KAIMU Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Bw. John Mnyika, amempa siku 14 aliyekuwa mgombea ubunge wa Jimbo la Isimani mkoani Iringa, Bw. Ben Kwapwani kutoa utetezi wake kwa maandishi kabla ya chama hicho hakitaja mwajibisha kwa kukikuka katiba ya Chadema.
Mbali na agizo hilo, pia Bw. Kapwani amesimamishwa rasmi nafasi ya Uenyekiti wa Mkoa wa Chama hicho hadi hapo uongozi wa juu utakapojiridhisha kuhusiana na shutuma mbalimbali zinazomkabili kada huyo.
Kwa mujibu wa barua ya Mnyika ya Septemba 14 mwaka huu aliyomwandikia Kapwani, ikiwa na kumbukumbu namba C.HQ/ADM/M/IR/05 inaeleza kuwa miongoni mwa mambo anayotakiwa kutolea maelezo ni pamoja na kushindwa kurudisha fomu ya uteuzi ya kugombea ubunge katika Jimbo la Isimani.
Shutuma nyingine zinazotakiwa kutolewa maelezo ni kuonekana kwake machoni pa umma akimnadi mgombea wa chama kingine wakati Chadema imesimamisha mgombea wake wa ubunge Iringa mjini ambaye anakubalika na wananchi wengi.
Anadaiwa kumpigia debe hadharani mgombea ubunge wa NCCR-Mageuzi Mariam Mwakingwe ambaye pia anaungwa mkono na muungano wa vyama vya upinzani vya TLP,DP,UDP na Chausta.
“Masuala hayo ni kinyume cha maadili ya chama kifungu cha 10.1 (viii),(xii) na 10.2 (10),(xi) zenye kutoa maadili ya viongozi na sifa mahususi za viongozi kwa pamoja.
Hata hivyo,Kwapani aliliambia mwandishi kwa njia ya simu jana kuwa yeye hajapokea barua hiyo hadi sasa lakini akadai haukubaliani na agizo hilo kwakuwa mwenye uwezo wa kumsimamisha uenyekiti ni mkutano mkuu wa mkoa na si Katibu mkuu kama alivyofanya Mnyika.
“ Mimi sijapata hiyo barua hadi tunavyoongea lakini hata hivyo huyo Mnyika au Katibu mkuu wa Chadema Dk. Wilbrodi Slaa hawezi kunisimamisha Uenyekiti isipokuwa mkutano mkuu pekee….Lazima aelewe mimi siwajibiki kwake”,alisema Kapwani.
Kuhusu tetesi kwamba leo Kapwani alikuwa akimsubiri mgombea Urais kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Jakaya Kikwete ili ajiunge na Chama hicho katika uwanja wa Samora mjini hapa,Kapwani alisema si kweli kama jinsi ambavyo inadaiwa ila yeye bado ni mwana Chadema na ataendelea kukitumikia chama chake.
Pamlomo24 is essentially a digital news platform that shares different types of news updates — social, political, economic, sports, entertainment, and community stories. From the context you’ve given, it is based in Iringa, Tanzania, and functions mainly as an online outlet (likely through social media such as Facebook, YouTube, or other channels) where audiences can get real-time updates.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
ASAS AWATOA HOFU WANANCHI KUHUSU VURUGU ZA UCHAGUZI
MJUMBE wa Kamati Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa, Salim Abri Asas , amewataka wananchi kujitokeza kwa wingi kupiga kura katika Uchagu...
-
Peter Mbata's the Deputy Headmaster and Amon Chota (academic master). Headmaster of Ifunda Technical School, Mpambwe Paul ...
-
KIKUNDI cha Upendo ni kikundi cha kina mama 20 walioamua kujiunga kwa pamoja na kuanz...
-
Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate ...
No comments:
Post a Comment