Pamlomo24 is essentially a digital news platform that shares different types of news updates — social, political, economic, sports, entertainment, and community stories. From the context you’ve given, it is based in Iringa, Tanzania, and functions mainly as an online outlet (likely through social media such as Facebook, YouTube, or other channels) where audiences can get real-time updates.
Sunday, 15 August 2010
UBALOZI WA UNITED ARAB EMIRATES NCHINI WATOA MSAADA KWA WAISLAM
UBALOZI wa United Arab Emirates (UAE) nchini kupitia kwa Balozi wake Maala llah Mubarak Suweid umetoa msaada kwa waislamu kupitia taasisi ya Dhi nureyn Islamic Foundation yenye makao yake makuu – mkoani Iringa.
Msaada huo ambao umetolewa na taasisi mbili za nchini UAE ambazo ni : Sheikh Khalifa Bin Zaid Al Nahyan Foundation for humanitarian aid na Red Crescent Society of UAE , misaada hiyo ni kwa jili ya Mwezi Mtukufu wa Ramadhan ambao waislamu hufunga na kuzidisha kufanya mema kwa ajili ya kujikurubisha kwa mwenyezimungu.
Akizungumzia kuhusu msaada huo, Mwenyekiti Mtendaji wa Taasisi ya Dhi Nureyn Sheikh Said Ahmed Abri, amemshukuru balozi Maala llah na ubalozi mzima wa UAE kwa msaada huo, na amemuomba afikishe salamu na shukrani za waislamu kwa uongozi mzima wa uae na watu wake.
Msaada uliotolewa unafikia shilingi milioni hamsini (50,000,000) ambazo ni :
35,000,000 fedha taslimu kwa ajili ya programu za ufuturishaji na bosks 500 za tende zenye jumla ya kg 6,000 zenye thamani ya shilingi milioni 15,000,000/=.
Misaada hiyo tayari imekwisha sambazwa kwa walengwa kupitia misikiti zaidi ya 50 katika mikoa ya Iringa, Singida, Mbeya, Kilimanjaro na Dar es salaam.
.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
ASAS AWATOA HOFU WANANCHI KUHUSU VURUGU ZA UCHAGUZI
MJUMBE wa Kamati Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa, Salim Abri Asas , amewataka wananchi kujitokeza kwa wingi kupiga kura katika Uchagu...
-
Peter Mbata's the Deputy Headmaster and Amon Chota (academic master). Headmaster of Ifunda Technical School, Mpambwe Paul ...
-
KIKUNDI cha Upendo ni kikundi cha kina mama 20 walioamua kujiunga kwa pamoja na kuanz...
-
Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate ...
No comments:
Post a Comment