Thursday, 19 August 2010

POLICE

RPC Assistant Commisioner of Police (ACP) Mangalla when he was speaking to reporters today not in the picture at his office in Iringa region.


IRINGA Regional Police Commander (RPC), Evarist Mangalla has attributed that the hit and run accidents have increased the number of accidents recorded in January to June this year.


RPC Mangalla told reporters yesterday at the press briefing that there were a lot of hit and run accidents than that of involving passenger buses, whereby there was 99 recorded accorded last this year and last there was 95, increase of four accidents.


Vis-à-vis, there were 74 fatal accidents last year but this year between the same period 75 deadly accidents were reported.
He noted that number of accidents that caused injuries last year was 21 and this year is 24 respectively.


“The numbers of people who died and injured last year were 86 and 73 respectively, and this year there were 85 deaths and 78 injuries respectively,” he said.


In Iringa region, number of accidents involving public passenger buses is smaller compared to other regions in the country due to intensive police patrols and checking on timetables at police checkpoints that are established along the road.


The hit and run accidents involve vehicles is mostly that are public but private, he noted.


In last, 20 licenses were cancelled due to reckless driving and drivers were penalized by using road traffic Act of 1973, which was revised in 2002, which empowers police to arrest any person violation the law.


He however pointed out that most people in Iringa don’t know how to use roads therefore is big challenge.


People also abuse the use of zebra crossings, whereby they stand there and start greeting each other on the zebra crossing.
But the zebra crossing is meant cross as faster as possible without delay by making that th


In order to reduce the road accident in the region, he urged pedestrians to use service roads if possible and driver to refrain from driving while they are drunk hence reduction both fatal and injury accidents respectively.

FOMU ZA UTEUZI

Dkt. William Mgimwa (CCM) wa kwanza kulia kusalimiana na mzee baada ya kurudisha fomu ya uteuzi leo.Dkt. Mgimwa aliyeshika fomu akisindikizwa na wananchi wa Kalenga baada ya kurudisha fomu yake ya uteuzi leo.Msimamizi wa Uchaguzi Msaidizi Bw. Martin Ndamo (wa tatu kulia) wa jimbo la Iringa mjini akibandika fomu zilizorudishwa na wagombea ubunge leo.Dkt. Mgimwa akiongea na wana habari muda mfupi baada ya kurudisha fomu ya uteuzi leo.

WAGOMBEA WAREJESHA FOMU ZA UTEUZI

WAGOMBEA ubunge katika majimbo ya Iringa mjini, Kalenga na Ismani mkoani Iringa warejesha fomu za uteuzi katika ofisi ya tume ya uchaguzi za Iringa Mjini na Iringa Vijijini leo.


Katika Jimbo la Ismani, ni mgombea mmoja tu ambaye ni Bw. William Lukuvi (CCM) ndiye karudisha fomu ya uteuzi kati ya wagombea watatu waliochukuwa fomu pamoja na Bw. Joseph Kapwani (CHADEMA) na Bw. Juma Fufumbe (CUF).


Bw. Lukuvi atatangazwa mshindi wa bila kupingwa katika Jimbo la Isimani baada ya maasa 24 na Msimamizi wa Uchaguzi, Bi. Tina Sekambo wa Wilaya ya Iringa, baada ya wagombea wengine kutorudisha fomu zao kabla ya saa 10 jioni.


Katika Jimbo la Kalenga, waliochukuwa fomu walikuwa wanne na wote wamerudisha fomu zao kabla ya muda uliopangwa na tume ya uchaguzi (NEC).


Waliochukuwa fomu za uteuzi na kurejesha ni pamoja na Bw. Katindasa Lumunko (TLP), Dkt. William Mgimwa (CCM), Bw. Makuke Majinga (Jahazi Asilia)na Bi. Rehema Paulo (CHADEMA).


Katika jimbo la Iringa Mjini ambapo aliyekuwa mshindi katika kura za maoni mwanzoni mwa mwezi huu, Bw. Frederick Mwakalebela ambaye pia ayeeuenguliwa NEC ya chama cha CCM baada ya kashfa ya kutoa rushwa na kesi yake inaendelea mahamani, na kumteuwa mshindi wa pili Bi. Monica Mbega kupitia tiketi ya CCM, basi urejeshaji wa fomu za uteuzi za ubunge umekamilika vizuri leo.


Bw. Willam Lukuvi akiongea na wana habari leo baada ya Msimamizi wa Uchaguzi katika Wilaya ya Iringa Bi. Tina Sekambo kumaliza kubandika fomu za uteuzi ubaoni.Mchungaji Peter Msigwa akirudisha fomu ya uteuzi leo kwa msafara wa gari mjini Iringa.
Waliochuwa na kurudisha fomu katika jimbo la Iringa mjini ni pamoja na Bi. Monica Mbega (CCM), Bi. Mariam Mwakingwa (NCCR-Mageuzi), Bi. Zaituni Mwaibula (CUF) na Mchungaji Peter Msigwa (CHADEMA).



Wednesday, 18 August 2010

UBALOZI WA UNITED ARAB EMIRATES NCHINI WATOA MSAADA KWA WAISLAM





From FRIDAY SIMBAYA in Iringa






SHEIKH Khalifa Bin Zayed Al-Nahyan Foundation for Humanitarian Aid and Red Crescent Society of United Arab Emirates (UAE) has jointly donated dates to various Muslim groups and the fasting Muslims in Tanzania through Dhi Nureyn Islamic Foundation-Iringa Region.






The two humanitarian aid institutions from UAE have donated the donation through their UAE Embassy in Tanzania in collaboration with UAE Ambassador to Tanzania , His Excellency Maalallah Mubarak Suweid for Muslims to observe the Holy Month of Ramadhan.






Dhi Nureyn Islamic Foundation Executive Chairman, Sheikh Said Ahmed Abri told the 'blogger’ today that the donation of ‘Iftar’ like dates is through the Programme of Breaking Fast for the Fasting Muslims in Tanzania , at the expense of Sheikh Kalifan Bin Zayed Al-Nahyan Foundation and Red Crescent Society Islamic foundations.






The total donation is 50,000,000/- including 35,000,000/- which will be for pragramme of breaking fast for Muslims in Tanzania and 500 boxes dates (6,000kgs) worth 15,000,000/-.






He noted has reached the beneficiaries through 50 mosques from Iringa, Mbeya, Singida, Kilimanjaro and Dar es Salaam regions.






Sheikh Abri has also expresed his graduates to the leadership of UAE and its pepole on behalf of all Muslims in tanzania for the generosty of giving the donation.


















According to the executive chairman , the Holy Month of Ramadan is all about fasting and teach Muslims about patience, humanity and spiritually.






He added that during Ramadan, Muslims ask forgiveness for past sins, pray for guidance and help in refraining from everyday evils, and try to purify themselves through self-restraint and good deeds.


















Tuesday, 17 August 2010

MWAKALEBELA KORTINI LEO


IRINGA MUNCIPALITY on Tuesday was the center of attraction when the residents of municipality flocked and packed full the court to follow the case of the former Tanzania Football Federation (TFF) Executive Secretary, Frederick Mwakalebela appeared in the Resident Magistrate Court of Iringa at Iringa.

Fredrick Mwakalebela appeared again in the Resident Magistrate Court of Iringa at Iringa on Tuesday before Resident Magistrate Festo Lwelu to answer charges of corruption raised against him, with criminal case No.4 of 2010.

Prevention and Combating of Corruption (PCCB) Prosecutor, Prisca Mpeka in collaboration with Imani Nitume before Magistrate Lwelu said Mwakalebela CCM candidate in nomination preferential on that material day was accused giving an advantage contrary to section 15 (1)(b) of PCCB Act No.11 of 2007 and lection Expenses Act No.6 of 2010.

She said that on the material day and date in June 2010 at Mkoga Village within Iringa Municipal in Iringa region being a CCM candidate in the nomination polls process did corruptly give Hamis Luhanga, Chairman for Mkoga Village and advantage of total sum of 100,000/- to be distributed to 30 CCM members who attended the meeting held at Hamis premises.



But the accused has denied his charge and he out on bond after the he had fulfilled all the conditions of bail, of which was supposed to bring two sureties and they have to execute the promise 5m/- each.

Meanwhile, Frederick Mwakalebela and his wife Selina Mwakalebela have appeared in the resident magistrate court of Iringa at Iringa on Tuesday over corruption.

The Prevention and Combating of Corruption-persecutors Prisca Mpeka and Imani Nitume said the Mwakalebela and Selina on that material day and date on 20th July 2010 at Mgongo Village within Iringa Municipality in Iringa Region conducted a meeting at the village where his wife Selina gave 100,000/- to Gwido Sanga so that he can distribute it 22 CCM members who attended the meeting.

However, this the second criminal No. 8/2010 which involves Mwakalebela and Selina his wife did corruptly y give Gwido Sanga total sum of 100,000/- to distribute to 22 members.

In this case two accused denied the charge and both cases No.4/2010 and No.8/2010 will brought to court again on 15th September, 2010 for another mention.

More than 80 CCM members came out to bail out Mwakalebela and Selina and they crowded the court to support although he was eliminated from the race of being an aspirant for Iringa Urban Constituency but the second winner Monica Mbega.

MWAKALEBELA KORTINI LEO



ALIYEKUWA Katibu wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Frederick Mwakalebela na mkewe Selina Mwakalebela wamefikishwa mahakamani na Taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa (Takukuru) Mkoa wa Iringa huku wakisindikizwa na umati mkubwa wa makada wa Chama cha cha Mapinduzi (CCM) na wananchi wa Manispaa ya Iringa.


Umati ulifurika mahakamani hadi kupelekea wasikilizaji wengine kusikilizia kesi inayowakabili huku wakiwa nje ya mahakama ya hakimu mkazi wa mkoa wa Iringa.


Umati huo unakuja siku chache baada ya Halmashauri kuu ya CCM (NEC) kumuengua Mwakalebela aliyeshinda kwa kupata kura 3,897 dhidi ya Mbunge aliyepita Monica Mbega aliyepata kura 2989 ambaye ameteuliwa na NEC.




Akisoma mashtaka hayo mbele ya hakimu mkazi wa mahakama ya Mkoa wa Iringa, Gladys Barthy, waendesha mashtaka wa Takukuru,Prisca Mpeka na Imani Mizizi walisema mshitakiwa namba moja na mbili kwa pamoja walitoa hongo ya sh. 100,000 kwa Gwido Sanga ili awagawie wajumbe ambao waliitwa kwenye kikao.


Mpeka alisema Julai 20 katika kijiji cha Mgongo Mwakalebela anadaiwa kuitisha kikao nyumbani kwa Sanga ambacho kilihudhuriwa na wajumbe wa CCM 22 ambapo baada ya hotuba Selina Mwakalebela alitoa Sh100,000 kwa Sanga ili awagawie wajumbe waliohudhuria.


Mpeka alisema washtakiwa hao kwa pamoja, walitoa rushwa kinyume cha sheria ya kupambana na rushwa namba 11 ya mwaka 2007 kifungu cha 15(1)(b) kinachokwenda sambamba na sheria ya gharama za uchaguzi namba 6 ya mwaka mwaka 2010 kifungu namba 21 (1) (a) na kifungu cha 24(8).


Washitakiwa wote walikana shitaka na kuachiwa kwa dhamana baada ya wadhamini kutimiza masharti yaliyowekwa na Mahakama.
Baada ya mabishano ya muda mrefu kati ya upande wa Mshaki ukiongozwa na Mizizi na wakili wa Mshakiwa, Basil Mkwata mahakama iliridhia sifa za wadhamini baada ya wadhamini wawili taarifa zao kutofautiana.


Alisema baada ya wadhamini kukamilisha masharti mahakama ilitoa dhamana ambayo masharti yake yalikuwa walitakiwa kuwa na Sh500,000, mali isiyohamishika na mmoja wapo kuwa mtumishi wa serikali au taasisi inayotambulika.


Katika kesi nyingine iliyotajwa kwa mara ya pili, Mwakalebela anadaiwa kutoa hongo ya Sh100,000 kwa Mwenyekiti wa CCM kijiji cha Mkoga, Hamis Luhanga ili awagawie wajumbe 30 waliohudhuria kikao alichoitisha.


Akisoma shitaka hayo mbele ya hakimu, mahakama ya Mkoa wa Iringa, Festo Lwelu, waendesha mashtaka wa Takukuru, Prisca Mpeka na Imani Mizizi walisema Juni 20 mshitakiwa Mwakalebela anadaiwa kutoa hongo ya sh. 100,000 kwa Hamis Luhanga ambaye ni mwenyekiti wa kijiji cha Mkoga ili awagawie wajumbe wa CCM 30 ambao waliitwa kwenye kikao.


Mshitakiwa alikana shitaka na aliachiwa kwa dhamana baada ya wadhamini wake wawili kutimiza masharti yote yakiwemo ya kuwa na Sh5m, kutoa ahadi ya sh5m na mmoja kuwa mtumishi wa Serikali au taasisi inayotambulika.


Mpeka alisema mshitakiwa anadaiwa kutoa rushwa kinyume cha sheria ya kupambana na rushwa namba 11 ya mwaka 2007 kifungu cha 15(1)(b) kinachokwenda sambamba na sheria ya gharama za uchaguzi namba 6 ya mwaka mwaka 2010 kifungu namba 21 (1) (a) na kifungu cha 24(8).


Frederick Mwakalebela akiwa mahakani leo.Wakazi wa Manispaa ya Iringa wakiwa wamefurika nje ya Mahakama baada ya kutoka kusikiliza kasi ya Mwakalebela leo 
Kesi zote mbili zimeahirishwa mpaka Septemba 15 zitakaposikilizwa tena. Mwakalebela anatetewa na wakili Mkwata kutoka Mkwata Law Chamber.

Monday, 16 August 2010

VIKAO VYA MAHAKAMA RUFANI





OFISI ya Mkurugenzi mkuu wa mashitaka nchini (DPP), imeiondoa rmahakamani rufaa iliyokata kwenye mahakama ya rufaa ya Tanzania, dhidi ya Philbert Mtweve aliyeomba rushwa ya sh. 15,000 kwa mwalimu wa Shule ya Msingi Kennedy Rubindu.


Wakili wa serikali, Vicent Tangoh, aliomba kuondoa rufaa hiyo kupitia kanuni ya 4(ii)(a) ya mwaka 2009 ya mahakama ya rufaa, mbele ya majaji watatu waliokuwa wakisikiliza rufaa hiyo, Edward Rutakangwa, Natalia Kimaro na William Mandia.


"Awali tuliwasilisha taarifa ya kuondoa rufaa hii kwa kanuni ya 77(i) na tukagundua kanuni hiyo sio sahihi kuitumia kwani inaeleza kuondoa rufaa kwa msajili na sio mahakama ya rufaa, hivyo sasa tunaomba kwa kupitia kanuni ya rufaa kuondoa rufaa hii," Tangoh aliwaeleza majaji hao mahakamani hapo.


Baada ya ombi hilo, Jaji Rutakangwa alishauriana na wenzake na kukubaliana na ombi hilo na kuamua kuondoa rufaa hiyo iliyokuwa imekatwa na DPP.


Awali mwaka 2001, Mtweve alidaiwa na mahakama ya Wilaya ya Mbinga kuwa alichukua rushwa ya sh. 15,000 kutoka kwa Rubindu aliyekuwa mwalimu wa shule ya msingi ili amsaidie kumhamishia katika shule ya maeneo ya karibu na wazazi wake.


Hata hivyo, mahakama hiyo ilimuachia huru Mtweve baada ya kukosekana ushahidi lakini serikali kupitia makahama kuu walikata rufaa na Jaji Manento alitoa uamuzi mwaka 2002 wa kuona mshtakiwa hana hatia na baadaye DPP tena akakata rufaa kwenye mahakama ya rufaa Tanzania kupinga maamuzi hayo, lakini mwanasheria wake ameondoa rufaa hiyo mahakamani.


Wakati huohuo,Rufaa ya Yassin Thomas wa Songea ya kupinga kunyongwa hadi kufa iliyotolewa mwaka 2007 baada ya kumuua Mwanaidi Abdallah mwaka 2004, iliyokuwa isikilizwe leo kwenye mahakama ya rufaa ya Tanzania iliyoketi Iringa imesogezwa mbele hadi Ijumaa (Agosti 20), baada ya wakili wa kujitegemea, Basil Mkwata kuomba ili aweze kupitia sababu za rufani hiyo.


"Mwenyekiti, nilikuwa Dodoma katika kikao cha nusu mwaka cha mawakili na nikiwa njiani kurudi nikaambiwa nipitie hapa kuna rufaa na sijapata muda wa kupitia faili la kesi hii, naomba ipangwe siku nyingine ili niweze kusoma sababu za rufaa," aliomba Mkwata kwa Mwenyekiti wa jopo hilo la majaji.


Hatahivyo wakili wa serikali Michael Lwena alipendekeza isikilizwe Agosti 27, lakini Jaji Rutakangwa baada ya kujadiliana na wenzake walipanga kuwa Ijumaa, huku akimtaka wakili huyo kuhakikisha anasoma sababu hizo kwani ameahirisha kwa shingo upande kutokana na mahakama hiyo kuwa na rufaa nyingi zisizotoa muda wa mapumziko.


Mahakama hiyo iliyoanza jana inajumla ya rufaa 30 ambazo za jinai ni 24 na zilizobaki ni za madai na inatarajiwa kumalizika Septemba 6.
MWISHO
*****





UPUNGUFU wa majaji wa mahakama ya rufaa ya Tanzania unasababisha rufaa nyingi kuchukua muda mrefu kusikilizwa na kutolewa maamuzi, imeelezwa.


Naibu Msaijili wa mahakama ya Rufaa Tanzania, John Mgetta alibainisha hayo leo mara baada ya kikao cha kusikilizwa rufaa zilizokatwa na pande mbalimbali wakipinga maamuzi ya mahakama kuu, kilichokaa Iringa na kujumuisha pia rufaa za Songea.


Mgetta alisema majaji hao wapo 16 pekee ambapo wanatakiwa kujigawa katika kanda 10 huku Dar es Salaam ikiwa na majaji sita tofauti na kanda nyingine ambao ni watatu pekee.


Alisema majaji hao 16 wanatakiwa kutoa maamuzi katika kanda za Arusha, Dodoma, Tanga, Mbeya, Sumbawanga, Mwanza, Tabora, Mtwara, Dar es Salaam na Iringa.


Alitoa mfano wa Kanda Iringa inayokaa mara moja kwa mwaka ikijumuisha rufaa za Iringa na Songea rufaa zake zimeanza jana ambazo zipo 30 na zinasikilizwa na majaji watatu, Edward Rutakangwa, Natalia Kimaro na William Mandia na zitamalizika Septemba 6.


"Angalia mtu kakata rufaa tangu mwaka 2008 mwaka huu ndo inaanza kusikilizwa na hii ni sababu ya majaji wachache kwani kama wangekuwa wengi ingekuwa imeshaisha," alisema Mgetta.
MWISHO
*****





































IN THE COURT OF APPEAL OF TANZANIA AT IRINGA



THE THREE panel of Justice of Appeal have starting hearing both criminal and civil cases in the Court of Appeal of Tanzania at Iringa, it has been established.


The three of judges including Edward Rutakangwa (chairman of the panelists), Natalia Kimaro and William Mandia have started hearing criminal and civil cases in the court of appeal of Tanzania at Iringa on Monday.


According to the Deputy Registrar of Court of Appeal John Mgetta, the cause list of sessions will involve a total of 30 cases, that is 24 criminal and six civil cases from 16th August until 6th September, 2010 for judgments, rulings and orders respectively.


However, in the court of appeal of Tanzania at Iringa three justice of appeal in the first session have heard two criminal appeals including Case No. 61/2008 involving The Director Public Prosecution (DPP) versus Philbert Mtweve involving corruption since 2002 in Songea.


The Case No.61/2008 was withdrawn because both the two had never appeared in court since then.


The second case with No.63/2008, Yassin Thomas Nyumayo versus The Republic of Tanzania and it is a murder case but it was applied for the appeal since 2004.


In that case Nyumayo was accused murdering Mwanaidi Abdullah of Mshangano Village in Songea, Ruvuma Region, and sentenced to death by hanging before the Judge Lameck Uzea.


However, the case was adjourned until 29th August, 2010 because his private Lawyer, Basil Mkwata asked the court to push forward to the next date because he did not go through the case.


The Court of Appeal of Tanzania at Iringa is done once a year.


Meanwhile, the Deputy Registrar of the Court of Appeal, John Mgetta told reporters yesterday the country is facing a crisis of justice of appeal hence making the criminal and civil appeals to take longer to be heard.


He noted that there are only 16 justice of appeal in Tanzania but 10 zones of court of appeals of Tanzania and in each zone three judges were to hear the appeal cases.
















Sunday, 15 August 2010

KITIMUTIMU JIMBO LA IRINGA MJINI

BAADHI ya wanachama wa Chama cha Mapinduzi (CCM) wa mjini Iringa katika Jimbo la Iringa Mjini, kesho wameahidi kuanza kurudisha kadi za chama hicho katika ofisi za matwi yao ikiwa ni matokeo ya Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya chama hicho kumuengua katika kinyang’anyiro cha ubunge, Fredrick Mwakalebela aliyeshinda kura za maoni za chama hicho katika jimbo la Iringa Mjini.






Katika kura hizo, Mwakalebela alimshinda kwa kura 3, 897 na mpinzani wake wa karibu Bi.Monica Mbega aliyepata kura 2,989.






NEC imemuengua Mwakalebela katika mbio hizo za kuusaka ubunge katika jimbo hilo kumeelezwa kuhusishwa na kashfa ya rushwa inayomkabili.






Baada ya kupata taarifa za kuwepo kwa baadhi ya wanachama walioapa kurudisha kadi za chama hicho na kumuunga mkono mgombea wa Chama cha demokrasia na Maendeleo (Chadema), mwandishi wa habari hii jana alitembelea baadhi ya matawi ya chama hicho mjini hapa na kushuhudia makundi ya wanaCCM wakijipanga na kuendelea kuwashawishi wenzao kesho kuzirudisha kadi za CCM katika ofisi za matawi yao.






Matawi hayo ni pamoja na Kichanngani, Kihesa, Wilolesi, Soko Kuu la Mjini Iringa, Mshindo na Igumbilo.






Baadhi ya wanaCCM hao walisema maamuzi ya NEC yamemtoa kafara Mwakalebela ambaye taarifa zilizopo zinaonesha kwamba hakuwahi kukamatwa akitoa rushwa katika kinyang;anyiro hicho cha kura za maoni.






“Taarifa za Takukuru zinadai kwamba kwa kupitia mke wake ambaye naye hakukamatwa akifanya hivyo, Mwakalebela alitoa rushwa ya Sh 100,000 kwa wanachama 22 wa kijiji cha Mgongo, waliokuwa wamekusanyika nyumbani kwa Gwido Sanga wakimsikiliza wakati akitangaza nia ya kuwania ubunge katika jimbo hilo,” alisema David Butinini wa tawi la Mtwivila.






Naye Julie Sawani wa tawi la Kichangani, alisema wakati Mwakalebela akienguliwa kwa madai hayo ya rushwa, inashangaza kuona NEC hiyo hiyo imeyapitisha majina ya Basil Mramba na Andrew Chenge ambao wanatuhuma kubwa za rushwa.






Alli Mduba wa tawi la Kihesa alisema uamuzi wa CCM wa kuwataka wanachama wote washiriki katika kura hizo umekiwezesha chama hicho kujua wagombea wanaokubalika katika mbio hizo za uongozi, hata hivyo akasema maamuzi yaliyofanywa na NEC dhidi ya Mwakalebela majibu yake watayapata Oktoba 31, siku ya Uchaguzi Mkuu.






Mohamed Kassim wa wilolesi alisema, kesho jumatatu wanachama watarudisha kadi zao za CCM katika ofisi ya tawi katika tukio ambalo pia watalitumia kumtangaza rasmi mgombea watakayemuunga mkono.






Naye Edgar Sanga wa Igumbilo alisema wanaCCM watamaliza jazba zao za mgombea wao kuenguliwa kwa kumpigia kampeni na kura mgombea wa Chadema. Mchungaji Peter Msigwa.






“Mwakalebela ndiye aliyekuwa chaguo letu vijana, na wananchi wote wa jimbo la Iringa Mjini bila kujali rangi, itikadi, dini na makabila yao, tumesikitishwa na uamuzi wa NEC,” alisema mwingine aliyejitambulisha kwa jina la Anna Michael wa tawi la Miyomboni.

…VIGOGO………….1







ALIYEKUWA mshindi wa pili katika kura za maoni za Chama cha Mapinduzi (CCM) katika Jimbo la Njombe Kaskazini, Alatanga Nyagawa huenda akatimkia CHADEMA ikiwa ni hatua mojawapo ya kupinga maamuzi ya vikao vya juu vya chama hicho yaliyomteua Deo Sanga (Jah People) kuwa mgombea ubunge wa jimbo hilo.






Katika kura hizo, Jah people alipata kura 6,313 dhidi ya kura 2,313 alizopata Nyagawa huku mbunge mkongwe aliyemaliza muda wake Jackson Makweta akipata kura 1,671.






Akizungumza kwa njia ya simu jana, Nyagawa alisema yeye pamoja na wanaCCM wengine 11 waliokuwa wakiwania kushinda kura za maoni za jimbo hilo, walipinga matokeo yaliyompa ushindi Jah People kwa madai kwamba yalitawaliwa na mazingira ya hila na rushwa.






Nyagawa alisema tofauti na matarajio yake vikao vya juu vya CCM vimetupilia malalamiko yao ambayo yana ushahidi wa kutosha.






Nyagawa alisema kutokana na kasoro hizo hayuko tayari kuunga mkono ushindi na uteuzi wa Jah People kuwania ubunge katika jimbo hilo.






Alipoulizwa wapi hatma yake ya kisiasa itakuwa baada ya malalamiko yao dhidi ya Sanga kutupiliwa mbali, Nyagawa alisema anaendelea kupokea ushauri kutoka kwa wanaCCM na wapiga kura wengine wa jimbo hilo la Njombe.






Hata hivyo vyanzo vyetu vya habari kutoka katika jimbo hilo vimethibitisha kwamba baadhi ya wanaCCM wanaendelea na jitihada kumshawishi Nyagawa agombee jimbo hilo kwa kupitia Chadema.






Mmoja kati ya vyanzo hivyo alilidokeza gazeti hili kwamba maoni ya haraka yanaendelea kukusanywa kutoka katika kata zote za jimbo hili ili kupata ushauri zaidi kuhusiana na ushawishi huo wa kumtaka Nyagawa agombee kwa chama hicho.


Wakati hali ya kisiasa katika jimbo hilo ikiwa na mtazamo huo, wapiga kura wa jimbo la Njombe Magharibi nao wamesema wanataka sauti zao zisikike katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba mwaka huu na hivyo kwa hamu kubwa wanasubiri kujua hatma ya kisiasa ya aliyekuwa mshindi wa kura za maoni za chama hicho, Thomas Nyimbo.






Licha ya kuongoza katika kura za maoni Nyimbo na mbunge aliyemaliza muda wake Yono Kevela ambaye katika kinyang’anyiro hicho alishika nafasi ya pili, NEC iliwatupilia mbali na nafasi ya kuliwania jimbo hilo ilikwenda kwa Meneja wa Wakala wa Barabara (Tanroads) mkoa wa Dodoma, Greyson Lwenge.






Katika kura hizo Nyimbo alipata kura 6,795 dhidi ya kura 3,434 alizopata Kevela na 2,971 alizopata Lwenge katika kinyang’anyiro hicho kilichokuwa na wagombea 13

WATOTO WAITAKA SERIKALI KUTUNGA SHERIA KALI ...

Na Friday Simbaya, Mufindi  Wanafunzi wa shule za msingi na sekondari wilayani Mufindi mkoani Iringa wameiomba serikali kwa kush...