Sunday, 10 January 2016

TATIZO LA MAJI JIMBO LA NYAMAGANA MKOANI MWANZA LAMTESA MABULA



Mbunge wa Jimbo la Nyamagana Stanslaus Mabula akifafanua jambo ofisini kwake.



Mbunge wa Jimbo la Nyamagana Mkoani Mwanza (CCM) Stanslaus Mabula amesikitishwa na baadhi ya wakazi wa jimbo hilo kukabiliwa na ukosefu wa Maji safi na salama huku baadhi ya miradhi ya maji ikichukua muda mrefu bila utekelezaji wake kukamilika kwa wakati.

Mabula ameelezea masikitiko yake baada ya kupokea malalamiko kutoka kwa wakazi wa jimbo la Nyamagana, juu ya kukosa huduma ya maji ya bomba licha ya jimbo hili kuzungukwa na ziwa Victoria.

Mabula ambae alikuwa Mstahiki Meya wa Jiji la Mwanza katika uongozi uliomalizika mwishoni mwa mwaka jana, amebainisha kuwa ipo miradi ya maji ambayo bado haijatekelezwa kutokana na serikali kushindwa kutoa pesa kwa wakati jambo ambalo amesema kuwa atalisemea mara kwa mara katika vikao vya bunge lijalo ili kufanikisha upatikanaji wa fedha kwa ajili ya kutekeleza miradi hiyo.


span style="background-color: magenta; line-height: 115%;">Bonyeza PLAY Hapa Chini Kusikiliza</span>
Bonyeza PLAY Hapa Chini Kusikiliza

No comments:

ASAS AWATOA HOFU WANANCHI KUHUSU VURUGU ZA UCHAGUZI

MJUMBE wa Kamati Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa, Salim Abri Asas , amewataka wananchi kujitokeza kwa wingi kupiga kura katika Uchagu...