Monday, 25 September 2017

MAJALIWA MGENI RASMI MAONESHO YA UTALII YA KARIBU KUSINI


Mkuu wa Mkoa wa Iringa Amina Masenza akizungumza na waandishi wa habari kuhusu maonesho ya utalii yajukalikanayo kama Karibu Kusini-Tanzania Southern Circuit yanataraijiwa kufanyika kwenye viwanja vya Kichangani, Iringa mjini, mkoani Iringa, kuanzia tarehe 27.09.2017 hadi 02.10.2017 jana. (Picha na Friday Simbaya)




Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika maonesho ya utalii yajukalikanayo kama Karibu Kusini-Tanzania Southern Circuit yanataraijiwa kufanyika kwenye viwanja vya Kichangani, Iringa mjini, mkoani Iringa, yatakayofunguliwa tarehe 29.09.2017.

Akizungumza na waandishi wa habari leo (Jumatatu) Mkuu wa Mkoa wa Iringa Amina Masenza alisema maonesho hayo yataanza tarehe 27 Septemba hadi 02 Oktoba, 2017.

Alisema kuwa mikoa ya nyanda za juu kusini (iringa, njombe, mbeya, songwe na ruvuma) kwa kushirikiana na wizari ya maliasili na utalii, shirika la kuhudumia viwanda vidogo (SIDO) pamoja na wadau mbalimbali wanaandaa maonesho.

Masenza alisema kuwa mwaka 2009, mkoa wa iringa uliteuliwa na wizara ya maliasilina utalii kuwa kitovu cha utalii kwa mikoa ya nyanda za juu kusini.

Alisema kuwa kutokana na uteuzi huo, mkoa wa iringa umepata heshima ya kuaandaa maonesho hayo.

“Lengo kuu ni kutangaza fursa na vivutio vya utalii vilivyopo katika mikoa ya nyanda za juu kusini ili wananchi na wageni kutoka ndani na nje wavifahamu na kuvitembelea na hivyo kukuza utalii kwa mikoa ya nyanda za juu kusini,” alisema masenza.

Alivitaja vivutio vilivyopo katika nyanda za juu kusini kama vile vya kihistoria, kiutamaduni na kiikolojia ambavyo vinafanya upekee wa mikoa hiyo katka utalii.

Maonesho ya utalii karibu kusini yanakwenda sambamba na maandhimisho ya kitaifa ya siku ya utalii duniani mwaka 2017 ikijumuisha pia maoneshoya bidhaa za wajasiriamali kutoka katika mikoa ya nyanda za juu kusini na mikoa minigine ya Tanzania.

Kwa mwaka huu 2017 maadhimisho ya siku ya utalii yanaongozwa na kauli mbiu isemayo, “ UTALII NI NGUZO YA UCHUMI WA VIWANDA.”

Sunday, 24 September 2017

HAFLA YA CHAKULA CHA JIONI ILIOANDALIWA NA KINANA KWA AJILI YA KIONGOZI WA CHAMA CHA KIKOMUNISTI CHA VIETNAM





Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Dodoma Alhaj Adamu Kimbisa akimtolea ufafanuzi wa zawadi ya kinyango Mjumbe wa kamati kuu ya chama cha kikomunisti cha vietnam (VCP) Comred Chau Van Lam uku katibu Mkuu wa (CCM) akishuhudia zoezi hilo,wakati wa hafla ya Chakula cha Jion ilioandaliwa na kinana.


Katibu mkuu wa Chama Cha Mapinduzi Comred Abdurahman Kinana akizungumza kabla ya Mjumbe wa kamati kuu ya chama cha kikomunisti cha vietnam (VCP) Comred Chau Van Lam kukabidhiwa zawadi na Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Dodoma Alhaj Adamu Kimbisa wakati wa hafla ya Chakula cha Jion.


Katibu mkuu wa Chama Cha Mapinduzi Comred Abdurahman Kinana akizungumza na balozi wa Vietnam Nguyen kim Doanh.



Katibu mkuu wa Chama Cha Mapinduzi Comred Abdurahman Kinana akifurahia jambo na wageni wake toka chama cha Kikomunisti cha Vietnam (VCP) jana wakati wa hafla ya chakula cha jion.




Katibu mkuu wa Chama Cha Mapinduzi Comred Abdurahman Kinana akizungumza wakati wa hafla ya chakula cha jion.


Wajumbe wa Chama cha kikomunisti cha Vietnam (VCP) pamoja na Katibu mkuu wa Jumuiya ya Umoja wa Wazaza CCM wa (pili toka kushoto) wakifuatilia mazungumzo ya Katibu mkuu wa CCM katika hafla ya chakula cha jion.



Baadhi Wajumbe wa Sekretariet wakifuatilia mazungumzo ya Katibu mkuu wa CCM katika hafla ya chakula cha jion.


Katibu Mkuu wa CCM Comred Abdurahman Kinana na Mjumbe wa kamati kuu ya chama cha kikomunisti cha vietnam (VCP) Comred Chau Van Lam wakinyanyua glasi kabla ya kuzigonganisha kutakiana heri kabla ya chakula cha jion alicho mwandalia Mjumbe wa kamati kuu ya chama cha kikomunisti cha vietnam (VCP) Comred Chau Van Lam Mjini dodoma.


Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Dodoma Alhaj Juma Kimbisa pamoja na Katibu wa idara ya SUKI kanal mstaaf Ngemela Rubiga wakinyanyua glasi kabla ya kuzigonganisha kutakiana heri kabla ya chakula cha jion Katibu mkuu wa CCM alicho mwandalia Mjumbe wa kamati kuu ya chama cha kikomunisti cha vietnam (VCP) Comred Chau Van Lam Mjini dodoma.


Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar DKT.Abdallah Mabodi akiagana na Mjumbe wa kamati kuu ya chama cha kikomunisti cha vietnam (VCP) Comred Chau Van Lam mara baada ya kumalizika hafla ya chakula cha Usiku ilioandaliwa na Katibu mkuu wa CCM Comred Abdulrahman kinana Mjini dodoma.


Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi Comred Abdulrahman Kinana akiagana na Mgeni wake Mjumbe wa kamati kuu ya chama cha kikomunisti cha vietnam (VCP) Comred Chau Van Lam mara baada ya kumalizika kwa hafla ya chakula cha jion aliomwandalia mgeni wake Mjini dodoma. (PICHA ZOTE NA FAHADI SIRAJI)











IFUNDA STUDENTS HAIL THE GOVERNMENT FOR SCHOOL RENOVATION


Peter Mbata's the Deputy Headmaster and Amon Chota (academic master).

Headmaster of Ifunda Technical School, Mpambwe Paul




The construction workers are going on with  rehabilitation  Ifunda Technical Secondary School e as they were found by our reporter yesterday (Photo by Friday Simbaya)



Students of the Ifunda Technical Secondary School in Iringa region congratulate the fifth-phase government headed by the president Dr. John Pombe Magufuli to revive and improve their school infrastructure.

They said that the government has decided to do rehabilitation of the oldest schools in the country including the Ifunda, that will contribute to the best outcomes for pupils as well as to create good educational and learning environment.

The Guardian yesterday paid a visit to the oldest of the Ifunda School and saw the rehabilitation and repairs managed by the Mbeya University of Science and Technology (MUST) going on.

Derika Makoi is a form three student, noted that the ongoing rehabilitation will help pupils do well in their studies as previously when the infrastructure was poor students were using candles and solar lamps to read.

He said that the ongoing rehabilitation of classrooms and dormitories will improve the environment for students to study because even in the classroom there is electricity when previously the students were studying in the dormitories.

Apparently, he said that they did not have a good studying place but instead in their dormitories with mix of pupils who slept in it and probably making noise.

"We had to use candles to study in classrooms because classes did not have electricity but at present we thank the government for repairing and improving our school infrastructure," said Makoi.

He said that the ongoing rehabilitation has been more profitable than the loss in that pupils are now confident in regular study because classrooms have light all the time.

Another form three student said the renovation has improved the environment in classes for many classes did not have doors and mirrors and during the wind could blow through the windows and blew all the papers away.

He said that sometimes the wind was blowing until the paper was shattered during the study but after the rehabilitation environment had been good.

He said previously few classes had electricity so pupils are doing preps all the time since most classes have electricity and read it until night.

However, he said the rehabilitation should also consider improving water supply because the school has poor water system and students spend more time looking for drinking water from afar.

He said that water is healthy so the government help improve water resources in school so that students can spend more time studying it, hence sanitation improvement.

In turn, the headmaster of Ifunda Technical School, Mpambwe Paul thanked the government for repairing their school as the program will raise the level of achievement for students.

He said that through the program the school environment will also contribute to the best outcomes for pupils and will also have a good teaching environment as infrastructure will be a companion for teaching and learning for students.

Other teachers who supported the government's plan for renovation was Peter Mbata's the Deputy Headmaster and Amon Chota (academic master).

Mpambwe said that the rehabilitation involved all classes, all dormitories with the administrative building except teachers' houses.

Recently the government through the ministry of education, science, technology and training has begun a comprehensive program for repairing all the oldest schools in the country after the oldest government schools have done poorly in national examinations for almost five years consecutively.

The government has established a strategic plan to revive and improve the schools.

In the past Parliament, Minister of Education, Science, Technology and Vocational Training, Dr. Joyce Ndalichako noted that during the 2016/17 budget, the Government has allocated a total of 33 billion shillings for the repair of all the oldest schools in the country and in the beginning, the total 20 schools will be allocated through the scheme where Sh 20 billion are allocated to the project.

She said the oldest 10 schools are Jangwani, Azania, Kibaha, Nangwa, Kigoma, Tosamaganga, Songea Girls' School, Malangali, Mirambo and Minaki School have already been entrusted to the Tanzania Real Estate Agency (TBA) and the rehabilitation work has begun and is expected to be completed this year.

The other 10 schools are Mpwapwa, Kibiti, Ifakara, Bwiru-Boys, Kantalamba, Moshi-Technical, Tanga Technical, Musoma- Technical, Ifunda- Technical and Mtwara technical have been awarded to the Mbeya University of Science and Technology (MUST).

End



Saturday, 23 September 2017

WANAFUNZI NA WALIMU WA SHULE YA UFUNDI IFUNDA WAMPONGEZA JPM KWA UKARABATI


makamu mkuu wa shule Peter Mbata (kulia) na Amon Chota (mtaaluma).


mwalimu mkuu wa shule ya sekondari ya ufundi Ifunda, Mpambwe Paul 



mafundi wakiendelea na ukarabati wa shule kongwe ya ifunda ufundi kama walivyokutwa na mwandishi wetu jana (Picha na Friday Simbaya)




Wanafunzi na walimu wa shule ya ufundi Ifunda (Ifunda Technical Secondary School) mkoani iringa wameipongeza serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na rais Dkt. John Pombe Magufuli kwa kufufua na kuboresha miundombinu ya shule yao.

Walisema kuwa baada ya mpango wa serikili kuamua kuanza ukarabati wa shule kongwe nchini ikiwemo Ifunda utachangia ufaulu bora kwa wanafunzi pamoja na kuweka mazingira mazuri ya kufundishia na kujisomea.

SIMBAYABLOG jana ilitembea shule hiyo kongwe ya Ifunda na kujionea ukarabati unaondelea kwa kusimamiwa na Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia cha Mbeya (MUST). 

Derika Makoi ni mwanafunzi wa kidato cha tatu alibainisha kuwa ukarabati huo unaoendelea utachangia wanafunzi kufanya vizuri katika masomo yao kwani hapo awali wakati miundombinu ilikuwa mibaya wanafunzi walikuwa wanatumia mishumaa kujisomea.

Alisema kuwa ukabarati ambao unaendelea katika madarasa na mabweni umeboresha mazingira ya wanafunzi ya kujisomea kwani hata madarasani kumekuwa na umeme wakati hapo awali wanafunfuzi walikuwa nasomea mabwenini.

Makoi alisema kujisomea mabwenini hakukuwa rafiki sana kwa kujisomea kwani kulikuwa na mchanganyiko wa wanafunzi wanaolala humo na pengine makelele kutoka kwa wanafunzi wa madarasa ya chini.

“Tulikuwa tunalazimika kutumia mishumaa kujisomea madarasani kwa vile madarasa hayakuwa na umeme lakini kwa sasa tunashukuru serikali kwa kukarabati pamoja na kuboresha miundombinu ya shule yetu,” alisema Makoi.

Alisema kuwa katika ukarabati unaoendelea umekuwa na faida nyingi kuliko hasara kwa wanafunzi sasa wanajiamini kwa kujisomea muda wote kwa sababu madarasani kuna mwanga muda wote.

Mwanafunzi mwingine wa kidato cha tatu alisema ukarabati huo umeboresha mazingira katika madarasa kwa madarasa mengi hayakuwa na milango na vioo madirishani kipindi cha baridi walikuwa wanapata shida.

Alisema kuwa kuna wakati mwingine upepo ulikuwa unapuliza mpaka kupeperusha makaratasi wakati wa kujisomea lakini baada ya ukarabati mazingira yamekuwa mazuri.

Alisema hapo awali madarasa machache yalikuwa na umeme kwa hiyo wanafunzi wanafanya prepo muda wote kutokana na madarasa mengi kuwa na umeme mpaka wanajisomea hadi usiku.

Alisema kuwa ukarabati pia uangalie suala la maji kwani shule hiyo ina miundmbinu mibovu ya maji kwani wanafunzi wanatumia muda mwingi kutafuta maji kutokana na visima vya maji kuwa vichache.

Alisema kuwa maji ni afya kwa hiyo serikali isaidie pia katika kuboresha miundombinu ya maji shuleni ili wanafunzi watumie muda mwingi kujisomea.

Kwa upande wake mwalimu mkuu wa shule ya sekondari ya ufundi Ifunda, Mpambwe Paul aliishukuru serikali kwa kukarabati shule yao kwani mpango utainua kiwango cha ufaulu kwa wanafunzi.

Alisema kuwa kupitia mpango huo mazingira ya shule pia utachangia ufaulu bora kwa wanafunzi na pia watakuwa na mazingira bora ya kufundishia kwa vile miundombinu itakuwa rafiki kwa kufundishia na kujisomea kwa upande wa wanafunzi.

Walimu wengine waliounga mkono mpango wa serikali kwa ukarabati huo ni makamu mkuu wa shule Peter Mbata na Amon Chota (mtaaluma).

Mpambwe alisema kuwa ukarabati huo unahusisha madarasa yote, mabweni yote pamoja na jengo la utawala isipokuwa nyumba za walimu.

Hivi karibuni serikali kupitia wizara ya elimu, sayansi, teknolojia na mafunzo imeanza mpango kabambe wa kukarabati shule zote kongwe nchini baada ya shule kongwe za Serikali kufanya vibaya katika mitihani ya taifa kwa kipindi cha takribani miaka mitano mfululizo.

Serikali imeanzisha mpango kabambe wa kufufua hadhi na kuziboresha zaidi shule hizo.

Katika Bunge lililopita, Waziri wa Elimu, Sayansi,Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi, Dk Joyce Ndalichako alibainisha kuwa kwenye bajeti ya mwaka 2016/17, Serikali imetenga jumla ya Sh bilioni 33 kwa ajili ya kukarabati shule kongwe zote nchini na kwa kuanza, jumla ya shule 20 zitakarabatiwa kupitia mpango huo ambapo Sh bilioni 20 zimetengwa kwa kazi hiyo.

Ilisema kuwa shule kongwe 10 Jangwani, Azania, Kibaha, Nangwa, Kigoma, Tosamaganga, Shule ya Wasichana ya Songea, Malangali, Mirambo na Minaki tayari zimekabidhiwa Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) na kazi ya ukarabati imeanza na zinatarajiwa kukamilika ndani ya mwaka huu.

Shule 10 nyingine ambazo ni Mpwapwa, Kibiti, Ifakara, Bwiru -Wavulana, Kantalamba, Moshi-Ufundi, Tanga-Ufundi, Musoma- Ufundi, Ifunda - Ufundi na Mtwara- Ufundi zimekabidhiwa Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia cha Mbeya (MUST).

Friday, 22 September 2017

IRINGA DISTRICT HAS SPENT 190 M/- AGAINST THE CHOLERA EPIDEMICS



Iringa District Health Officer Samwel Nkya (right)oversees the exercise of erecting red flags on households that does not use proper toilets in the district, Iringa region recently. (Photo by Friday Simbaya)




IRINGA District Council (IDC) has spent a hundred and ninety million (190 million) shillings against the cholera epidemics in the Pawaga and Idodi division in Iringa Region and is one of the 156 councils implementing the national sanitation campaign in Tanzania mainland.

Speaking at the time of delivery education of good toilet facilities in the district, health district health officer Samwel Nkya asked the people to start using the toilet to solve the problem of epidemics of the cholera that has been repeatedly affecting them.

"One of source of cholera epidemic is the use of toilets that are not so good you have to use better toilets and educate your citizens and today we give this education to the leaders, we want to bring education to the people," said Nkya.

Nkya said they offered education for toilet facilities and hand washing with soap from home-to-home level and primary and secondary schools, Colleges, religious institutions, private institutions, government institutions such as government offices and health centers aimed at eliminating the cholera disease.

"Looking so far we have succeeded in achieving a total of 24 households who have implemented this campaign through various stakeholders such as the health ministry, the water ministry (RWSSP),, the education department, the Iringa district council, the UNICEF, the SNV and the WARID in four wards, Mlenge,Mboliboli na Itunundu have begun to officially implement this campaign for the 2017/2018 financial year "said Nkya

In the February and April 2016, there was an outbreak of cholera disease in the Iringa district council where Mboliboli and Mlenge were affected by the disease while the villages of Luganga, Mnadani, Idodi and Mafuruto had a small number of cholera patients. .

Moreover Nkya said that the strategies of the district council of Iringa identify households with NGOs and sanitation, recognizing laborers and owners of rice fields, doing audits periodically to rural sanitation and hygiene education to the environment for protect yourself from cholera disease no longer appear in the council.

"We are placing the red flag households without better toilets and providing special time to improve their toilets, and even finances that will be provided to households and institutions that will not improve their toilets" said Nkya.

Nyamiki Kimsau is a citizen of Usolanga village Pawaga said that the cholera disease has become resistant to the village since citizens in the area have no toilet toilets that satisfy their health and well-being.

"We call on leaders to provide adequate education to the people so that they can know the importance of having better toilets than the present situation," said Kimsau.  By Friday Simbaya, Iringa



Thursday, 21 September 2017

SHAHIDI AIELEZA MAHAKAMA JINSI DC ALIVYOPEKUWA CHUMBA CHAKE



Na Woinde Shizza


SHAHIDI wa utetezi katika kesi ya kughushi Mukhtasari,wa serikali ya mtaa wa Levolosi ,mfanyabiashara ,Mathew Moleli ameieleza mahakama jinsi mkuu wa wilaya mstaafu alivyoingia kwa mabavu nyumbani kwake na kuamrisha askari polisi aliokuwa ameambatana nao wapekuwe chumba chake wakitafuta hati inayodaiwa kughushiwa.

Akitoa utetezi mbele ya hakimu Gwanta Mwankuga wa mahakama ya hakimu mkazi Arusha ,anayesikiliza shauri hilo huku akiongozwa na wakili wa utetezi Ephraim Koisenge, aliieleza mahakama hiyo jinsi alivyofedheheshwa wakati askari hao,akiwemo mwendesha bodaboda na mlalamikaji Makanga walivyopekuwa chumba chake wakitafuta hati ambayo ni mali.

Shahidi huyo aliiendelea kueleza kuwa, mnamo oktoba ,2 mwaka 2014 alishtakiwa katika mahakama ya wilaya iliyopo Sekei mkoani Arusha, kwa shauri kama hilo huku mlalamikaji akiwa ni Danny Makanga na baadae oktoba 1,mwaka 2015 kesi hiyo ilifutwa baada ya upande wa jamhuri kuomba kuondoa shauri hilo mahakamani jambo ambalo anadai linampotezea muda wake.


Alidai kuwa kufutwa kwa shauri hilo aliandika barua kwa mkuu wa upelelezi wa mkoa wa ARUSHA (RCO) kuomba kurejeshewa hati yake ya nyumba iliyokuwa inashikiliwa ofisi ya RCO, jambo ambalo hakuwahi kujibiwa hadi oktoba ,28 mwaka 2016 alipokamatwa na polisi na kufikishwa mahakamani akishtakiwa kwa makosa mawili ya kughushi Mukhtasari wa serikali ya mtaa wa Levolosi na kuwasilisha nyaraka za kughushi katika ofisi za jiji la Arusha ,

Hata hiyo upande wa mashtaka ukiongozwa na wakili wa serikali Mary Lucas ulimtaka mshtakiwa kueleza uhalali wa eneo anakoishi kwa sasa ,jambo ambalo shahidi huyo alisema ni mali yake na waliuziana kindugu na mlalamikaji Makanga bila kuandikishana na baadae alifuata taratibu zote za kuomba hati miliki kupitika kikao cha dharura kwa uongozi wa serikali ya mtaa wa Levolosi kilichoketi Septemba,10 mwaka 2006.


Pia shahidi huyo alieleza kuwa tangu kikao hicho cha serikali ya mtaa kiketi kwa dharura na baadae kupeleke maombi ya kupatiwa hati ya umiliki wa nyumba yake kiwanja namba 231 kitalu DD kilichopo Mianziani jijini Arusha ,hakuwahi kupata malalamiko yoyote kuhusu kughushi nyaraka za serikali,jambo ambalo ameiomba mahakama kuifuta kesi hiyo kwa sababu malalamiko hayo hayana ukweli wowote.


Kesi hiyo namba 430 ya mwaka 2016 inatarajiwa kuendelea tena ,Septemba 28 mwaka huu ,ambapo upande wa utetezi unatarajia kufunga utetezi wake kwa shahidi wa pili na wa mwisho baada yashahidi wa kwanza ambaye ni mshtakiwa kukamilisha utetezi,ambaye pia aliwasilisha nyaraka mbalimbali kama vielelezo mahakamani hapo.

Awali wakili wa serikali Mary Lucasi alipinga kuwasilishwa kwa baadhi ya nyaraka muhimu za mshtakiwa mahakamani hapo kwa madai kuwa nyaraka hiyo ni kivuli ,jambo ambalo lilipigwa na wakili wa utetezi Koisenge ambaye aliiomba mahakama izipokee kama kilelezo,jambo ambalo hakimu Mwankuga baada ya kuzipitia hoja ya upande wa mashtaka aliona hazina mashiko na kuzipokea ili zitumikea mahakamani hapo kama kielelezo.

AVUNJWA MGUU KWA RISASI


Mkazi wa kitongoji cha Endevesi ,kata ya Oljoro wilaya ya Arumeru,Hwanga Ndaskoy(30)amefunjika mkuu wake wa kulia baada ya watu wanaodaiwa kuwa ni askari polisi mkoani Arusha, wapatao nane kumvamia na kumpigwa risasi ,akiwa shambani kwake .


Akizungumza kwa masikitiko nyumbani kwake, baada ya kuruhusiwa kutoka hospitali ya Mount Meru alikokuwa amelazwa kwa zaidi ya wiki moja,Ndaskoy ameeleza kwamba tukio hilo limetokea mnamo,Agost 31,mwaka huu majira ya saa saba wakati akivuna mahindi shambani kwake akiwa na familia yake.


Alisema kua alifuatwa na askari hao waliokuwa wamevalia kiraia na mmoja mwenye silaha akiwa amevaa sare za kipolisi.


Pia askari hao walikuwa wameongozana na mkazi mmoja wa kitongoji hicho aliyemtaja kwa jina la ,Yohane Palay aliyemtambua kuwa ni baba mkwe wake .



‘’Nilimsikia baba mkwe akiwaelekeza askari hao wanikamate huku akiwatahadhalisha kuwa mimi ni mkorofi na wasinisogelee nitawakata na sime jambo ambalo sio kweli,ndipo askari mmoja mwenye silaha aliponifyatulia risasi ya mguu na kuanguka chini’’alisema Ndaskoy 


Aidha alisema askari baada kumpiga risasi walimpakia kwenye gari lao na kumpeleka katika hospital ya Mkoa Mt,Meru ambapo walimweleza daktari kuwa ameanguka na pikipili Jambo ambalo si kweli.


Alieleza kuwa kabla ya tukio hilo ,Agost 26 mwaka huu ,aligombana na mke wa kaka yake aitwaye ,Jehova Baraka ambaye wanaishi jirani baada ya mbuzi kula mahindi yake yaliyokuwa nyumbani .


Alisema ugomvi huo ulienda mbali zaidi kiasi cha kutoleana maneno makali ,ambapo Jehova aliamua kwenda kwa baba yake mzazi aitwaye Yohane Palay na kutoa taarifa kuwa amepigwa na shemeji yake .


Palay aliamua kwenda kituo cha polisi cha Mbauda jijini hapa na kutoa taarifa juu ya tukio hilo,hata hivyo viongozi wa kitongoji hicho wakiwemo wazee wa ukoo waliingilia kati na kumtaka Palay alirejeshe nyumbani ili wazee wa ukoo walipatie ufumbuzi wa kudumu jambo ambalo waliafikiana.


Alisema Kikao cha ukoo kiliketi,agost 30 na kukubaliana kumaliza jambo hilo kwa kuwatoza faini za kimila wahusika wote wawili baada ya kubaini wote wanamakosa,hata hivyo walishangaa kesho yake agost 31 kufuatwa na polisi na kupigwa risasi.


Kwa upande wake,Palay alikiri kupeleka malalamiko yake kituo cha polisi ,Mbauda ,akidai kuwa mtoto wake,ambaye ni mke wa kaka yake na majeruhi alipigwa na kudhalilishwa. Hata hivyo aalikana kuwarubuni Polisi ili wampige risasi mtuhumiwa





Akizungumzia tukio hilo,kamanda wa polisi mkoa wa Arusha,Charles Mkumbo alisema kuwa anafuatilia undani wa tukio hilo ikiwemo kubaini ni askari gani walienda kwenye tukio hilo na kuahidi kulitolea ufafanuzi.


"Kwa kweli sina taarifa ya tukio kama hilo ila nitachunguza kama lipo nitalitolea ufafanuzi" Kauli ya Mkumbo.


Mkumbo alisema analifanyia uchunguzi jambo hilo kupitia wasaidizi wake na kuahidi kuchukua hatua kali iwapo itabainika hapakuwa na ulazima wa matumizi makubwa ya silaha ya moto kwa askari wake.


Na Woinde Shizza 





Monday, 18 September 2017

WATALII ZANZIBAR HAWAJAKAUKA LICHA YA MSIMU ULIOPO KUZOELEKA KUWA WACHACHE


Na Jumia Travel Tanzania


Tanzania imebarikiwa kuwa na vivutio lukuki takribani kila sehemu utakayoipendelea. Mji Mkongwe uliopo visiwani Zanzibar ni mojawapo ya maeneo hayo yenye utajiri wa vivutio vya watalii kama vile maisha na vyakula vya wakazi wake, biashara pamoja na majengo ambayo yanayoakisi tamaduni za mataifa tofauti kama vile Waarabu, Waajemi, Wareno, Waafrika na Waingereza ambayo yamekuwepo tangu karne za 18 na 19.



Katika kuhakikisha maeneo hayo yanajulikana miongoni mwa watanzania na wageni wanaotembelea nchini, Jumia Travel wamezindua kampeni ambayo itakuwa ikiangazia maeneo mbalimbali. Ikiwa imejikita kwenye Mji Mkongwe wa Zanzibar, kampuni hii ambayo inajishughulisha na huduma za hoteli kwa njia ya mtandao ilifanya mahojiano na Meneja Operesheni wa Africa House Hotel, Bw. Justus Kisome na mazungumzo yalikuwa kama ifuatavyo.





JT: Unaizungumziaje hoteli yako?

Justus: Africa House Hotel ni hoteli ya nyota nne inayopatikana kwenye jengo la kihistoria linalomilikiwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar lililopo katika Mji Mkongwe wa Zanzibar. Hoteli yetu ina vyumba 15 vikiwa na hadhi tofauti kukidhi haja ya wateja mbalimbali wanaotembelea hapa. Miongoni mwa vyumba hivyo 6 vinatazamana na bahari ya Hindi ambavyo huwapatia wageni fursa ya kutazama tukio nadra na kuvutia la kuzama kwa jua. Vyumba 9 vinawapatia wateja mandhari nzuri ya Mji Mkongwe wa Zanzibar ambao umebarikiwa kuwa na majengo na tamaduni za kale kwa karne kadhaa sasa.


JT: Unadhani ni vitu gani vinaifanya hoteli yako kuwa ya kipekee?

Justus: Naweza kusema kwamba tunajivunia hoteli yetu kuwa ndiyo pekee yenye maktaba katika Mji Mkongwe huu wa Zanzibar ambapo wageni wanayo fursa ya kujisomea masuala mbalimbali. Lakini pia ukiachana na hilo, Africa House Hoteli ndiyo hoteli pekee yenye mgahawa unaopika vyakula vya Kichina katika Mji Mkongwe wa Zanzibar. Mgahawa huu tumeujenga hivi karibuni, hakuna hoteli yoyote hapa yenye huduma kama hii, mgahawa unaendelea vizuri kwani tunapata maombi ya huduma mpaka moja kwa moja kutoka nchini China.


JT: Je unafikiri wateja wako ni wa aina gani? Kutoka ndani au nje ya nchi?

Justus: Naweza kusema kwamba idadi kubwa ya wateja wetu ni mchanganyiko, wengi wakiwa ni kutoka nje ya hapa Mji Mkongwe. Kwa wageni wa hapa nyumbani wengi tunaowapokea hupendekezwa na serikali na kwa wenyeji pia huwaleta au kuwaelekeza wageni wao kuja hapa.


JT: Ni shughuli gani zinazopendelewa kufanywa au kuuliziwa zaidi na wateja pindi wanapotembelea hoteli yako?

Justus: Asilimia kubwa ya wageni tunaowapokea hapa huja kwa madhumuni ya kibiashara au kikazi sio kwa mapumziko. Kwa ujumla, kama zilivyo hoteli nyingi kwenye Mji Mkongwe, hufanya sehemu hii ni kama kituo na kisha kuendelea na safari zao. Hivyo basi, mara nyingi wageni wanaofika hapa hulala kwa siku moja au mbili na kisha kuendelea na safari zao kama vile kwenda sehemu za ufukweni, uwanja wa ndege au bandarini.


JT: Una maoni gani juu ya ukuaji wa utalii wa ndani? Je kuna mabadiliko yoyote uliyoyaona?

Justus: Ukuaji wa utalii wa ndani kwa hapa Mji Mkongwe ni mzuri kwani wageni huongezeka mara kwa mara kadiri siku zinavyokwenda. Ingawa hatupokea wageni wengi wazawa kwenye hoteli yetu lakini kuna idadi kubwa ambao huwaleta wageni wao hapa. Hata kama hawatembelei hapa lakini kuna maeneo mengi ambayo tunawaona watalii wazawa wakitembelea na kwenye mitaa ya Mji Mkongwe.



JT: Unaizungumziaje Zanzibar kama mojawapo ya sehemu inayopendelewa kutembelewa zaidi? Je unadhani umaarufu wake unaongezeka au kupundua kadiri miaka inavyozidi kwenda?

Justus: Zanzibar kama kitovu cha utalii bado ni imara na kinaedelea kukua kadiri siku zinavyozidi kwenda. Wateja ni wengi na wanaendelea kuongezeka. Kwa mfano, kuanzia mwezi wa Julai, Agosti na huu wa Septemba ni vipindi ambavyo huwa tunapokea wageni wachache lakini tofauti na kipindi cha nyuma wateja ni wengi na kuna baadhi ya hoteli zimejaza vyumba na zingine zikiwa zimebakisha vichache! Hii ni ishara na dalili nzuri kwamba hali ni shwari huku Zanzibar ambapo kwa kipindi kama hiki hapo awali hakukuwa na wageni wengi kama sasa.


JT: Unazungumziaje kuhusiana na tozo mbalimbali kwenye sekta ya utalii, ukiachana na 18% za VAT, je zinaathiri biashara yako?

Justus: Kwa upande wangu naweza kusema kwamba Zanzibar haijaathirika na hizo tozo mbalimbali na sidhani kama zimeathiri biashara yetu. Kwa mfano, tozo ambazo zinalipwa ni zilezile na wageni kutoka nje ambao wanakuja nchini kuja kutembelea vivutio mbalimbali zikiwemo kodi na viingilio. Kama kungekuwa na athari basi tungewasikia wageni wakilalamika lakini wanaridhika na kuelewa kuwa ni taratibu ambazo ziko kama sehemu nyingine ukizingatia ni vivutio ndivyo wamekuja kuviangalia na sanasana huwashawishi na wageni wengine kuja kutembelea Zanzibar.


JT: Una maoni gani juu ya shughuli za mitandaoni kwenye kukuza sekta ya utalii nchini Tanzania?

Justus: Ni kweli dunia imebadilika hususani kwenye namna biashara zinavyoendeshwa siku za hivi karibuni. Kama zilivyo sehemu zingine, Zanzibar nayo imeipokea teknolojia ya mtandaoni vizuri kwa sababu idadi kubwa ya wageni tunaowapokea tunawapata kwa njia ya mtandaoni. Na kitu kizuri ni kwamba wanaiamini mitandao hiyo katika kufanya huduma zao na sisi tunajiimarisha kila kukicha kwenye Nyanja hiyo.


JT: Kwa kuongezea, unauzungumziaje ushirikiano baina ya Jumia Travel na hoteli yako? Unadhani ni msaada katika uendeshaji wa biashara yako?

Justus: Mahusiano na ushirikiano wetu na Jumia Travel ni mazuri kwani wanatusaidia kwa kiasi kikubwa kwenye uendeshaji wa shughuli zetu. Jumia Travel inakuja vizuri na inakua kwa sasa kwani mchango wake kwenye uendeshaji wa shughuli zetu ni mkubwa kutokana na wao kuwepo kwenye soko. Ukilinganisha na mwanzo ambapo kulikuwa na changamoto kadhaa kama vile kutokuwepo na mawasiliano ya kutosha pale kunapokuwepo na matatizo. Hivi sasa wanatutembelea na kuwasiliana mara kwa mara kujua tunafanyaje shughuli zetu. Naweza kusema wanastahili pongezi kwa hilo na naamini timu ya sasa iliyopo inafanya kazi vema na inajitambua zaidi.

WATOTO WAITAKA SERIKALI KUTUNGA SHERIA KALI ...

Na Friday Simbaya, Mufindi  Wanafunzi wa shule za msingi na sekondari wilayani Mufindi mkoani Iringa wameiomba serikali kwa kush...