Friday, 6 May 2011

SIKU YA MALARIA DUNIANI IMANI ZA KISHIRIKINA ZA CHANGIA KUONGEZEKA KWA VIFO

Na Friday Simbaya, Ludewa
WAKATI Taifa likishehekea mafanikio ya kuudhibiti ugonjwa hatari wa Maralia kwa kugawa vyandarua kwa mama wajawazito na watoto walio na umri chini ya miaka mitano Mkoani Iringa bado vyandarua havitoshi, lakini vilivyopo vinatumika kujifunika kama blanketi kujikinga na baridi imefahamika.

Hayo yalithibitika hivi karibuni katika kijiji cha Mbwila Kata ya Luana Ludewa Mkoani Iringa wakati wa maadhimisho ya siku ya malaria kimkoa ambapo mkuu wa wilaya ya Ludewa Bi Georgina Bundalla alimwakilisha Mkuu wa Mkoa huo kama mgeni rasmi.

Desmola Salo (37) aliliambia gazeti hili kuwa vyandarua vinavyotolewa na serikali havitoshi. “” mimi mwenyewe pale nyumbani ninayo familia ya watoto watano, lakini tunacho chandarua kimoja tu ambacho tunakitumia mimi na mume wangu huku watoto wakilala bila chandarua.”” Alilalamika Bi Desmola

Kwa upande wake Bi Evelina Haule (65) na Pendo Kayombo wao walikiri kupokea vyandarua vyenye dawa kutoka kwa mawakala wa mabadiliko katika jamii lakini wao wakaweka bayana kuwa wanatumia vyandarua hivyo kwa kujifunika nje ya shuka kama blanketi kwa kuwa hawajui matumizi vyandarua hivyo.

Bi Georgina Bundalla Mkuu wa Wilaya ya Ludewa aliwataka wananchi kuacha mara moja tabia ya kuamini na kuhusisha ushirikina na ugonjwa wa malaria kwa sababu wanapoteza muda na nguvu nyingi kwa waganga wa kienyeji wakati dalili za malaria ziko wazi ni vema kwenda Hospitalini kupima kwanza kuliko kukimbilia ushirikina. Aliongeza Bundala

“Tunasema malaria haikubaliki kwa sababu inawezekana kuidhibitiwa. Kwa nini ukubali kitu ambacho kinakuletea madhara. Malaria kwanza ina tabia ya kupunguza damu, wengi wetu tuna tabia ya kuchelewa kwenda hospitali na kuwahi kwa mganga wa jadi ambako tunachanjwa na kupunguzwa damu tabia hiyo ife,” alikemea

Meneja wa PSI Kileo Optatus alimwambia mgeni rasmi kuwa malaria ni ugonjwa hatari ambao unaongoza duniani kila baada ya dakika tano hufariki dunia ambapo katika bara la Afrika hasa nchi zilizo chini ya jangwa la Sahara na kuongeza kuwa Tanzania ni nchi ya katika Afrika kwa vifo vinavyotokana na malaria.

“wananchi wa Mbwila na Ludewa kwa ujumla tukishikiana na wadau wengine mbalimbali kwa kuzingatia kanuni zinazotolewa na wizara ya Afya kwa kutumia vyandarua vyenye dawa kila siku kwa mwaka mzima tutafanikiwa kuutokomeza ugonjwa huu wa malaria.”” Alisisitiza Bw Kileo

Mganga Mkuu wa Wilaya ya Ludewa Bw Happines Ndosi alimwambia mgeni rasmi kuwa ugonjwa huu ni hatari hasa katika makundi maalumu kama wajawazito na watoto waliopo chini ya miaka mitano na kwa Kitaifa maadhimisho haya yalifanyika mkoani Arusha kimkoa maadhisho haya yalifanyika wilayani Ludewa na kiwilaya yalifanyika kijiji cha Mbwila.

Mratibu wa malaria mkoa wa Iringa Bi Linda Chatila akitoa takwimu za ugonjwa wa malaria ailimwambia mgeni rasmi kuwa ugomjwa wa malaria unaongoza kwa kuwa na idadi kubwa ya wagonjwa wa nje yaani (OPD) na wale wanaolazwa katika mkoa.

Bi Linda alisema mwaka 2009 malaria iliongoza wagonjwa wa nje chini ya miaka mitano walikuwa asilimia 34.8 ya wagonjwa wote wa umri huo, pia kati ya wagonjwa wote waliolazwa umri chini ya miaka mitano malaria isiyokali iliongoza kwa asilimia 36.6 ya wagonjwa wote waliolazwa katika umri huu. Aidha ugonjwa wa malaria kali uliongoza kwa vifo kwa asilimia 19.5 ya vifo vyote vilivyotokea katika wagonjwa wa kulazwa wenye umri chi ya miaka mitano.

Alisema kwa wagonjwa wa nje wenye umri wa zaidi ya miaka mitano ugonjwa wa malaria ulichukua nafasi ya kwanza sawa na asilimia 24.8 ya wagonjwa wote wa umri huu takwimu hizi zinaonesha kuwa tatizo la malaria bado linaongezeka ingawa jitihada mbalimbali zimefanywa ili kudhibiti tatizo hili.

Wadau wengine wanao jishughulisha na mapambano dhidi ya malaria katika Nyanja mbalimbali mkoani wa Iringa ni pamoja na PSI (T), Chama cha Msalaba mwekundu, Meda, Tagurode, na maajenti wa kuleta mabadiliko katika jamii ambao shughuli zao ni pamoja na kusambaza vyandarua.



ASASI NYINGI NCHINI ZIMO HATARINI KUFA



MASHIRIKA yasiyokuwa ya kiserikali (NGOs) yamo hatarini kufunga milango ya ofisi zao kutokana na viongozi wengi wa mashirika hayo kukosa kabisa utaalamu wa kuandika miradi mbalimbali kwa ajili ya huduma za kijamii na badala yake yanasubiri wafadhili wenyewe wajitokeze jambo ambalo ni gumu sana kwa wafadhili kufanya hivyo imefahamika.

Hayo yalijitokeza jana katika semina ya siku tano ya kuwajengea uwezo viongozi wa mashirika hayo yasiyo ya kiserikali wilayani Ludewa iliyofanyika katika ukumbi wa MTC Mlangali na kuandaliwa na Ludewa Non Governmental Umbrella (LUNGOU) chini ya ufadhili wa The Foundation for civil society ya jijini Dar es salaam.

Pamoja na kuyajengea uwezo mashirika hayo juu ya uandaaji na uandishi wa miradi ya kijamii LUNGOU pia ili iliendesha semina ya ufahamu juu ya utawala bora ndani ya mashirika hayo na katika watumishi na wafanyakazi na watendaji ndani ya serikali na vyombo vya umma.

Akifungua semina hiyo Afisa maendeleo ya jamii wilayani Ludewa Bw. William Malima aliwataka viongozi hao wa mashirika yasiyo ya kiserikali kuacha tabia ya kusubiri wafadhiri waje kuwatafuta badala yake wayatumie mafunzo hayo kuwajengea uwezo wa kuandaa na kuandika wenyewe miradi ili kuwashawishi wafadhili kutoa fedha kwa ajili ya miradi mbalimbali.

Bw. Malima alisema asasi nyingi za kiraia nchini zinakosa pesa kutokana na kutofahamu namna ya kundika maandiko ya miradi (project write up)hata zile chache zinazopata fedha bado zinakabiliwa na tatizo la utawala bora. Utawala bora ni pamoja na jinsi asasi inavyoendeshwa shughuli zake kwa njia ya vikao hasa kwa kukosa uwazi (Transparency) na uwajibikaji yaani (Accountability).

“Ndugu washiriki wa semina kuna umuhimu mkubwa wa kuandika miradi/maandiko ambayo malengo yake ni pamoja na kupata raslimali fedha, rasrimali mitambo (mashine) na vitendea kazi, rasriamali watu wenye ujuzi kama wataalamu ambao leo watatoa mafunzo namna ya kutayarisha na kushawishi wafadhili,”alisema Bw Malima.

Aidha, mgeni rasmi alisema asasi nyingi hushindwa kuandika miradi kwa kutojua ni miradi gani waandike, wakati gani na wapi wapeleke lakini wanasahau kuwa kwa sasa dunia inakabiliwa na matatizo kama ugonjwa wa Ukimwi, Umaskini uliokithiri hasa wa kipato, Uharibifu wa mazingira,Ukosefu wa utawala bora na Ukiukwaji wa haki za binadamu n.k.

Bw. Malima aliwataka washiriki na wadau wengine kwenda kuwaelimisha na kuhamasisha jamii, taasisi na vikundi viweze kuanzisha na kusajili asasi kwani katika Wilaya nzima ya Ludewa kuna asasi 38 tu zilizo hai wakati Tanzania yote hadi 2010 kulikuwa na asasi 6,000 idadi ambayo ni ndogo sana ukilinganisha na nchi ya Ufaransa yenye asasi 80,000 hadi sasa.

Awali akimkaribisha mgeni rasmi Bw. Emanuel Kayombo mwenyekiti wa mwavuli wa mashirika yasiyokuwa ya kiserikali wilayani Ludewa aliwataka washiriki wa semina kushiriki vikamilifu mafunzo hayo kwani ndiyo ukombozi na uhai wa mashirika yao ama sivyo mashirika hayo yamohatarini kufutiwa usajili.

Bw. Kayombo aliwataka wanachama hao wa mtandao (LUNGOU) kutoa viingilio na michango yao ya kila mwaka ili kuweza kupata fedha za kuendeshea ofisi, na kuwataka viongozi ambao hawajasajili asasi zao kwa mwavuli wa mashirika ili kujua shughuli wanazofanya nia ikiwa ni kuepusha migongano ya kuandika miradi inayofanana kwa wafadhili na huduma zinazofanana.

Mkufunzi wa mafunzo hayo na mtaalam wa maandiko Bw Elwin Mligo kutoka Njombe aliwataka washiriki wa mafunzo hayo kuwa makini katika kuandika miradi hasa kutokuchanganya Dira ya shirika, Dhima na Maadili sanjari na kuzingatia mfumo wa mti wa matatizo, mti wa malengo, bo la mantiki na Bajeti bila kusahau visababishi,matatizo na madhara.

Mafunzo yaliyotolewa katika semina hiyo ni pamoja na upangaji na usimamizi wa miradi, uchambuzi wa ndani na nje ya azaki, uchambuzi wa wadau na tathmini ya mahitaji, utayarishaji wa malengo yenye kuzingatia matokeo, kupanga bajeti ya mradi uchambuzi na umuhimu wake, tathmini na ufuatiliaji,viashiria na utawala bora.

Hata hivyo, washiriki wa mafunzo hayo waliomba shirika la The Foundation For Civil society lilifadhili mafunzo hayo kuongeza ufadhili mwingine kwenye mwavuli wao ili kuweza kukamilisha mafunzo hayo kwani muda uliotumika hautishi kumaliza masomo yote jambo lililofanya kukatisha kutokana na ufinyu wa bajeti yenyewe.





MEI MOSI WAFANYAKAZI LUDEWA WAKERWA NA KIBURI NA KEJELI...



.Waajiri na Wakuu wa idara wakwepa kujitokeza kwenye sherehe hizo.



MAADHIMISHO ya sherehe za mei mosi yanayofanyika kila mwaka duniani kote yamewachefua wafanyakazi nchini hususani Wilayani Ludewa kutokana na viongozi na baadhi ya wakuu wa idara kupuuza na kuchelewesha maslahi na stahili za wafanyakazi wa kada za chini.

Akisoma risala kwa niaba ya wafanyakazi wote mwenyekiti wa shirikisho la vyama huru vya wafanyakazi Wilayani Ludewa Mkoani Njombe Bw Joseph Thomas Mvanga alisema waajili wanakatisha tamaa wafanyakazi wao na kusababisha kufanyakazi chini ya kiwango.

Bw Mvanga alizitaja kero hizo kuwa ni pamoja na kuchelewesha mishahara yao ya kila mwezi, kutopandishwa vyeo kwa wakati, mazingira mabaya ya kufanyia kazi, viongozi na waajili kutoa lugha chafu na kejeli kwa wafanyakazi wa kada ya chini, wastaafu kucheleweshewa mafao yao kunapelekea wastaafu waatarajiwa kukata tama na kuingiwa na hofu kila wanapokaribia kustaafu hasa wanapoona mateso wanayopata waliotangulia.

Naye mwenyekiti wa chama cha walimu (CWT) Wilaya ya Ludewa mwalimu William Kunyanja Akimkarisha mgeni rasmi Bw John Mahali ambaye ni katibu tawala wilaya ya Ludewa alisema kero za wafanyakazi zitatuliwe kwa ushirikiano ili kuondoa wasiwasi na kujenga uaminifu baina ya mwajiri na mwajiriwa.

“Inasikitisha sana kuona kila mwaka mei mosi wafanyakazi wanawasilisha kero na malalamiko yao lakini serikali imeziba masikio kama vile haisikii hii inaondoa maana ya maadhimisho haya kwa sababu matatizo kila mwaka tunatoa kero lakini hazitekelezwi”” alilalamika Bw Kunyanja

Alimwambia mgeni rasmi kuwa kupuuzia kunakofanywa na waajili kunaongeza msongo wa mawazo na mheuko kwa watumishi wenye uhitaji wa huduma kutoka kwa viongozi wao na kuitaka serikali kuchukua hatua na kushughulikia kero kwa wakati bila mizengwe na kwamba kwa kufanya hivyo rushwa na uzembe kazini vitakwisha.

Akijibu risala hiyo ya watumishi Bw John Mahali katibu tawala wa wilaya ya Ludewa (DAS)ambaye alimwakilisha Mkuu wa wilaya hiyo aliyekwenda kuhudhria maadhimisho ya mei iliyofanyika kimkoa wilayani mfindi alikiri kuzitambua kero hizo na kusema kuwa zinahitaji ushirikiano katika kuzitatua.

Hata hivyo aliahidi kuzishughulikia kero hizo lakini akawaambia waajili na wakuu wa idara wachache waliohudhuria sherehe hiyo kuwa mei mosi ijayo wawe wamezishughulikia kero hizo. Na kwamba siyo busara kila mwaka wafanyakazi kulalamikia mambo yaleyale.

Hata hivyo Bw Mahali alisikitishwa na tabia mbaya iliyooneshwa na wakuu wa idara katika Halmashauri hiyo na waajili kwa kutohudhuria na kutoshiriki vyema katika viwanja yalipofanyika maadhimisho ya sherehe hizo za mei mosi zilizofanyika kiwilaya katika kata ya Ludewa.

“Katika sherehe kama hizi inatakiwa wakuu wa idara na waajili wawepo wenyewe hapa na kusikiliza kero za watumishi waliochini yao kwa sababu yapo mambo yanayowahusu wao na matatizo mengi yapo chini ya uwezo wao kwa sababu wao ndio wanaoshinda na watumishi hao.” Alisema Bw Mahali

Hata hivyo aliwaagiza waandaaji wa maadhimisho hayo kuwashirikisha waajili wengine wa kutoka katika sekta binafsi kwa sababu mfanyakazi siyo wa serikalini tu na kwamba siyo vizuri kuwatenga watu binafsi na kuwataka waajili kuacha tabia ya kusema njoo kesho hiyo hali imepitwa na wakati.

WASOMALI 87 KIZIMBANI KWA KUINGIA NCHINI BILA KIBALI






WAKIMBIZI 87 wa kabila la wahadia kutoka nchini Ethiopia wamefikishwa katika mahakama ya hakimu mkazi wilayani Ludewa kwa kosa la kuingia nchini kwa makusudi bila ya kibali chochote huku wakijua kufanya hivyo ni kosa kisheria.

Waethiopia hao ambao idadi yao kubwa ni wakristo na muislamu mmoja walikamatwa huko mwambao wa ziwa Nyasa katika kijiji cha Ngelenge Manda wakiwa wanajaribu kuvuka ziwa kwenda nchi jirani ya Malawi ambako wanakwenda kuomba hifadhi kutokana na kukimbia machafuko ya kisiasa nchini kwao.

Akisoma mashtaka mbele ya Hakimu mkazi wa mahakama ya Wilaya ya Ludewa Emanuel Mwambeta (DM) mwendesha mashtaka mratibu msaidizi wa polisi ambaye ni Mkuu wa upelelezi wilaya ya Ludewa ASP Thomas Mtikatika aliiambia mahakama hiyo kuwa washtakiwa walitenda kosa hilo April 13 mwaka majira ya tano asubuhi huko Ngelenge Manda mwambao wa ziwa Nyasa.

Bw Mtikatika aliendelea kuiambia mahakama hiyo kuwa wakimbizi hao wamevunja sheria chini ya kifungu na 31 (1) (i) sheria namba 7 ya uhamiaji ya mwaka 1995 na kwamba kama watapatikana na hatia sheria itazingatiwa ikiwa ni pamoja na kurejeshwa nchini kwao.

Naye Bw Ali Abeid ambaye yuko kitengo cha sheria doria na uchunguzi katika idara ya uhamiaji wilayani Njombe aliongeza kuwa kwa mujibu wa sheria wanaweza kuhukumiwa chini ya kifungu na 31 au kwa mamlaka ya waziri anaweza kutumia kifungu na 14 kinampa mamlaka waziri kumrudisha mhamiaji haramu alikotoka.

Wao dhamira yao ni kwenda Afrika kusini kupitia Malawi na kwamba vipenyo vya kwenda nchi za kusini viko vitatu ambavyo ni Wilaya ya Kyela, Ludewa mkoa wa Iringa na Mbambabay mkoani Ruvuma maeneo hayo ndiyo yanayo sumbua. Hata hivyo washtakiwa wote walikiri kosa na sasa wanasubiri kurudishwa nchini kwao.

Alisema mikakati iliyopo ni kuzima mtandao wa mawakala wanaojihusisha na biashara hiyo ya kuwasafirisha wakimbizi hao haramu kwa manufaa binafsi, kesi hiyo imesikilizwa tena Mei 2 mwaka huu kwa kutekeleza amri kuridishwa kwao kwa mujibu wa mamlaka ya waziri wa mambo ya ndani ya nchi.

“”Awali wahamiaji haramu idadi yao ilikuwa 88, lakini mmoja alifariki dunia April 9 mwaka huu katika kundi la kwanza kutokana na kuugua malaria, kaharisha na kubadili hali ya hewa.”” Alisema Bw Alli

Katika kesi nyingine kijana Jackson Luoga (15) amehukumiwa kifungo kwenda jela mia miwili kwa kosa la kuiba kuku wenye thamani ya shilingi 45,000.



Wednesday, 4 May 2011

MAFISADI WATESA KWA ZAMU!

Na Gustav Chahe, Iringa


Jumla ya watuhumiwa wanane (8) ambao walitakiwa kupelekwa mahakamani kwa sababu za ubadhilifu wa pesa za mradi wa kijiji cha Madege umeingia dosari na wanakijiji kuutupia uongozi lawama za kushindwa kufanya hivyo. Zaidi ya shilingi milioni ishirini na moja (21m/-) za mradi huo ambao unaendeshwa kwa ufadhili wa Districts Agricultural Development Programme Support (DADS), yaani mpango wa kilimo wilayani, kutoka Denmark ulitiwa dosari na baadhi ya wanakijiji walioamua kujinyakulia fedha kinyemela na kuzitia mifukoni mwao.

Kijiji hicho kilipata bahati ya ufadhili wa mashine mbili zenye vinu vya kukoboa na kusaga kwa ajili ya maendeleo ya kijiji hicho licha ya kuwa kinakabiliwa na changamoto mbalimbali za kila aina ambazo zinahitaji nguvu kubwa itumike ili kujikwamua nazo.

Hasara hiyo inatokana na usimamizi mbovu wa wale waliopewa dhamana na kijiji kusimamia ikiwa ni pamoja na kutokuwa na na mwongozo wa uendeshaji na kuzitumia mashine hizo kama mali zao binafsi kwa ajili ya maslahi yao. Kwa kutochukuliwa hatua yoyote watuhumiwa hao kunatokana na ama kula njama moja na viongozi hao au kwa kile kinachosadikiwa na wengi kuwa ni hali ya kulindana ili kuepusha kuumbuana pindi watakapo kuwa kizimbani kwa ajili ya kutolea maelezo juu ya ubadhilifu huo. Itakumbukwa kuwa mmoja wa watuhumiwa alipohojiwa na mwandishi hapo katika makala ya awali alieleza kuwa haogopi kwenda mahakamani kwa kuwa kule ndiko atakakotolea maelezo ya ukweli na uhakika.

Bw. Elenasi Kikoti ambaye ni miongoni mwa watuhumiwa alidiriki kusema hivyo kwa mwandishi kwa kile alichosema hawezi kumwambia mtu yeyote siri aliyo nayo hadi kitakapoeleweka mahakamani hiko kwani akiongea mapema anaweza akageuziwa ubaya. “Ukweli mwandishi mimi siwezi ni katoa siri niliyonayo sasa hivi ili tutakapofika mahakamani ndiko nitakako toa siri yangu na kuzungumza ukweli kutokana na mambo ninayoyajua kuhusiana na mradi huu na mengine ambayo si ya mradi huu, lakini yanahusiana na maendeleo ya kijiji” alisema Bw. Kikoti.
Kwa mujibu wa ripoti ya tume iliyoundwa kwa ajili ya uchunguzi wa mradi huo, lilikuwa na orodha ya watuhumiwa ambao wanahusika moja kwa moja kujibu tuhuma na kustahili uadabishwa juu ya ubadhilifu wa pesa hizo. Ripoti hiyo imeorodheshwa majina ya Santina Msuva, Zamda Mtenga, Waride Sechambo, Elenasi Kikoti, Jasimini Kikoti pamoja na Boazi Kadinda, Athumani Kisima na Elisha Mhile. Mradi huo ulianza tangu mwaka 2006 ambao ulilenga kukinufaisha kijiji hicho chenye wakazi 2,225 pamoja na maeneo jirani ambao hutegemea kilimo katika kujipatia mahitaji yao ya kila siku na kuwajibika katika shughuli mbalimbali za maendeleo yao binafsi, kijiji hata kwa ajili ya maendeleo ya kitaifa kwa ujumla.

Aidha, Lesamu Msuva naye anaingizwa katika tuhuma hizo kwa kushindwa kuwajibika katika tatizo hilo wakati wa uongozi wake alipokuwa Diwani katika Kata hiyo katika kipindi cha awamu ya kwanza ya uongozi wa Rais Jakaya Kikwete. Mheshimiwa huyo anaingizwa katika kundi hilo kwa kile kinachodaiwa ufisadi kwake lilikuwa ni jambo la kawaida kwani aliogopa kuwakoromea wenzake kwa kuwa hata yeye wanakula sahani moja. Kama isemwavyo “mtoto umleavyo, ndivyo akuavyo”, kutokumuadabisha fisadi ni kuna maanisha kuwa hali hii ni ya kawaida kwa kuwa hakuna aliye safi wa kumuondoa mwenzake au wa kumkaripia na kumchukulia hatua. Hii ni kwa sababu ya usemi usemwao “ndege wenye mabawa yanayofanana, huruka pamoja”, ndivyo ilivyo hata kwa watu wa namna hiyo kulindana kwa ili wasiumbuane, lakini pindi inapotokea mmoja ameumbuka huwa inakuwa tafrani kubwa kwa maswahiba hao.

Awali akiongea na mwandishi wa habari hizi, Afisa Mtendaji wa kijiji hicho Bw. Elijus Kikoti alisema kuwa watuhumiwa hao wanatarajiwa kufikishwa mahakamani wakati wowote utaratibu utakapokuwa umekamilika. Kadiri siku zinavyozidi kwenda hali ya kijiji inazidi kuwa mbaya kutokana na watu kutojitokeza kwa uwingi katika kutumia nguvu zao katika maendeleo ya kijiji hususani katika michango, na kujitoa pale wanapotakiwa kutumia nguvu zao.

Ikiwa viongozi wa kijiji hicho walikanusha madai ya wanakijiji kuwepo na hali ya kuogopana na viongozi kula sambamba na watu wanaotia hasara maendeleo ya kijiji hicho, hali inazidi kuonekana wazi kwa tuhuma hizo. Kiongozi mmoja ambaye jina tunalo, alipohojiwa na mwandishi wa makala haya juu ya kujihusisha na wanaosadikiwa kuwa ni wabadhilifu wa miradi ya maendeleo ya kijiji, alieleza kuwa wao hawatakuwa wa kwanza kujihusisha na watu kama hao wakati wapo wengi wanaofanya hivyo. “Siwezi kukubali au kukata, watanzania wa leo siyo wajinga kiasi kwamba wanaweza kudanganywa kirahisi. Najua watakuwa wanaongea wanachokijua. Kama ni hivyo, hatutakuwa wa kwanza sisi kufanya hivyo kwa sababu hata ukiangalia jinsi nchi inavyokwenda tunasikia kabisa hata ngazi za juu wanafanya hivyo sembuse na sisi ambaye ni wadogo kabisa. Kumbuka mwandishi kuna usemi ambao husemwa “mtoto wa nyoka ni nyoka tu” alieleza kiongozi huyo.

Kiongozi huyo ambaye aliomba jina lake lisiandikwe alieleza waziwazi kuwa mpango huo kautatimia endapo safu ya uongozi uliopo haitafanyiwa marekebisho kwani haiwezekani watu wanaokula pamoja wakatafutana ubaya. “Ninaomba unilinde jina langu ili nikwambie ukweli. Ninakwambia, kama watuhumiwa hawa watapelekwa mahakamani tutaona. Ninasema hivi kwa sababu ninajua; miongoni mwetu tunakula sahani moja na watuhumiwa kwa hiyo mpango wa kuwapeleka watuhumiwa mahakamani utabaki maneno tu hadi utakapopotea tu hewani kwa sababu si rahisi wakafanya usaliti wanaoijua siri yote” alisema.

Mpango wa kuwapeleka watuhumiwa wa ubadhilifu wa fedha za mradi wa DADS wa kijiji cha Madege mahakamani umeota mabawa na kuwaacha watuhumiwa wakitesa kwa zamu kijijini hapo kwa raha zao. Watuhumiwa hao imeshindikana kupelekwa mahakamani kutokana na udhaifu wa uongozi wa kijiji hicho kuingiza udugu na urafiki badala ya kuwajibika katika nafasi zao za kiutendaji katika kuwahudumia wananchi.

Awali wananchi waliilalamikia serikali ya kijiji hicho kuwachukulia watuhumiwa kama ndugu zao na kuwakingia kifua ili suala liweze kupotea bila maelezo na kuwaacha wananchi gizani bila kujua kinachoendelea. Mradi huo ulitiwa dosari na baadhi ya wanakijiji hicho walioamua kujinyakulia fedha kinyemela na kuzisweka wanakokujua wao na kuwaacha wanakijiji wakihaha bila kupata majibu huku wakipoteza nguvu zao kwa ajili ya maendeleo ya kijiji.

Itakumbukwa awali wananchi walidai kuwepo na hali ya kubebana ambako ni sababu kubwa inayosababisha kutowafikisha watuhumiwa hao mahakamani. Maelezo ya viongozi wa kijiji yalionekana kwenda tofauti na kauli za wananchi kwa kile walichokieleza kuwa hawezi kumuogopa mtu yeyote kwa namna yoyote ile. Hali inazidi kuwa mbaya kutokana na mashine hizo kusimama badala ya kuhudumia wanakijiji huku wanakijiji wakibaki na mahangaiko yasiyokuwa na majibu na viongozi wao wakiendelea kubaki kimya. Bado wanakijiji wanaendelea kulalamika ili haki iweze kutendeka na sheria iweze kuchukua mkondo wake dhidi ya watuhumiwa hao vinginevyo hali si shwari. Wakizungumza na mwandishi wa makala haya kwa nyakati tofauti, wanakijiji wanaulalamikia uongozi wa kijiji hicho kuwa wanafanya kazi kwa upendeleo huku wengine wakiumia kwa ajili ya maendekeo ya kijiji. “Ndugu mwandishi, sisi wanakijiji tupo gizani hadi sasa kuona viongozi wetu wanakaa kimya bila kutuelekeza ni nini kinaendelea kwa watuhumiwa hao wanaotutesa sisi wengine” anasema mwanakijiji mmoja.

Pia anasema ni bora kutolea maelezo kama wanashindwa badala ya kukaa kimya kwani wapo wanakijiji ambao wanaweza wakalifanya hilo kwa ufanisi kulingana na uchungu wao kwa kijiji na nguvu zao wanazozipoteza kwa ajili ya maendeleo ya kijiji hicho. “Kama wanashindwa kufanya kazi na kuwapeleka watuhumiwa hao mahakamani watueleze ili sisi wanakijiji tujue la kufanya; tunaweza tukawateua watu ambao tunawaamini walisimamie suala hilo kuwapeleka mahakamani” anasema mwanakijiji huyo.

Naye katibu wa kamati ya uchunguzi wa mradi huo Bw. Felix Kayage anaeleza kuwa, tatizo ni porojo nyingi kuliko uwajibikaji na ndiyo maana maendeleo ya kijiji yanazidi kudumaa. “Ukweli ni kwamba porojo ni nyinyi kuliko uwajibikaji na ndiyo maana tunashindwa kufanya kazi za msingi; kama uwajibikaji ungekuwa wa kifanisi, watu kama hao wasingekuwa wanafumbiwa macho kwa muda wote huo na kusabasha hasara kuendelea kujitokeza zaidi” anasema Bw. Kayage. Taarifa za kuaminika zilizolifika gazeti hili zinasema, moja ya mambo ambayo yanakwamisha maendeleo katika kijiji hicho ni kuwepo kwa undugu zaidi kuliko uwajibikaji wa viongozi katika nafasi zao kwa kutenda haki. “Ndugu mwandishi, hiki kijiji hakiwezi kuendelea kamwe kutokana na viongozi kuendekeza undugu na urafiki badala ya kuwajibika katika nafasi zao. Tabia hii ndiyo inayotumaliza sisi wananchi kila kunapokucha kwa kuwa hata anayeonekana kwenda kinyume na utaratibu wetu akiowa ni rafiki wa kiongozi au ndugu wa kiongozi, hawezi kuadabishwa” kinasema chanzo hicho. Katika maelezo ya wanakijiji waliowengi, wanakijiji wanazidi kukata tamaa siku hadi siku kutokana udhaifu walionao viongozi wao kiutendaji na kuwajibika katika malalamiko na ushauri wao kwa ajili ya ufanisi bora.



Monday, 2 May 2011

BREAKING NEWS- OSAMA BIN LADEN IS KILLED

By JULIE PACE and MATT APUZZO, Associated Press Julie Pace And Matt Apuzzo, Associated Press – 50 mins ago


WASHINGTON – Osama bin Laden, the glowering mastermind behind the Sept. 11, 2001, terror attacks that killed thousands of Americans, was slain in a firefight Sunday with U.S. forces in Pakistan, ending a manhunt that spanned a frustrating decade.

"Justice has been done," President Barack Obama said in a dramatic late-night announcement at the White House.

A jubilant crowd of thousands gathered outside the White House as word spread of bin Laden's death. Hundreds more sang and waved American flags at Ground Zero in New York — where the twin towers that once stood as symbols of American economic power were brought down by bin Laden's hijackers 10 years ago.

Another hijacked plane slammed into the Pentagon on that cloudless day, and a fourth was commandeered by passengers who forced it to the ground before it could reach its intended target in Washington.

U.S. officials said the helicopter raid in Pakistan was carried out by CIA paramilitaries together with the elite Navy SEAL Team Six. The U.S. team took custody of bin Laden's remains, which American officials said were being handled in accordance with Islamic tradition.

The death marks a psychological triumph in a long struggle, although its ultimate impact on al-Qaida is less clear.

The greatest terrorist threat to the U.S. is now considered to be the al-Qaida franchise in Yemen, far from al-Qaida's core in Pakistan. The Yemen branch almost took down a U.S.-bound airliner on Christmas 2009 and nearly detonated explosives aboard two U.S. cargo planes last fall. Those operations were carried out without any direct involvement from bin Laden.

Obama said he gave the order for the operation after receiving intelligence information that he did not further describe.

Former President George W. Bush, who was in office on the day of the attacks, issued a written statement hailing bin Laden's death as a momentous achievement. "The fight against terror goes on, but tonight America has sent an unmistakable message: No matter how long it takes, justice will be done," he said.

Senior administration officials said the terrorist mastermind was found inside a custom-built compound with two security gates. They said it appeared to have been constructed to harbor one high-value target and that for undisclosed reasons, officials believed the hideout was bin Laden's.

Officials also said they believe the death puts bin Laden's al-Qaida on a path of decline that will be difficult to reverse, but there was no word on the whereabouts of bin Laden's second-in-command, Ayman al-Zawahri.

The stunning end to the world's most widely-watched manhunt came just months before the 10th anniversary of the Sept. 11 attacks on the World Trade Centers and Pentagon, orchestrated by al-Qaida that killed nearly 3,000 people.

The attacks a decade ago seemed to come out of nowhere, even though al-Qaida had previously struck American targets overseas.

The terrorists’ hijacked planes flew one of them into one of Manhattan's Twin Towers — and, moments later, into the other one. Both buildings collapsed, trapping thousands inside and also claiming the lives of firefighters and others who had rushed to help them.

A third plane slammed into the Pentagon, defacing the symbol of America's military night. Officials have speculated that the fourth plane had been heading for the U.S. Capitol or perhaps even the White House when it crashed in Pennsylvania.

The attacks set off a chain of events that led the United States into wars in Afghanistan, and then Iraq, and America's entire intelligence apparatus was overhauled to counter the threat of more terror attacks at home.

A senior administration official said Obama gave the final order for U.S. officials to go after bin Laden on Friday. The official added that a small team found its quarry hiding in a large home in an affluent suburb of Islamabad. The raid occurred in the early morning hours Sunday.

Administration officials offered some details of the operation.

Based on statements given by U.S. detainees, intelligence officials have known for years that bin Laden trusted one al-Qaida courier in particular, and they believed he might be living with him in hiding. In November, intelligence officials found out where he was living, a huge fortified compound in an affluent suburb of Islamabad. It was surrounded by walls as high as 18 feet high, topped with barbed wire. There were two security gates and no phone or Internet running into the house.

Intelligence officials believed the $1 million home was custom-built to harbor a major terrorist. CIA experts analyzed whether it could be anyone else, but time and again, they decided it was almost certainly bin Laden.

Three adult males were also killed in Sunday's raid, including one of bin Laden's sons, whom officials did not name. One of bin Laden's sons, Hamza, is a senior member of al-Qaida.

Obama spoke with Bush and former President Bill Clinton Sunday night to inform them of the developments.

The president struck a less than boastful tone in his brief announcement, although he said the death of bin Laden was "the most significant achievement to date in our nation's effort to defeat al-Qaida.

"His death does not mark the end of our effort. There's no doubt that al-Qaida will continue to pursue attacks against us. We must and we will remain vigilant," he added.

Moments after Obama spoke, the State Department put U.S. embassies on alert and warned of the heightened possibility for anti-American violence. In a worldwide travel alert, the department said there was an "enhanced potential for anti-American violence given recent counterterrorism activity in Pakistan."

____

Associated Press reporter Kimberly Dozier contributed to this story..



OSAMA BIN LADEN

MBUNGE AFADHILI MASHINDANO YA MEI MOSI

Mbunge wa Jimbo la Peramiho katika Wilaya Songea vijijini mkoani Ruvuma, Mhe. Jenista Mhagama akifuatilia kwa umakini mkubwa mechi kati ya wafanyakazi wa misioni (Abasia Peramiho) na watumishi wa serikali jana wakati wa maadhimisho ya siku ya wafanyakazi duniani maarufu kama (MEI MOSI), yaliyofanyika katika viwanja vya Peramho. Wanaomfuatia ni Diwani wa Kata ya Peramiho, Izack Mwimba (katikati) pamoja na Dr. Bonus Mtega wa Hospitali ya Peramiho. Katika mechi hiyo Timu ya Abasia Peramiho iliichapa Timu ya watumishi wa serikali  mabao 4-2. (PICHA: FRIDAY SIMBAYA)

Sunday, 1 May 2011

TIMU YA PERAMIHO YAIBAMIZA TIMU YA SERIKALI 4-2, MEI MOSI

Na Friday Simbaya,


Peramiho

Timu ya wafanyakazi wa misioni ya Abasia Peramiho imeichapa Timu ya watumishi wa serikali mabao 4-2 Jumapili katika mashindano ya Mei Mosi 2011, yaliyofanyika katika viwanja vya Peramiho misioni, yakiwa ni sehemu ya maadhimisho ya siku ya wafanyakazi duniani, wilayani Songea vijijini mkoani Ruvuma.

Katika mechi hiyo kipindi cha kwanza timu zote mbili ziliaanza kwa kushambuliana, ambapo timu ya Peramiho Misioni walifanikwa kupata magoli mawili ya chapuchapu ambapo timu ya watumishi wa serikali hawakupata chochote hadi kipindi cha kwanza kimalizika.

Kipindi cha pili kilipoanza timu ya watumishi iliaamka kutoka usingizini na kushumbulia lango la abasia ya Peramiho bila mafanikio na matokeo yake kuaacha mwanya kwa timu ya Abasia kuongeza magoli mengine mawili.

Timu ya Abasia walibweteka na ushindi wa magoli manne na kuwadharau ndipo timu ya watumishi walicheza kufa na kupona na kurudisha magoli mawili dakika za mwisho na mpira kumaliza kwa matokeo 4-2, ambapo timu ya Abasia walitoka kifua mbele na zawadi ya shilingi 50,000/=.

Mbunge wa Jimbo la Peramiho, Jenista Mhagama alikuwa nidiye mgeni rasmi na mfadhili wa mashindano hayo ya Mei Mosi 2011, alishukuru timu zote mbili kwa kujitokezana kucheza vizuri bila ugomvi.

Wageni wengine walioambatana na mbunge huyo ni pamoja na Diwani wa Peramiho Izack Mwimba, wenyeviti wa vijiji vya Peramiho ‘A’ na Peramiho ‘B’ na watendaji wa vijiji hivyo.

Mbunge huyo ambaye ndiye mfadhili wa mashindano yaliyoshirikisha timu za soka za wafanyakazi wa misioni na watumishi wa serikali na kukabidhi zawadi ya shilingi hamsini taslimu (50,000/=) kwa timu wa Abasia Peramiho na timu ya watumishi wa serikali nao waliambulia shilingi 30,000/=.

Kwa upande wa mchezo wa mpira wa pete timu ya Abasia iliibuka na ushindi wa mezani baada ya timu ya watumishi wa serikali kushindwa kufika kiwanjani, na kupatiwa zawadi ya shilingi 50,000/-.

Aidha, mbunge huyo wa Peramiho alielezea kupungua kwa zawadi kwa mwaka huu ikilinganishwa na mwaka jana kuelekeza nguvu kwa timu ya soka ya Wilaya ya Songea vijijini daraja la kwanza itakayo wakilisha mashindano ya ligi ya daraja.


Mbunge wa Jimbo la Peramiho, Jenista Mhagama (katikati) akifantilia mashindano ya Mei Mosi kwa makini akiambatana na Diwani wa Peramiho, Izack Mwimba (wa kwamza kushoto)

Timu ya wafanyakazi wa Abasia ya Peramiho ya wanawake upande mpira wa pete.


Mbunge Jenista Mhagama akisalimia Timu ya watumishi wa serikali kabla mechi kuanza katika viwanja vya Peramiho.


Mpira wa kona katika lango la Timu ya Peramiho wenye jezi ya mistali mweupe na golikipa wao mwenye tracksuit ya rangi damu ya mzee.

Kiongozi wa Timu ya Abasia (Netiboli) akipekea zawadi kutoka kwa mbunge Jenista Mhgama wa pili kutoka kulia.

Timu ya watumishi wa serikali wakipata zawadi ya shilingi 30,000/= kama mshindi wa pili katika mchezo wa soka.


Mabingwa wa mashindina ya Mei Mosi 2011 ambao ni Timu ya Abasia ya Peramiho wa kupita zawadi ya 50,000/= kutoka kwa mbunge, ikiwakirishwa na kepteni timu mwenye t-shirt ya bendera ya Marekani na begi mgongoni.



Timu ya wafanyakazi wa Abasia Peramiho katika picha ya pamoja kwa mechi.





Timu ya soka ya watumishi wa umma katika picha ya pamoja kwa kabla ya mechi.

Saturday, 30 April 2011

BREAKING NEWS

Kesho ni Siku Kuu ya Wafanyakazi duniani (Mei Mosi), ambapo timu ya soka ya wafanyakazi wa misioni Peramiho itamenyana na timu ya watumishi wa serikali katika viwanja vya Peramiho wilayani Songea, mkoani Ruvuma, ikiwa ni sehemu yao ya maadhimisho ya siku ya wafanyakazi duniani. Pia timu ya wanawake ya mpira wa Pete (Netball) ya Peramiho vile vile itashuka dimbani kumenyana na timu ya wafanyakazi wa serikali katika mechi zitakazoanza Saa Kumi jioni. Mgeni Rasmi anatarajia kuwa Mbunge wa Jimbo la Peramiho, Mhe. Jenister Mhagama (CCM) akiambatana na viongozi wengine chama hicho na viongozi serikali. 

TATIZO LA TAKA MJINI SONGEA IN KUBWA

This is what has been is in Songea  Municipal Council in Ruvuma Region, a lot of trash has not been collected for a long time hence causing health hazard to the residents staying nearby those dumpsites. This garbage was captured by the roving cameraman today along Kaulu Street towards Police line area. Many areas in the town of Songea have uncollected rubbish.

WATOTO WAITAKA SERIKALI KUTUNGA SHERIA KALI ...

Na Friday Simbaya, Mufindi  Wanafunzi wa shule za msingi na sekondari wilayani Mufindi mkoani Iringa wameiomba serikali kwa kush...