidi wanahabari kwa kuwaelimisha juu ya masuala ya kodi kwa kushirikiana na MCT ambao waowatawajengea uwezo juu ya uandishi bora kwaajili ya kuchochea ushindani zaidi katika kundi hili mwaka ujao kwa kazi ambazo zitaandikwa katika mwaka huu wa 2016.” Alisema Bw. Kayombo


MCT ilianzisha kundi la tuzo za uandishi wa habari za kodi na ukusanyaji mapato baada ya Mamlaka ya Mapato Tanzania kuomba kundi hili liingizwe katika tuzo hizo kwa kuzingatia kwamba waandishi na watangazaji wa habari wanaweza kushiriki kwa kuandika masuala ambayo yataongeza ridhaa ya kulipa kodi kwa hiari.


Sehemu ya barua ya TRA kwa MCT inasema, “TRA inatekeleza majukumu mbalimbali na mojawapo ni kuihabarisha jamii kupitia vyombo mbalimbali. TRA pekee haiwezi kufanikisha jukumu hili bila kuwashirikisha wadau ndio maana inaiomba MCT kuanzisha kundi la tuzo ya uandishi wa masuala ya kodi”


Tuzo ya kundi la uandishi wa Kodi na ukusanyaji mapato ya serikali ilijumuisha habari mbalimbali za masuala ya kodi, masuala ya ukusanyaji wa kodi, umuhimu na matumizi ya kodi hasa katika kugharimia huduma za jamii, nidhamu ya ukusanyaji na utumiaji, mianya ya upotevu wa mapato, njia za kuongeza wigo wa kodi. Nia ni kuongeza uhiari wa ulipaji kodi kwa ili kukuza mapato ya serikali


MCT ilizindua uwasilishaji wa kazi za wanahabari tarehe 12 Februari 2016 kwa makundi 22 yaliyojumuisha uandishi wa habari za Uchumi na Biashara, Michezo na Utamaduni, Mazingira, Watoto, Virusi vya Ukimwi na Ukimwi, Utawala Bora, Jinsia, Sayansi na Teknolojia, Afya ya Uzazi, Uandishi wa Uchunguzi, Elimu, Utalii na Uhifadhi, walemavu, Mpiga picha bora wa magazeti, Mpiga picha bora, Mchoraji kibonzo bora, Afya ya Uzazi kwa Vijana, Gesi, petrol, Utafiti wa Madini pamoja na habari za kodi na ukusanyaji mapato.


TRA inatoa wito kwa waandishi wote kujitokeza kwa wingi zaidi kuwania kinyang’anyiro hiki katika mashindano ya mwaka ujao ili kuendelea kupaza sauti juu ya masuala mbalimbali yahusuyo kodi na kujishindia zawadi mbalimbali zitakazotolewa kwa kipindi hicho.
“Pamoja Tunajenga Taifa Letu”

WATOTO WAITAKA SERIKALI KUTUNGA SHERIA KALI ...

Na Friday Simbaya, Mufindi  Wanafunzi wa shule za msingi na sekondari wilayani Mufindi mkoani Iringa wameiomba serikali kwa kush...