Pamlomo24 is essentially a digital news platform that shares different types of news updates — social, political, economic, sports, entertainment, and community stories. From the context you’ve given, it is based in Iringa, Tanzania, and functions mainly as an online outlet (likely through social media such as Facebook, YouTube, or other channels) where audiences can get real-time updates.
Friday, 12 November 2010
MKUU WA MKOA WA TANGA APASUA HISIA ZAKE KWA WAANDISHI
Mkuu wa mkoa wa Tanga, Said Kalembo amewataka wahariri kusaidia kupatikana kwa nyenzo za wafanyakazi wao waliopo mikoani ili kuwaondolea utegemezi.
Mkuu wa mkoa alisema utegemezi huo unawafanya wasiwe huru katika kufanyakazi zao.
Alisema yeye anaona taabu sana anapowaona waandishi wa habari wakihangaika kwa kukosa usafiri na kulazimika kuomba hapa na pale akisema kwamba hali hiyo inamuingiza mtegoni.
"Mtu hawezi kuwa huru kama anafadhiliwa kila kitu" alisistiza Mkuu huyo wa mkoa ambaye alisema pamoja na hayo ofisi yake husaidia pale inapowezekana ili waweze kuandika habari za maendeleo.
Pia katika mazungumzo yake aliwataka kuzingatia mafunzo na kutumia mafunzo hayo kuunga daraja la kuhabarisha wananchi.
"Wahariri fikirini kuwawezesha, wasaidieni wapeni nyenzo, magari na vitendea
tunawanyima uhuru kwa ajili ya fadhila, kapewa usafiri wa gari, posho na mahali pa kulala. ataandika nini" alisisitiza mkuu huyo wa mkoa.
Mkuu ambaye alikuwa akifungua warsha ya wadau katika uchaguzi uliopita alisema kwamba ipo haja ya kuangalia dhamana kama viongozi kuwajali walio chini.
Katika uchaguzi uliopita malalamiko mengi yalikuwa ni ufadhili wa vyma a kwa waandishi ambao ulionekana kuchachafya kanuni za kazi za kiuandishi.
Imeelezwa kuwa wengine waliachwa kwa sababu ya kuandika kinyume na wengine hawakujereshwa katika msafara hali inayoonesha kuna mambo gani yanaweza kutukia ukitumia usafiri na posho ya mtu unayetakiwa kumwandikia ukiwa huru.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
ASAS AWATOA HOFU WANANCHI KUHUSU VURUGU ZA UCHAGUZI
MJUMBE wa Kamati Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa, Salim Abri Asas , amewataka wananchi kujitokeza kwa wingi kupiga kura katika Uchagu...
-
Peter Mbata's the Deputy Headmaster and Amon Chota (academic master). Headmaster of Ifunda Technical School, Mpambwe Paul ...
-
KIKUNDI cha Upendo ni kikundi cha kina mama 20 walioamua kujiunga kwa pamoja na kuanz...
-
Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate ...
No comments:
Post a Comment