Saturday, 5 December 2015

KUELEKEA SIKU KUU YA KRISMASI (START THE COUNDDOWN TO CHRISMAS)



Make sure you're able to relax and enjoy the countdown to Christmas by finishing off the shopping early. For more inspiration, take a look at our SEASONAL ESSENTIALS. 

TUNAKARIBISHA MATANGAZO YA BIASHARA KATIKA BLOG HII KUELEKEA SIKU KUU YA KRISMASI NA MWAKA MPYA  KWA BEI NAFUU KABISA KWA SHILINGI ELFU TANO TU KWA TANGAZO! KWA MFANO;  WAFANYABIASHARA WA NGUO, VYOMBO VYA NDANI, MITI YA KRISMASI N.K... WASILIANA NASI KWA SIMU. 0755528409. NYOTE MNAKARIBISHWA!

Friday, 4 December 2015

WAWILI WAFARIKI KATIKA AJALI YA GARI ILIYOBEBA MAGAZETI YA MWANANCHI





GARI iliyokuwa imebeba magazeti ya Mwananchi, The Citizen na Mwanaspoti ikitokea Dar es Salaam kuelekea Iringa na Mbeya, imepata ajali katika mlima wa Kitonga, wilayani Kilolo mkoani Iringa leo alfajiri.

Watu wawili wamekufa papo hapo na wengine sita kujeruhiwa, mmoja vibaya baada ya gari lililokuwa likisafirisha magazeti ya mwananchi kutoka Dar es Salaam kwenda Iringa na Mbeya kupata ajali eneo la mlima kitonga barabara kuu ya Dar-es-Salaam-Iringa.

Akizungumza na waandishi wa habari Kamanda wa polisi Mkoa wa Iringa Ramadhan Mungi alisema ajali hiyo ilitokea jana majira ya saa 11 alfajiri gari hilo la magazeti kuingia nyuma ya roli likiwa katika mwendo kasi.

“Leo imetoka ajali mbaya sana hapa Iringa, ajali hiyo ilihusisha gari aina ya Haice iliyokuwa imebeba magazeti ya Kampuni ya Mwananchi Communication LTD; gari hilo lilipata ajali baada ya kuganga lori lenye tela kwa nyuma:

“Dereva wa gari hilo lililopata ajali alitaka kulipita roli ambalo nalo lilikuwa linaelekea Mbeya; alipokuwa akitaka kulipita aliona gari likija mbele yake na wakati akifanya maamuzi ya kurudi upande wake aligonga roli hilo kwa nyuma,”alisema.


Mungi aliwataja waliopoteza maisha katika ajali hiyo kuwa ni Eliud Ogwasa (40) na Godfrey Owino (34) wote wakazi wa mkazi Dar es Salaam.

Aliwataka majeruhi kuwa ni Baraka Shitindi (32) ambaye hali yake ni mbaya na Kevin Shitindi (30) wakazi wa Mbozi Mkoani Mbeya na Herold Shitindi (25) mkazi wa Morogoro.

Wengine ni Zabroin Izote (29) mkazi wa mbeya na Joseph Kayani (37) mkazi wa Mafinga mkoani Iringa.

“Kamanda Mungi aliwaasa madereva kuwa makini na kuendesha gari kwa kuzingatian sheria za barabarani ili kuepuka ajali zinazoweza kuwapotezea maisha wao na abria wao,” alisema.

Kaimu Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Iringa, Alfred Mwakalebela alisema wamepokea maiti mbili ambazo wamehifadhi kwenye chumba cha kuhifadhia maiti hospitalini hapo.

Dkt. Mwakalebela alisema pia wamepokea majeruhi wanne ambao wameumia maeneo mbalimbali mwilini ikiwemo kuvunjika mguu huku mmoja kati yao akiwa na hali mbaya zaidi kiasi cha kushindwa kuzungumza.

Majeruhi Kevin Shitindi ambaye ameumia mkono na kifuani alisema walitoka Dar es Salaam saa sita usiku wakiwa 10 kwenye gari hiyo na walipofika Morogoro saa nane watu wawili walishuka.

Majeruhi Kayani na Lisote walisema hiace hiyo ilikuwa inakwenda kasi na wakati ajali inatokea wao walikuwa wamelala walichosikia ni kishindo na baadaye kuona madereva wamekufa papo hapo.

HALMASHAURI YA IRINGA MJINI YATOA AHADI 15 KWA WANANCHI WA JIMBO HILO


Meya wa Manispaa ya Iringa Alex Kimbe na Naibu wake Joseph Lyata,


Na Frank Leonard, Iringa

MSTAHIKI Meya wa Manispaa ya Iringa Alex Kimbe na Naibu wake Joseph Lyata, wote kutoka Chadema, wamekutana na wanahabari kwa mara ya kwanza ofisini kwao hii leo na kuainisha mikakati yao mbalimbali inayolenga kuharakisha maendeleo ya wananchi wa Jimbo la Iringa Mjini katika kipindi cha miaka mitano ijayo.


Viongozi hao wanaunda halmashauri hiyo baada ya chama chao, Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kujizolea viti 14 kati ya 18 vya udiwani mjini Iringa huku nafasi ya ubunge ikichukuliwa na chama hicho kwa mara nyingine tena kupitia kwa mbunge yule yule wa 2010-2015, Mchungaji Peter Msigwa.


Kuhusu watendaji wa kata, mitaa na vijiji
1. Ni marufuku kuchukua fedha kwa wananchi wakati wakihitaji huduma ya muhuri kwa ajili ya barua za utambulisho, mikopo na zinginezo. Huduma hiyo ni bure sio ya kibiashara
2. Ni marufuku kwa watendaji na wenyeviti kujishughulisha na uuzaji wa viwanja katika maeneo yasio rasmi kama milimani na mabondeni ili kutoelendelea kuwapa hasara wananchi pindi mamlaka zinapolazimika kuwaondoa


Kuhusu barabara
1. Kwa kuwa ina greda kwa ajili ya kazi hiyo, halmashauri hiyo itajenga barabara katika maeneo yote ambayo ramani ya mipango mingi inaonesha kuna barabara zinapita ili wananchi wasirubuniwe na kuuziwa maeneo hayo kwa ajili ya shughuli zao za maendeleo
2. Barabara ya samora, kijiweni hadi hospitali ya manispaa ya Iringa Frelimo imeanza kujengwa kwa kiwango cha lami


Mwaka wa masomo 2016
1. Wanafunzi wa darasa la kwanza wanatakiwa kuandikishwa bure na inawataka walimu wa shule zote za msingi hadi sekondari kidato cha nne wasithubutu kuwabugudhi wanafunzi kwa kuwadai michango yoyote ile kwasababu serikali imekwishatoa maelekezo kwamba elimu hiyo itatolewa bure bila michango yoyote


Iringa kuwa jiji
1. Halmashauri ya Chadema itahakikisha inazifanyia kazi taratibu zote zinazotakiwa ili mji wake upate hadhi ya jiji.
2. Ili kufanikisha ndoto hiyo sheria zote za mipango miji zitasimamiwa na kutekelezwa kwa umakini mkubwa
3. Halmashauri mji wa Iringa unakuwa mji wa maghorofa na kwamba wale wote waliopewa likizo ya kujenga maghorofa katika maeneo yanayotakiwa kisheria kujengwa nyumba hizo (katikati ya mji) watatakiwa kufanya hivyo kama muda waliopewa umekwisha. Vibali vya ujenzi wa maghorofa na nyumba nyingine za kisasa vitaendelea kutolewa
4. Ili malengo hayo yafikiwe, wafanyakazi wa halmashauri hiyo (wataalamu) watatakiwa kufanya kazi kwa mujibu wa majukumu yao, kuzingatia sheria kanuni na taratibu zote za kazi ikiwa ni pamoja na muda wanaotakiwa kuwepo au kuondoka kazini


Kuhusu kodi
1. Kodi za halmashauri zinazotozwa kwa wananchi wa halmashauri hiyo zitaangaliwa upya, ili zile zinazoonekana kuwa kero kwa wananchi wa kawaida zifanyiwe marekebisho
2. Kodi za lazima ambazo hazina kero kwa wananchi zitakusanywa kwa nguvu ili kufidia nakuongeza mapato ya halmashauri hiyo; kodi hizo ni pamoja na za majengo.


Kuhusu matumizi ya halmashauri
1. Halmashauri hiyo mpya imeahidi kusimamia na kupunguza matumizi yote ya halmashauri yasio ya lazima ili fedha zitakazookolewa zitumike kuboresha huduma za kijamii


Kuhusu Gari la kubeba wagonjwa na taka
1. Mapato yatakayokusanywa, yakiwemo yale kutoka kwa wale wanakwepa kodi za majengo yatatumika kununua gari la kubeba wagonjwa na hivyo kufuta ule mpango wa kuuza gari la Meya ili fedha zitakazopatikana zitumike kununua gari hilo
2. Mapato hayo pia yatatumika kununua gari lingine la kubeba taka ili kukidhi mahitaji ya kuung’arisha mji wa Iringa


Kuhusu Mikopo ya Vijana na Wanawake
1. Halmashauri hiyo ya Chadema itafuatilia marejesho ya mikopo yote iliyotolewa kwa makundi hayo ili makusanyo yake yaendelee kuwanufaisha wananchi wengine


Kuhusu uwekezaji
1. Maeneo yaliyopendekezwa kwa ajili ya uwekezaji vitega uchumi vitakavyoiongezea mapato halmashauri hiyo kama ujenzi wa miradi mikubwa ya vitega uchumi katika maeneo ya Tembo Bar na Kilabu cha Kijiweni yatafanyiwa kazi kwa haraka.


Mapema mwaka 2011, halmashauri hiyo kwa kupitia aliyekuwa Meya wa Manispaa hiyo, Amani Mwamwindi iliahidi kuyabomoa majengo hayo ili kupisha uwekezaji mkubwa utakaoongeza mapato ya halmashauri hiyo.


Wakati Tembo Bar ipo pembeni mwa stendi kuu ya mabasi yaendayo mikoani, mjini Iringa, kilabu cha Kijiweni kipo karibu na Chuo cha Ufundi Stadi cha Veta.

Katika eneo la Tembo Bar, mpango wa halmashauri hiyo ulikuwa ni kujenga jengo la ghorofa tano na kituo cha mafuta huku katika kilabu cha Kijiweni mpango ulikuwa ni kujenga maegesho, ukumbi wa muziki, sherehe, bar, hoteli, maduka makubwa, ukumbi wa mazoezi na bwawa la kuogolea.


Kuhusu wamachinga
1. Halmashauri itakaa ili kuyapitia maamuzi ya halmashauri iliyopita yaliyowaondoa machinga katika gulio la Jumamosi na Jumapili katika eneo la mashine tatu ili wafanyabishara hao wapate fursa hiyo.
2. Ahadi hiyo itakwenda sambamba na kutafuta maeneo mengine kwa ajili ya wafanyabiashara hao


Kuhusu Michezo
1. Halmashauri itaangalia uwezekano wa kuwa na timu moja itakayosaidiwa kwa nguvu ya halmashauri na wadau wake ili kiu ya watu wa Iringa ya kuona wana timu inayoshiriki ligi kuu ifanikiwe


Kuhusu Mazingira
1. Halmashauri itatumia rasilimali zake, wakiwemo wananchi wenyewe kuhakikisha wanaufanya mji wa Iringa kuwa Mji wa Kijani kwa kupanda miti mingi huku mazingira yake yakiwekwa safi siku zote.


Kuhusu Biashara
1. Halmashauri ya Chadema itahakikisha wafanyabishara wanatengenezewa mazingira mazuri yatakayowafanya wafanye biashara zao bila kuvunja sheria, taratibu na kanuni zingine.


Kuhusu huduma za afya na maji
1. Halmashauri hiyo imeahidi kuziimarisha huduma hizo kwa kushirikiana na wadau wengine wote muhimu ili afya za wakazi wa Iringa ziimarike


Huduma zinginezo
1. Zitatekelezwa kwa kushirikiana pasipo kupindishwapindishwa na serikali ya awamu ya tano ya Dk John Pombe Magufuli


Kuhusu wanahabari
1. Halmashauri hiyo itahakikisha wanahabari wanashirikiana nao vyema ili kufikia malengo yao. Kutakuwepo na utaratibu wa kukutana na wanahabari wote kila baada ya miezi mitatu au pale inapohitajika kulingana na mahitaji yenyewe

World Soil Day



World Soil Day 2015 : ‘Soils a solid ground for life’


World Soil day celebrates the importance of soil as a critical component of the natural system and as a vital contributor to the human commonwealth through its contribution to food, water and energy security and as a mitigator of biodiversity loss and climate change. It is celebrated particularly by the global community of 60 000 soil scientists charged with responsibility of generating and communicating soil knowledge for the common good.

Soils have been neglected for too long. We fail to connect soil with our food, water, climate, biodiversity and life. We must invert this tendency and take up some preserving and restoring actions. The World Soil Day campaign aims to connect people with soils and raise awareness on their critical importance in our lives. 

The WSD 2015 will be celebrated on the 4th of Decemberat FAO headquarters in Rome and FAO regional offices. National events will also be organized so make sure to regularly check the map of the WSD2015 events and/or register your event. The theme for this year will be “Soils a solid ground for life”. 

Did you know? 

Soil is the basis for food, feed, fuel and fibre production and for services to ecosystems and human well-being. It is the reservoir for at least a quarter of global biodiversity, and therefore requires the same attention as above-ground biodiversity. Soils play a key role in the supply of clean water and resilience to floods and droughts. The largest store of terrestrial carbon is in the soil so that its preservation may contribute to climate change adaptation and mitigation. The maintenance or enhancement of global soil resources is essential if humanity’s need for food, water, and energy security is to be met. 

COSATO CHUMI AMALIZA TATIZO LA VITANDA HOSPITAL YA MAFINGA MJINI

Mbunge wa jimbo la Mafinga mji Cotato chumi akimkabidhi msaada wa vitanda ,magodoro pamoja na vifaa mbalimbali kaimu mganga mkuu wa hospitali ya Mafinga dk Abdul Msuya juzi



baadhi ya waandishi wa habari wakifuatiliwa ugawaji wa vifaa hivyo wakati wa makabidhiano






mbunge wa mafinga mjini cosato chumi akikabidhi vifaa hivyo kwa vitendo







baadhi ya wadau na wanachama wa chama cha mapinduzi ccm walihudhulia tukio hilo




TATIZO la upungufu wa vitanda katika wodi ya akina mama na watoto katika hospitali ya wilaya ya Mufindi mkoani Iringa ambalo kwa muda mrefu limekuwa chanzo cha msongamano na uwalazimu
baadhi ya wagonjwa kulala sakafuni sasa limepatiwa ufumbuzi baada ya uongozi wa hospitali hiyo kupokea msaada wa vitanda na vifaa tiba kutoka kwa mdau wa maendeleo katika sekta ya afya.
 
Mbunge wa Mafinga Mjini (CCM) Cosato Chumi alisema kuwa kwa muda mrefu hospitali hiyo ilikuwa ina upungufu wa vifaa mbalimbali ikiwemo vitanda hali iliyofanya kuandika maandiko mbalimbali kwa wahisani wa nje ya nchi ili kuweza kumsaidia kupata vifaa hivyo .

Alisema kuwa umefika wakati sasa wadau mbalimbali, mifuko ya kijamii na makampuni kujenga utamaduni wa kusaidia watu wenye mahitaji mbalimbali wakiwemo watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu na wagonjwa hospitalini kwani kufanya hivyo ni sehemu ya kurudisha kile wanachokitapa kwa jamii.
 
“Unajua afya ni kila kitu katika maisha ya binadamu hivyo lazima nitekeleze ahadi zangu nilizotoa wakati wa kampeni na wanachi lazima tufanye kazi kwa kujituma ili tumuunge mkono rais wetu ambaye anania ya ya kutuletea maendeleo na kuwataka wadau mbalimbali kusaidia jamii zenye mahitaji na kuacha kutegemea serikali pekee “alisema
 
Chumi aliwaomba wananchi wa jimbo hilo kuunga mkono kwa kufanya kazi kwa nguvu zote ili walete maendeleo kwa pamoja maana akifanya kazi pekee yake bila wao hawezi kuleta maendeleo
pekee yake.

Msaada huo wa vitanda 16 na magodoro 11 na vitu mbalimbali umetolewa na taasisi binafsi inayojishughulisha na masuala ya afya ya nchini Astralia ijulikanayo kama “Rafiki Surgical Mission” kwa uratibu wa ofisi ya mbunge wa jimbo la Mafinga mjini

Alisema kuwa msaada huo aliopatiwa na rafiki zao hawajatoa hata
senti tano bali huwa marafiki hao wanachangishana fedha na kununua vifaa hivyo na kisha kuvisafirisha mpaka bandari kavu ambapo hapo ndio hutumia gharama kusafirisha vifaa hivyo mpaka sehemu husika

“Ndugu zangu nadhani kila mmoja alikuwa akifahamu machungu waliyokuwa wakipata mama zetu wanapokuja kujifungua kwa kukosa sehemu za kujifungulia lakini leo hii msaada huu utatusaidia sana na yoyote atakayeguswa na anaweza kuja na kuchangia chochote maana mufindi ni yetu sote na mufindi itajegwa na wanamufindi wenyewe”alisema

Alisema jambo kubwa lilokuwa likimuumiza kicha kila kukicha ni tatizo la vifaa katika hospital, elimu pamoja na tatizo la maji hivyo ni wakati wawanamafinga kushikana kwa pamoja katika kusumkuma mbele gurudumu la maendeleo ili kuendana na kauli mbiu ya sasa ya HAPA NI KAZI TU.

Akipokea msaada huo kaimu mganga mkuu wa hospitali ya Mafinga dk Abdul Msuya alisema kuwa msaada wa vitanda hivyo na magodoro na vifaa mbalimbali utakuwa umemaliza kabisa tatizo la vitanda hospitalini hapo licha ya kukabiliwa na changamoto mbalimbali ambazo zinaweza kumalizika endapo kutatokea mdau mwingine kuwasaidi.
 
Kwa upande wake katibu wa ccm wilaya ya Mufindi Jimsoni Mhagama alimpongeza mbunge huyo kwa kutekeleza majukumu yake ipasavyo huku akimwambia kuwa ni wakati wa kutekeleza kazi kwa vitendo na wala si maneno kwani wananchi wanapaswa kutatuliwa kero mbalimbali zinazowakabili badala ya kupiga porojo zisizo na msingi .

Mhagama alisema kuwa kila mmoja anapaswa kuwajibika ipasavyo katika nafasi yake kwani kasi anayokwenda nayo Rais John Magufuli si ya mchezo bali ni ya mchaka mchaka na ili nchi iweze kusimama katika mstari ulionyoka kila mmoja anapaswa kucheza wimbo wa mchaka mchaka.

‘’Huuu si wakati lelemama huu sio wakati mchezo mchezo ni wakati wa uwajibikaji,hakika Tanzania tumepata kiongozi mchapa kazi tazama sasa ni siku ya 27 nchi inaongozwa na watu wanne lakini kila sektaa imenyoka na mimi  nasemaa Magufuli wanyooshe tu kwa kuwa watu walikuwa wakifanya kazi kwa mazoeya bila ya kuangalia madhara wanayopata watanzania wengi

Hata hivyo Mhgama alisema kuwa kwa kuwa kipindi cha muda mchache nchi inaongozwa na watu wachache na nchi imesimama haoni sababu ya kuwa na baraza kubwa la mawaziri, bali Rais Magufuli achague baraza dogo kama la watu10 ili kupunguza mzigo kwa serekali yake ya kuwa na mawziri wengi wasiokuwa na tija .





Thursday, 3 December 2015

AMKA NA SIMBAYABLOG KWA MAGAZETI YA LEO IJUMAA




















MEYA WA MANISPAA YA IRINGA KUZUNGUMZA NA WANAHABARI KESHO





MSTAHIKI Meya wa Manispaa ya Iringa, ambaye pia ni diwani kata ya Isakalilo, Alex Kimbe (Chadema) pichani kesho saa 5 asubuhi ataongea na waandishi wa habari ofisini kwake, juu ya mustakabali ya Manispaa ya 2015-2020.

Diwani wa kata ya Isakalilo, Alex Kimbe (Chadema) jana alichaguliwa kwa kura 21 kuwa Meya wa Manispaa ya Iringa.

Kuchaguliwa kwa Kimbe kumemaliza mvutano wa ndani kwa ndani uliokikumba chama hicho wakati kikiwa katika mchakato wa kumpata mgombea wa nafasi hiyo na kumaliza historia enzi ya Chama cha Mapinduzi (CCM) kutoa Meya kila baada ya Uchaguzi Mkuu.

Katika kinyang’anyiro hicho ambacho CCM walikuwa wasindikizaji kwasababu ya kuwa na idadi ndogo ya madiwani; mgombea wake Bashir Mtove alijipatia kura 6.

Mtove aliwania nafasi hiyo iliyoachwa wazi na aliyekuwa Meya wa miaka mingi wa manispaa hiyo, Amani Mwamwindi ambaye katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba mwaka huu, alishinda kwa kura chache kiti cha udiwani wa kata ya Mlandege dhidi ya mgombea wa Chadema, Richard Mfune.

Baraza hilo la madiwani lilimchagua pia Joseph Lyata wa Chadema kuwa Naibu Meya kwa kujinyakulia kura 21 dhidi ya kura 6 alizopata Dora Nziku wa CCM.

Awali katika salamu zake kwa madiwani hao, Katibu wa CCM Manispaa ya Iringa, Elisha Mwampashi aliwataka madiwani na halmashauri hiyo kufanya kazi, kupunguza tambo za barabarani na kushirikiana na wananchi kuleta maendeleo kupitia Ilani ya CCM.

Chadema imeunda halmashauri hiyo baada ya kufanikiwa kushinda kata 14 kati ya 18 za Jimbo la Iringa Mjini linaloongozwa kwa awamu ya pili na Mchungaji Peter Msigwa aliyemshinda mgombea wa CCM, Frederick Mwakalebela katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu.

CHAVITA wamuomba Rais Magufuli awakumbuke

Rais John Magufuli


CHAMA Cha Viziwi Tanzania (CHAVITA) Tawi la Mkoa wa Iringa kimemuomba Rais Dkt.John Pombe Magufuli kuhakiksha kuwa makundi yote maalumu yanapata haki sawa na mengine ili kuondoa dhana ya ubaguzi.

Akiongea na SIMBAYABLOG Katibu wa CHAVITA Mkoa wa Iringa Shaibu Juma ambapo alisema kuwa wanamshukuru Rais John Magufuli kwa kutoa kibali cha kufanya sherehe za siku ya Walemavu kitaifa Mkoani Mwanza.

Alisema kuwa kuna makundi mengine, yamekuwa yakiwezeshwa mara kwa mara aidha kupitia kwa mashirika yasiyo ya Kiserikali na hivyo kuweza kupata maendeleo kwa haraka na kumudu maisha yao ya kila siku.

Juma alisema kuwa katika Kampeni zake za kutafuta Urais Dkt. Magufuli alisema katika utawala wake hatabagua makundi maalum hasa wenye ulemavu katika uongozi wake hali ambayo imeonyesha dhahiri kuwa amedhamiria kuwasaidia.

“Tunampongeza Rais John Magufuli kwa kuchaguliwa kuongoza Taifa la Tanzania na sisi kama makundi ya watu wenye Ulemavu tumeahidi kumpa ushirikiano wa hali ya juu kutokana na utendaji wake wa kazi hali ambayo itasaidia katika kuleta mabadiliko kwa wananchi wake ikiwa ni pamoja na kutekeleza kauli mbio ya “hapa kazi tuu,” alisema katibu hiyo wa CHAVITA.

Aidhi, katibu huyo alielezea masikitiko yake kwa Chama cha Walemavu Tanzania (SHIVYAWATA) Mkoa wa Iringa kwa kushindwa kuviunganisha vyama vya watu kwenye walemavu mbalimbali mkoani hapa na kumemuomba Rais Dkt.John Pombe Magufuli kuhakiksha kuwa makundi yote maalumu yanapata haki sawa na mengine ili kuondoa dhana ya ubaguzi.

Alisema tangu kuanzisha kwa tawi hilo la Chavita mkoa wa iringa mwaka 1994 hakijawahi kupata msaada wote kutoka kwa idara ya ustawi wa jamii mkoa, manispaa ya iringa pamoja na SHIVIWATA.

Kwa upande wake mjumbe wa CHAVITA Mkoa wa Iringa Alfred Emmanuel Chengula alisema kuwa ni vema kwa Serikali akangalia makundi kama hayo kwa sasa ili na wao pia wawe na uwezo wa kumudu changamoto nyingi zinazowakumba watu wa makundi ya Wenye ulemavu.

“Ni vema sasa kwa Serikali ya awamu ya tano Chini ya Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dk,John Magufuli kuliangalia kwa jicho la kipekee kundi hilo na kuangalia changamoto mbalimbali zinazolikumba ili kuweza kuwawezesha kiuchumi na kuweza kumudu maisha yao ya kila siku,” alisema Mjumbe huyo.

Mjumbe mwingine aliyeambatana na katibu huyo wa Chavita ni pamoja na Zawadi Boniface aliyehoji kuwa ile asilimia kumi inayotenga na serikali kila mwaka kwa ajili ya watu wenye ulemavu inaenda wapi.

Tarehe 3, Desemba ya kila mwaka ni siku ya Watu wenye Ulemavu duniani. Siku hii inatokana na uamuzi wa Umoja wa Mataifa kui tangaza siku hii kuwa ni siku ya Watu wenye Ulemavu duniani kufuatia Azimio Na. 47/3 la mwaka 1992.

Tanzania kama nchi mwanachama imeridhia na kusaini mkataba huu, na imekuwa ikiadhimisha siku hii kitaifa katika mikoa toufati na mwaka jana maadhisho huyo walifanyika mkoani Iringa.

maadhimisho haya ni kwa lengo la serikali na wadau mbalimbali utambua uwezo wa Watu wenye U lemavu na kujenga mazingira yanayotoa fursa na ushiriki wao katika shughuli mbalimbali za maendeleo hapa nchini.

Kutangazwa kwa siku hii kumelenga kuinua u fahamu wa jamii kuhusu masuala ya Haki za Witu Wenye Ulemavu pamoja na kutoa fursa kwa Serikali za kila nchi duniani kutafakari juu ya utoaji wa huduma endelevu kwa nia ya kuinua hali za maisha ya Watu Wenye Ulemavu. 



Australia Tanzania society donates hospital equipment to Mafinga Hospital





By Friday Simbaya, Mufindi 

Mufindi district hospital is now going to reduce the problem of shortage of beds for the pregnant women, after the hospital receiving medical equipment and supplies from Australia Tanzania society (ATS) yesterday. 

The overcrowding of pregnant women in the maternity ward with the shortage of beds at the hospital has forced the pregnant women to sleep more than one in one bed and others are left sleeping on the floor. 

Speaking to the journalist yesterday the acting medical officer in charge Dr. Abdul Mussa Msuya said that the donation will go a long way in reducing some of the problems the hospital was facing on a daily basis. 

He said that lack of hospital equipment and medical supplies was a major barrier for doing surgical operations and limitation of nurses and midwives is also another challenge but with that donations it will help minimize the huge challenge that they face on daily basis. 

Dr. Msuya said the hospital is at the moment facing the big challenges of doctors, health workers in all cadres, buildings and a laundry machine for washing hospital bedding. 

Although he did not specify the number of doctors and health workers the hospital needed, he said that his hospital is badly in need of health workers in all cadres. 

He said the hospital is also facing the challenge of overcrowding of patients because it is the only big hospital in the district. 

"The hospital receives more than 130 outpatients’ everyday and it has the capacity of accommodating 237 inpatients due to the limited number of beds in wards, which means the hospital needs more buildings for wards," he said. 

However, the newly elected Member of Parliament for Mafinga Town Constituency, Cosato Chumi has handed a number of hospital equipment and medical supplies to the district hospital yesterday. 

He said the donation came from their development partner called Australia Tanzania Society (ATS) through Rafiki Surgical Missions which includes beds, mattresses, trolleys, wheelchairs, crutches, walking frames and many others. 

Chumi said that ambition is to see help the community in Mafinga and Mufindi residents excel in health and water sectors as their major challenges the people is facing. 

Rafiki Surgical Missions is part of the Australia Tanzania Society, an Australian and Tanzanian is a non-government organization. 

Rafiki's mission is to help Tanzania deal with its reconstructive surgery needs whilst at the same time assist in capacity building through the transfer of surgical, anesthetic, physiotherapy and nursing skills to medical professional in Tanzania. 

In an effort to help alleviate severe shortages in medical and hospital equipment, Rafiki also aims to provide much-needed equipment to hospitals and medical facilities in Tanzania. 

RAS: Fufuani mifumo ya kukagua maziwa ili kulinda afya ya mlaji





Katibu Tawala wa Mkoa wa Iringa, (RAS) Wamoja Ayubu ametoa wito kwa wakaguzi wa maziwa kutoka mikoa ya iringa, njombe na mbeya kuwa jukumu la ukaguzi wa maziwa ni kazi yao ya msingi na sio kazi ya ziada kwao.

Alisema kuwa jukumu la ukaguzi wa maziwa kwa wakaguzi sio kazi ya ziada bali ni kazi yao ya msingi na kusisitiza watoe ushirikiano wa dhati kwa bodi ya maziwa na mradi wa uendelezaji sekta ya maziwa afrika mashariki (EADD II), ili kujenga na kuimarisa vituo vya mauzo ya maziwa.

RAS huyo alitoa rai hiyo jana wakati akifungua mafunzo ya siku nne ya wakaguzi wa maziwa kutoka mikoa ya iringa, njombe na mbeya yaendelea mkoani Iringa.

Alisema kuwa kukagua maziwa ni muhimu sana kwakuendeleza tasnia ya maziwa na kulinda afya ya mlaji na hasa kwa viwanda ili kuweza kusindika maziwa wanahitaji maziwa yaliyo na viwango vya juu vya ubora.

“Napenda pia nichukue nafasi hiikuwahamasisha halmashauri zote nchini kuanzisha au kufufua mifumo ya kukagua maziwa ili kulinda afya ya mlaji,” alisema Ayubu.

Alisema kuwa katika sheria za kulinda afyaya mlaji wa maziwa nchini Tanzania zipo sheria mbalimbali kama vile sheria ya maziwa ‘The Dairy Industry Act, 2004, Tanzania food, drugs and cosmestics Act, 2003, the local government act, 1982 na ‘the public health act,1992, sheria zote hizo zina lengo kuu ka kuhakikisha maziwa yanashughuliwa kwa usafi na kumfikia mlaji yakiwa bora na salama.

lisema kuwa serikali ina jukumu la kumwahakikisha mlaji anapata maziwa bora na salama na bila ya udanganyifu kama kuchanganywa maji na pia kudanganywa kwenye vipimo.

“maziwa ni kinywaji na ni chakula muhimu katika mwili wa binadamu, kwani ni katika maziwa ndiko unapopata virutubisho vyote vinavyohitajika mwilini kwa wakti mmoja. Maziwa ya protini, wanga, vitamin na madini ya aina nyingi,” alisema.

Soko la mawaziwa linashikiliwa namfumo wa soko lisilo rasmi ambalolinaaendeshwa na wachuuzi na wafanyabiashara wadogowadogo ambao huuza kati ya lita 20-100 kwa siku kutoka kwa wafugaji wadogo na mara nyingi wanatumia baiskeli kwa kusafirishia na kusambazia maziwa yakiwa ghafi.

WATOTO WAITAKA SERIKALI KUTUNGA SHERIA KALI ...

Na Friday Simbaya, Mufindi  Wanafunzi wa shule za msingi na sekondari wilayani Mufindi mkoani Iringa wameiomba serikali kwa kush...