Sunday, 22 March 2015

Lee Kuan Yew afariki dunia

Waombolezaji wakiweka mashada ya maua mbele ya hospitali aliyofia baba Lee Kuan Yew.
Waziri mkuu mwanzilishi wa Singapore, Lee Kuan Yew amefariki dunia.Lee amefariki akiwa na umri wa miaka tisini na mmoja kutokana na ugonjwa wa mapafu.
Kwa miongo mitatu ya utawala wa Lee alifanikiwa kuipitisha nchi yake katika kipindi cha mpito na kuleta mabadiliko makubwa ya kiuchumi hasa katika usafirishaji majini kwa kutumia rasilimali kidogo walizokuwa nazo na sasa kuwa kitovu kikubwa cha kibiashara cha kimataifa.
David Adelman ni balozi wa zamani wa Marekani nchini humo, ametuma salamu zake za rambi rambi.Kifo cha Lee ni mwisho wa zama zake.mwisho wa mwanamume mwenye nguvu ya ushawishi aliyeingia madarakani katikati ya miaka ya sitini .
Lee alifanikiwa kuanzisha ushirikiano wa kirafiki kati ya nchi yake na Marekani ambao umedumu hata leo na unaweza kuvuka mipaka sio kwa singapore tu bali hata kwa watu wa Asia ya kusini Mashariki. (BBC)

ARUSHA YAMKUBALI KINANA

Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia wakazi wa Arusha mjini kwenye uwanja wa mkutano wa Sheikh Amri Abeid ambapo aliwaambia wananchi hao kuwa CCM itaendelea kuwatetea watu masikini na itahakikisha inawapa nafasi za uongozi watu wanaokubalika na wananchi.


Mwenyekiti wa CCM wa mkoa Onesmo Ole Nangole akihutubia wananchi wa Arusha ambapo aliwataka mawaziri kufanya ziara vijijini badala ya kukaa maofisini.

Katibu wa Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akihutubia wakazi wa Arusha mjini na kuwaambia pesa isitumike kununulia madaraka .


Amani Ole Silanga aliyekuwa Mwenyekiti wa Chadema wilaya ya Monduli na kujiunga na CCM akihutubia wananchi kwenye uwanja wa Sheikh Amri Abeid.

Amani Ole Silanga aliyekuwa Mwenyekiti wa Chadema wilaya ya Monduli na kujiunga na CCM akihutubia wananchi kwenye uwanja wa Sheikh Amri Abeid ambapo alisema Chadema hakina watu wenye sifa za kuongoza.

MANYONI MVUA HAIJANYESHA KWA MUDA MREFU MPAKA MAZOA YAMEKAUKA...!


Wakazi wa babati wilayani manyoni wakiwa katika pilikapili leo kama walivyokutwa stendi ya basi. 



Administrator wa blog ya SIMBAYA (FRIDAY SIMBAYA) akiwa Manyoni akichagua vinyago. NAMSHUKURU MUNGU NIMEFIKA SALA ARUSHA KUUNGANA NA KIKOSI KAZI.



Manyoni Lodge abiria tukipata chakula cha mchana baada ya safiri ndefu ya kutoka iringa kwenda Arusha. 

Friday, 20 March 2015

ONDOKA

POLISI WAMALIZA MZOZO WA TUNDUMA


JESHI la Polisi mkoa wa Mbeya, limefanikiwa kuzima mzozo na vurugu zilizodumu kwa siku tatu eneo la Tunduma wilayani Momba mkoani Mbeya.

Vurugu hizo zilitokea baada ya kiongozi wa Mtaa wa Makambini kata ya Sogea (chadema) kuwadanganya baadhi ya wananchi anaowaongoza kuwa alikuwa ameshinda kesi ya kiwanja kinachomilikiwa na Chama Cha Mapinduzi(CCM), na kuamuru uchimbwe msingi ili ijengwe hospitali.

Je Wajua Kilimo cha Nyanya kwenye Banda-kitalu




Kama ilivyo kwa vijana wengi wanaohangaikia maisha, Darius Cheruiyot wa Silibwet, Tarafa ya Bomet, amejaribu kushindana na maisha kwa njia nyingi, amejaribu ufundi makanika, udereva hadi kuwa dereva wa bodaboda. 

Huko kote hakukumfanikisha kimaisha hadi alipojishughulisha na kilimo. Darius (36) mkulima wa nyanya anapenda kuwashirikisha kwenye kilimo cha nyanya kwa kutumia banda kitalu (green-house). “ Wazo la kuanzisha banda kitalu ili kulima nyanya liliibuka mwaka 2012 baada ya kutembelea shamba la binamu yangu. Nilivutika sana na kile nilichokiona.” Cheriiyot alibainisha. Aliamua kulima kwa kilimo cha banda kitalu kwani alikuwa amejaribu kulima nyanya kwenye eneo la wazi; alipata hasara kwa kuwa nyanya zilishambuliwa na magonjwa na wadudu waharibifu.

SAMAKI WAADIMIKA MTERA


Soko Kuu la Manispaa ya Iringa, mkoani Iringa linakabiliwa na uhaba wa samaki kutokana na uvuvi haramu unaoendelea katika Bwawa la Mtera.

Baadhi ya wafanyabiasha wa samaki walioongea na gazeti la Nipashe leo walisema uhaba wa samaki katika soko hilo unatokana na sababu nyingi na kubwa zaidi ni uvuvi haramu uliyokidhiri katika Bwawa la Mtera.

TANZANIA, JAPAN WATILIANA SAINI UJENZI WA KITUO CHA UFUNDI STADI ILEJE


Signing the grant contract, witnessed by Hon. Janet Mbene, Deputy Minister of Industry and Trade, and Hon. Rosemary Senyamule, Ileje District Commissioner. Front line from the left: Mr. Mussa Otieno, District Executive Director, Mr. Simon Mwango'nda, Executire Director of the recipient organisation, Integrated Rural Development Organisation, Mr. Kazuyoshi Matsunaga, Chargé d'affaires of the Embassy of Japan.

Na Mwandishi wetu

MKATABA wa Ujenzi wa kituo cha mafunzo ya ufundi stadi katika Wilayani Ileje, Mkoani Mbeya umetiwa saini.

Mradi huo uliobuniwa na Naibu waziri wa Viwanda na Biashara, Janet Mbene na Simon Kamiyoge umelenga kuwawezesha wakazi wa Ileje kuwa na taaluma ya ufundi na baadae kutumika kuendelea wilaya hiyo.

Mkataba huo ulitiwa saini kati ya Kazuyoshi Matsunaga wa ubalozi wa Japan nchini na na Mwakilishi wa Integrated Rural Development Organisation (IRDO) Simon Kamiyoge wakishuhudiwa na Naibu waziri wa Viwanda na Biashara, Mh. Janet Mbene , Mbunge wa Ileje Rosemary Staki na Mkuu wa wilaya ya hiyo Mohamed Maliyao Mwala, na Mwenyekiti wa halmashauri ya Ileje Musa J. Otieno na maofisa wengine wa wilaya hiyo.

Kaimu Balozi wa Japan Kaziyoshi alisema amefurahishwa sana kutiwa saini kwa mkataba huo kwa kuwa unamkumbusha miaka 70 iliyopita katikati ya vita kuu ya pili ya dunia ambapo Japan ilijikuta katika uharibifu mkubwa pamoja na kubomolewa kwa majengo ya shule.

Alisema katika vita hiyo Japan ilijikuta si tu hawana shule bali hakukuwa na nyumba, maji, umeme hamna chochote kile lakini sasa hivi Japan ni ya tatu kiuchumi.


Discussion between Mr. Kazuyoshi Matsunaga, Chargé d'affaires of the Embassy of Japan, and Hon. Janet Mbene, Deputy Minister of Industry and Trade. From left: Hon. Janet Mbene, Deputy Minister of Industry and Trade, Hon. Rosemary Senyamule, Ileje District Commissioner, Hon. Mohamed Maliyao Mwala, Chairperson of Ileje District Council, Mr. Mussa Otieno, District Executive Director, Mr. Kazuyoshi Matsunaga, Chargé d'affaires of the Embassy of Japan.

MAMA WA MITINDO ASIA IDAROUS KUPAMBA SIKU YA MWANAMKE DUNIANI ZANZIBAR MACHI 22


..burudani kutolewa na Baby J, Coconut na Zanzibar One Modern taarab

Na Andrew Chale wa Modewji blog

Machi 22 mwaka huu Kisiwa cha Unguja, Zanzibar kinatarajiwa kuwa na tukio moja kubwa litakalowakutanisha Wanawake mbalimbali na kusheherekea siku ya Mwanamke Dunia, ndani ya ukumbi wa Bwawani Hoteli.

Katika tukio hilo, linatarajiwa kuwa pia na shamra shamra ikiwemo za mitindo ya mavazi kutoka kwa gwiji wa mitindo Nchini, Mama Asia Idarous Khamsin atakaye onesha mavazi mbalimbali siku hiyo akiwa sambamba na Mbunifu wa mavazi wa Zanzibar, Matilda Revelian wa Matty Designs.

Sherehe hizo zimeandaliwa na kikundi cha akina mama cha Zanzibalicious Women Group, chenye maendeleo makubwa kwa sasa hapa nchini.


Usiku huo utapambwa na burudani mbalimbali akiwemo mwanamuziki Baby J. Wengine ni bendi ya Coconut na Zanzibar One Modern taarab.

MKURUGENZI WA TIGO JACKSON KISWAGA ATUMIA ZAIDI YA SH MILIONI 10 KUFANIKISHA LIGI SOKA WILAYA YA IRINGA MAARUFU KAMA KISWAGA CUP




Kamu Meneja Mkuu wa Tigo Tanzania, Cecile Tiano akikabidi jezi kwa moja ya timu zinazoshiriki ligi ya wilaya ya Iringa (Kiswaga Cup) anayeshuhudiakushoto ni mdhamini wa ligi hiyo Jackson Kiswaga ambaye pia ni Mkurugenzi wa Tigo Nyanda za Juu Kusini. 









Kiswaga akieleza sababu za kufadhili ligi hiyo kwa lengo la kukuza sekta ya mchezo wa soka wilayani Iringa. 





Wakiwa katika picha ya pamoja na wawakilishi wa timu hizo 

WATOTO WAITAKA SERIKALI KUTUNGA SHERIA KALI ...

Na Friday Simbaya, Mufindi  Wanafunzi wa shule za msingi na sekondari wilayani Mufindi mkoani Iringa wameiomba serikali kwa kush...