Wednesday, 29 July 2015

SAFARI YA MATUMAINI YA LOWASSA YAIBUKIA CHADEMA...!





WAZIRI Mkuu Mstaafu, Edward Lowassa amejiunga rasmi na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) huku akiahidi kuendeleza safari yake ya matumaini iliyopigwa STOP na alivyoviita vikao vya Chama cha Mapinduzi (CCM) vilivyokiuka katiba yake.


Katika hafla rasmi ya kukabidhiwa kadi yake, iliyofanyika hii leo jijini Dar es Salaam, Lowassa alisema mchakato mzima wa kumpata mgombea urais kupitia CCM uligubikwa na hila, chuki, majungu na uzushi dhidi yake.


Lowassa alisema maamuzi yaliyofanywa na vikao vilivyochuja jina lake na ya wengine, hayajawahi kufanywa katika historia ya chama hicho..

Alisema Kamati ya Maadili na Usalama ya chama hicho ilipokonya madaraka ya Kamati Kuu na akakifananisha kitendo hicho na lugha ya mtaani ya kubaka demokrasia.

Alisema CCM ile aliyoiona Dodoma sio ile iliyomlea na kumkuza na akaomba watanzania wajiunge na kuing'oa madarakani


Alisema kama ilivyowahi kusemwa na Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere, kwamba CCM sio baba yangu wala mama yangu; “na mimi hii leo natangaza rasmi kujiondoa CCM na kujiunga na Chadema. CCM sio mama yangu wala baba yangu. Naondoka CCM najiunga Chadema.”


Akizungumzia kashafa ya Richmond, Lowassa alisema ameitolea majibu mara kwa mara lakini watu wanataka kuziba masikio.


Lowasa alisema hausiki na kashfa hiyo na madai yanayotolewa dhidi yake kama yana ushahidi, mwenye ushahidi huo aende mahakamani.


MBOWE
SIASA ni mchezo ambao wakati mwingine gia ni lazima ibadilishiwe angani na kwamba chama ambacho hakiamini mabadiliko hicho sio chama.

Monday, 27 July 2015

MUCOBA Bank PLC LAUNCHES 20,000,000 ORDINARY SHARES SELLING TO GENERAL PUBLIC TODAY

Minister for Lands, Housing and Human Settlements Development, William Lukuvi

BY FRIDAY SIMBAYA, IRINGA: MUCOBA Bank PLC has started offering 20,000,000 ordinary shares at 250/- per share to the general public by way of Initial Public Offer (IPO) as part of its ongoing capital restructuring program, The Guardian has established.

The community bank is expecting to sell 20,000,000 ordinary shares to the general public worth five billion shillings (5bn/-) before the closing of the offer by way of IPO.

According to the General Manager, Ben Mahenge, that is representing 54.70 percent of the issued share capital of 36,560,760 ordinary shares of a nominal value of 50/-each.

Mahenge said that offer was officially launched today by the Minister for Lands, Housing and Human Settlements Development, William Lukuvi and the offer will be closed on 4th September this year.

Saturday, 25 July 2015

Maadhimisho ya Kumbukumbu ya siku ya Mashujaa Mkoani Iringa

Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama Mkoa wa Iringa Mhe. Amina J Masenza (kuume) na Mshauri wa Mgambo Mkoa Meja Akili katika Maadhimisho ya Kumbukumbu ya siku ya Mashujaa Mkoani Iringa.

Hepautwa:nafahamu maumivu yaliyotokea kwa wana CCM baada ya kuichagua Chadema uchaguzi wa mwaka 2010


Nuru Hepautwa



Na Friday Simbaya, Iringa

KADA maarufu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) wa mjini Iringa, Nuru Hepautwa amesema anafahamu maumivu yaliyotokea kwa wana CCM baada ya kuachia jimbo hilo mikononi mwa Chadema katika uchaguzi wa mwaka 2010 lakini akaahidi kuyamaliza endapo atapewa ridhaa hiyo.

Hepautwa ambaye pia ni mfadhili wa mashindano ya soka yaliyojizolea umaarufu mjini Iringa ya Hepautwa Cup alitoa mchango huo jana wakati akijinadi kwa wanachama katika Kata ya Kitwiru Jimbo la Iringa mjini.

MFANYABIASHARA huyo alitangaza nia ya kuwania ubunge wa jimbo la Iringa Mjini hivi karibuni katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba mwaka huu kwa kupitia tiketi ya chama chake, Chama cha Mapinduzi (CCM).

Hepautwa ambaye pia ni Naibu Kamanda wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Iringa Mjini alisema anafahamu maumivu yaliyotokea kwa wana CCM baada ya kuachia jimbo hilo mikononi mwa Chadema katika uchaguzi lakini akaahidi kuyamaliza endapo atapewa ridhaa hiyo.

Kwa mwaka wa tano sasa, jimbo la Iringa Mjini limeendelea kuongozwa na Mchungaji Peter Msigwa aliyechaguliwa kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) katika Uchaguzi Mkuu wa 2010.

Akizungumzia vipaumbele vyake endapo atapewa ridhaa hiyo, Hepautwa alivitaja kuwa ni pamoja na kubuni vyanzo vipya vya ajira kwa vijana na kuboresha huduma katika sekta mbalimbali zikiwemo za afya, maji, elimu, miundombinu ya barabara na biashara.

Kwa upande wa sekta ya biashara alisema mpango wake ni kuwashawishi wafanyabiashara wenye uwezo mkubwa kujenga viwanda vya mazao ya kilimo, kutenga maeneo ya wafanyabiashara wadogo na kuufanya mji wa Iringa kuwa mji wa kibiashara.

“Nataka kuona Iringa unakuwa mji wa biashara za aina zote, magari, vipuri, mitambo, nguo, vyakula na nyinginezo ili waliojirani na CCM wasiende tena Dar es Salaam ili sehemu ya kununua mali wanazohitaji kwa jumla iwe Iringa,” alisema.

Alitaja biashara nyingine zinazoweza kufanywa na wakazi wa Iringa Mjini kuwa ni pamoja na ya kuongoza na kusafirisha watalii ili kuiongezea msukumo wa kutosha.

“Kule kaskazini, vijana wengi kama sisi wamenufaika na mapato yatokanayo na utalii kwasababu wamethubutu kuwekeza katika sekta hiyo. Nataka kuona na sisi wa Iringa tunatumia ujirani wetu na hifadhi ya Taifa ya Ruaha kuchangamkia fursa hiyo,” alisema.

Katika afya alizungumzia namna atakavyosaidia kuboresha huduma hasa za mama na mtoto, mapambano ya virusi vya Ukimwi na upatikanaji wa vifaa tiba na dawa katika vituo vyote vya kutolea huduma.

Katika Jimbo la Iringa mjini, mkoani Iringa chama hicho kimeandaa mikutano kwa wagombea ubunge wote ya kuwatambulisha kwa wanachama ikiwa sehemu ya pili ya mchakato ya kumpata mgombea pekee atakaye peperusha bendera ya chama hicho kwa kushindana na vyama vya upinzani katika Uchaguzi Mkuu Oktoba mwaka huu.

Jumla ya wagombea ubunge 13 Iringa mjini waliochua na kurudisha fomu na wameanza safari ya kuwatambulisha kwa wanachama katika matawi 81 ya CCM Jimbo la Iringa Mjini.

Wana CCM hao wanaoomba nafasi ya ubunge ni pamoja na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Iringa Jesca Msambatavangu, Mkuu wa Wilaya ya Wanging’ombe Frederick Mwakalebala na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Mahamudu Madenge.

Katika orodha hiyo yupo pia Dk Yahaya Msigwa, Nuru Hepautwa, Addo November Mwasongwe, Adestino Mwilinge, Frank Kibiki, Aidani Kiponda, Peter Mwanilwa, Fales Kibasa, Michael Mlowe na Balozi mstaafu Dk. Augustine Mahiga.

UWT CCM MKOA WA IRINGA WACHAGUANA


Rose Tweve

Ritta Kabati

Lediana Mng'ong'o

wajumbe

Zainabu Mwamwindi

wagombea

UMOJA wa Wanawake wa Tanzania (UWT) mkoa wa Iringa umekataa kumuongezea kipindi kingine cha miaka mitano bungeni, Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Iringa, Lediana Mng’ong’o (58) katika mkutano wake wa kura za maoni uliofanyika juzi, mjini Iringa.


Mng’ong’o ambaye pia alikuwa mmoja wa wenyeviti wa bunge la 10 linalomazima muda wake amekuwa mbunge wa viti maalumu mkoa wa Iringa kwa miaka 15.

Friday, 24 July 2015

Kibiki aikumbuka Lipuli, asema ni agenda yake akipata Ubunge




NA MWANDISHI WETU, IRINGA

MGOMBEA wa nafasi ya Ubunge kwa tiketi ya CCM, Mwanahabari Frank Kibiki ameahidi kushirikiana na wadau wa soka kupandisha daraja timu ya soka ya Lipuli ya mjini Iringa iwapo atapewa ridhaa ya kupeperusha bendera ya CCM katika uchaguzi mkuu ujao.

BHALALUSESA ASISITIZA UMUHIMU WA UMAHIRI KATIKA TEHAMA



Kiongozi wa kitaifa wa mradi wa CFIT, Prof. Ralph Masenge akimkaribisha mgeni rasmi Kaimu Kamishina wa Elimu, Benjamin Kulwa (hayupo pichani) kufungua kongamano linalohusu upitiaji wa waraka wa mafunzo ya Tehama kwa wakufunzi wa vyuo vya ualimu linalofanyika mjini Bagamoyo.


Kaimu Kamishina wa Elimu, Benjamin Kulwa akisoma hotuba kwa niaba ya Kamishina wa Elimu, Profesa Eustella Bhalusesa wakati akifungua rasmi kongamano linalohusu upitiaji wa waraka wa mafunzo ya Tehama kwa wakufunzi wa vyuo vya ualimu linalofanyika mjini Bagamoyo. Kulia ni Ofisa Miradi ya Mawasiliano, Habari na Tehama wa Shirika la Kimataifa la Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) nchini, Al Amin Yusuph.

Na Mwandishi wetu, Bagamoyo

KAMISHINA wa Elimu, Profesa Eustella Bhalalusesa amesisitiza haja ya kuhakikisha kwamba viwango vya umahiri vya Tehama kwa wakufunzi wa vyuo vya ualimu nchini vinakua vya juu kukidhi haja ya matumizi ya kufundishia na kujifunza nchini.

Alitoa kauli hiyo mjini hapa wakati akifungua kongamano linalohusu upitiaji wa waraka wa mafunzo ya Tehama kwa wakufunzi wa vyuo vya ualimu.

Thursday, 23 July 2015

KUMEKUCHA WATIA NIA WASHUTUMIANA KWA RUSHWA JIMBO LA IRINGA MJINI


Watia nia Jimbo la Iringa Mjini kushoto ni Peter Mwanilwa, Micheal Mlowe, Mahamudu Madenge, Dk. Yahaya Msigwa, Frank Kibiki na Frederick Mwakalebela wakati wakiongea na waandishi wa habari kuhusu ukiukwaji wa kanunu za uchaguzi wa CCM.





Madenge (katikati) akisoma kanunni hizo kwa wanahabari

WAKATI Joto la uchaguzi likishuka na kupanda mkoani Iringa kada wa chama chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Iringa ambaye pia ni Mwenyekiti wa CCM Mkoa huo na mtia nia kugombea ubunge wa jimbo la Iringa Mjini kwa tiketi ya chama cha mapinduzi CCM, Jesca Msambatavangu ametuhumiwa na makada wenzake wa chama hicho kwa kutoa rushwa kinyume na matakwa ya maadili na kanuni ya chama hicho.

Msambatavangu ametuhumiwa na makada wenzake 11 kati ya 13 ambao wameomba ridhaa ya kuwania kugombea ubunge jimbo la Iringa Mjini kwa tiketi ya CCM .

TOP JOBS FOR THIS WEEK







S/No. COMPANY NAME JOB LINK



3. RELIANCE INSURANCE COMPANY TANZANIA LTD http://www.brightermonday.co.tz/jobs/branch-manager-66




7. THE INTERNATIONAL RESCUE COMMITTEE (IRC) TANZANIA http://www.brightermonday.co.tz/jobs/monitoring-evaluation-coordinator


HERE COMES WOMEN’S EMPOWERMENT SHOW, SUCCESSFUL WOMEN IN THE SPOTLIGH











Educate, Empower and Inspire is a women’s empowerment show. The aim of this show is to put successful women in the spotlight and get a glimpse as to how they are making a difference to our society and how they can inspire others to do the same.

My first guest was Dr. Trish Scanlan who runs the paediatric oncology department at Muhimbili hospital. Since her involvement in 2008, along with her dedicated team of Tanzanian doctors and nurses, the short term survival rates of children with cancer rocketed from 12% to 60%.

WATOTO WAITAKA SERIKALI KUTUNGA SHERIA KALI ...

Na Friday Simbaya, Mufindi  Wanafunzi wa shule za msingi na sekondari wilayani Mufindi mkoani Iringa wameiomba serikali kwa kush...