Saturday, 13 June 2015

International Albinism Awareness Day!



It was on June 13, 2013 that the UN adopted its first resolution on albinism. The UN resolution instating International Albinism Awareness Day, came 17 months later, recognizing the need to increase awareness and understanding of albinism in order to fight against global discrimination and stigma against persons with albinism.


Awareness raising activities are taking place all over the world including a UTSS commemoration ceremony and program at the Sengerema Monument in Mwanza, Tanzania. Click here to learn more: www.albinismday.com


Leading up to this special occasion, UTSS launched the Hat Giving Challenge on June 1st, because simple items like HATS AND SUNSCREEN CAN HELP PREVENT the deadly skin cancer that claims the lives of most people with albinism in Tanzania before their 40th birthday. WE THANK THE MANY OF YOU WHO HAVE ALREADY PARTICIPATED! To date we've raised enough to buy 124 hats and 198 sunscreens, and the word about this preventable issue is spreading.

Friday, 12 June 2015

MAHAMOD MGIMWA ANOGESHA ZAWADI ZA MSHINDI WA KOMBE LA MUUNGANO







naibu waziri wa maliasili na utalii mahamod mgimwa ambye pia mbunge wa jimbo la mufindi kasikazini.



hapa mabingwa wa kombe hilo wakishangia ushindi pamoja na mgeni rasmi pamoja na viongozi mbalimbali.



mratibu wa mashindano hayo aliyetangaza kustahafu kuratibu mashindano hayo. 




na fredy mgunda,iringa

akizungumza wakati wa kufunga mashindano ya kombe la muungano mratibu wa kombe hilo DAUDI YASSIN alimpongeza mbunge wa mufindi wa jimbo la mufindi kasikazini ambaye pia ni naibu waziri wa maliasili na utalii MAHAMOD MGIMWA kwa kisaidia kutoa zawadi.

UN YATAKA KUWEZESHWA ZAIDI KWA SERIKALI ZA MITAA





Balozi wa Spain nchini, Mh. Luis Cuesta Civis (kushoto) na Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez (wa pili kushoto) wakikagua mitaala ya kufundishia kwenye ofisi za walimu katika shule ya msingi Yombo ambayo imejengwa na mradi wa awamu ya pili wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) iliyopo katika kijiji cha Chasimba, wilayani Bagamoyo mkoa wa Pwani, wakati wa kukagua miradi inayofadhiliwa na TASAF wilayani humo huku Afisa Program Kitengo cha Uahulishaji Fedha (TASAF), Edith Mackenzie (wa pili kulia) akitoa maelezo kwa ugeni huo.(Picha na Zainul Mzige wa Modewjiblog).

Na Mwandishi Wetu, Bagamoyo

MRATIBU Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini Tanzania Alvaro Rodriguez ametaka serikali za tawala za mikoa na serikali za mitaa kuwezeshwa zaidi ili kuweza kuwatumikia wananchi.

Aliyasema hayo wakati alipozuru kijiji cha Chasimba mwishoni mwa juma akiwa na Balozi wa Hispania Luis Cuesta Civis kuona miradi ya maendeleo inayofadhiliwa kwa pamoja kati ya serikali ya Tanzania, Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Ubalozi wa Hispania.

Mratibu huyo alisema kwamba mafanikio makubwa yanayoonekana katika kijiji cha Chasimba ni matokeo ya ushirikiano mzuri wa wadau wa maendeleo na wanakijiji.

Alisema ushirikiano huo ni muhimu katika kutokomeza umaskini uliokithiri katika jamii.

Alisema pamoja na mafanikio hayo Umoja wa Mataifa na wadau wengine wa maendeleo wangelipenda kuona serikali za mitaa zinawezeshwa zaidi ili kuweza kusaidia jamii kama inavyofanyika sasa katika kijiji cha Chasimba.

Kijiji hicho ni miongoni mwa vijiji kadhaa nchini vinavyofaidika na mpango unaotekelezwa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii, TASAF, ambao nao unachangiwa na mashirika ya Umoja wa Mataifa na wadau wengine wa maendeleo.

Alisema anapenda kuona kwamba maisha ya wakazi wa kijiji hicho yanabadilika na kuwa kama ya mama Kicheko ambaye ameondoka katika umaskini uliokithiri baada ya kutumia vyema mradi uliofikishwa kijijini hapo.

Alitoa wito kwa wadau wa maendeleo na mashirika ya kimataifa kusaidia kuwezesha serikali za mitaa na mashirika yanayoapambana na umaskini nchini kuwezesha miradi ya kuondoa umaskini kufanikiwa.

Bi. Kicheko ambaye mwaka mmoja uliopita alikuwa hohehahe kwa sasa anatengeneza sabuni, ameboresha nyumba yake kwa kuiwekea bati na ana kula mlo zaidi ya mmoja sasa.

Katika ziara hiyo, Mratibu huyo alitaka kujua wananchi wa Chasimba katika miaka mitano hadi saba ijayo wanataka kuwaje na kujibiwa kwamba wanataka kuwa na hali bora zaidi ilivyo sasa na kuanzisha viwanda vidogo.


Balozi wa Spain nchini, Mh. Luis Cuesta Civis (kushoto) na Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez (kulia) wakipitia baadhi ya kurasa za mwongo wa kufundishia kitabu cha Uraia wakati wa ziara ya kukagua miradi inayofadhiliwa na TASAF wilayani Bagamoyo mkoa wa Pwani.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF), Ladislaus Mwamanga, alisema mpango huo wa miaka 10 ambao umeingia katika mwaka wa tatu umelenga kuwezesha afya, elimu na lishe na sasa wanafanya kuwajengea uwezo wa kuweka akiba na kuwekeza.

Alisema uwekaji akiba huo unawezekana kwa kutoa ajira wakati wa vipindi vigumu.

Alisema mpango huo wa kukabili umaskini uliokithiri unachangiwa pamoja na Benki ya Dunia, Shirika la Maendeleo la Uingereza, Shirika la maendeleo la Sweden na serikali ya Tanzania.

Alisema kuna kaya milioni moja zinazokula mlo mmoja ambazo zinatakiwa kubadilishwa kuwa katika hali bora.

Aidha alisema wameshakamilisha kutengeneza ramani ya umaskini baada ya kumaliza kuandikisha kaya maskini zilizopo nchini.

Diwani wa kata ya Yombo ambapo kijiji cha Chasimba aliyejitambulisha kwa jina la Idd alisema kwamba ni matarajio yao katika miaka 10 ijayo kubadilika kabisa kutokana na kijiji hicho kuwa na umeme na maji ya kutumia.

MEMBE: TUMCHAGUE RAIS MWENEYE HEKIMA NA BUSARA


WAGOMBEA urais waendelea kumiminika mkoani Iringa kusaka wadhamini wakutia saini fomu za udhamini kwa ajili ya kuteuliwa uwania urais katika Uchaguzi Mkuu mwaka huu kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe amepata wadhamini 380 mkoani Iringa katika harakati zake za kuomba kuteuliwa na Chama cha Mapinduzi (CCM) kuwania urais katika Uchaguzi Mkuu wa Mwaka huu.

Thursday, 11 June 2015

JANUARY MAKAMBA APATA WADHAMINI 680 MKOANI IRINGA LEO!



Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Januari Makamba ambaye pia ni Mbunge wa Bumbuli akiwatambulisha wasanii walioambatana nao ambao ni  Fid Q na Mwana FA.

Wasanii P. Funky Majani na Ditto wakisiliana wakazi wa Iringa, wasanii waliambatana msafara wa January Makamba ambaye anatafuta wadhimini katika mikoa mbalimbali Nyanda za Juu Kusini.

Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Januari Makamba ambaye pia ni Mbunge wa Bumbuli (CCM) akimtambulisha mke wake.

MASHINDANO YA MUUNGANO YAMEFIKIA MWISHO KWA MAFANIKIO MAKUBWA SANA,HUKU DAUDI YASSINI AKING’ATUKA



DAUDI YASSINI AKIMKARIBISHA MKUU WA WILAYA YA MUFINDI MBONI MAHITA KATIKA UWANJA WA WAMBI MJINI MAFINGA





MKUU WA WILAYA MBONI MAHITA AKIKAGUA TIMU KABLA YA MCHEZO





MSIMAMIZI DAUDI YASINI NA MGENI RASMI MBONI MAHITA WAKIWA KATIKA PICHA MOJA NA MABINGWA WA MUFINDI CUP TIMU YA MKOBA





MSIMAMIZI DAUDI YASINI NA MGENI RASMI MBONI MAHITA WAKIWA KATIKA PICHA MOJA NA TIMU YA DODOMA ACADEMY





SEHEMU YA MASHABIKI WA WALIOJITOKEZA KATIKA MCHEZO HUO WA FAINALI

ADAI FIDIA KWA MWAJIRI BAADA YA KUKATWA VIDOLE VINNE AKIWA KAZINI!


Aliyekuwa mfanyakazi wa Kiwanda cha FibreBoards 2000 Ltd Arusha, Tawi la Mafinga Jane Paschal Nziku (19) akionesha mkono wake wa kulia uliokatwa vidole vinne na kubakia na kidole gumba. Aliyemshika mkono ni kaka yake Omary Mbilinyi. (PICHA NA FRIDAY SIMBAYA)

KIWANDA cha Fibre Boards 2000 Ltd cha Arusha, Tawi la Mafinga kunadaiwa fidia na mfanyakazi wake ambaye alipata ajali akiwa kazini ambapo katika ajali hiyo alipoteza vidole vinne vya mkono wa kulia na kubakia na kidole gumba.

Mfanyakazi huyo, Jane Paschal Nziku (19) pichani mwenye elimu ya kidato cha nne na mkazi wa Mafinga alipata ajali ya kazini tarehe 24.12.2014 katika kiwanda kinachomilikiwa na Darshan Singh kilichopo mjini Mafinga wilayani Mufindi, mkoani Iringa.

Wednesday, 10 June 2015

LIGI YA UJIRANI MWEMA SAOHILL YAANZA KUTIMUA VUMBI

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Mahmood Mgimwa ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Mufindi Kusini akifungua mashindano ya Ligi ya  Ujirani Mwema yalioandaliwa kwa udhamini wa Shamba la miti Sao Hill mjini Mafinga wilayani Mufindi, mkoani Iringa jana. walioketi kutoka kushoto ni Meneja wa Shamba la miti Sao Hill Salehe Beleko na Mwenyekiti wa CCM (W) Mufindi ambaye pia Diwani wa Kata ya Makungu Yohanes Cosmas Kaguo

Meneja wa Shamba la miti Sao Hill, Salehe Beleko (kushoto) akisalimia na golikipa wa Timu ya Ihalimba Vijijini FC kabla ya mechi kuanza.


Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Mahmood Mgimwa (kulia) ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Mufindi Kusini akiwasili katika viwanja vya Ihefu kwa ajili ya ufunguzi wa Ligi ya Ujirani Mwema ya Sao Hill jana.




SAOHILL imeanzisha mashindano ya Ligi ya Ujirani Mwema kwa kushirikisha vijiji vinavyozunguka shamba hilo ili kulinda na kutunza rasilimali za misitu na nyuki.

Mwenyekiti wa Kamati ya Michezo, Said Aboubakar alisema kuwa Ligi ya Ujirani Mwema itashirikisha timu nane ambazo ni Ihefu Misitu, Ihalimba Mseto, Ihefu Mseto, Mgololo Misitu, Mgololo Mseto, Irindi Misitu na Irindi Mseto zilizogawanywa katika makundi A na B.

HISPANIA YASAIDIA BILIONI 3.1/- KUKABILI UMASKINI TANZANIA


Balozi wa Spain nchini, Mh. Luis Cuesta Civis (kulia) na Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez (katikati) wakiwasili kwenye ofisi za Halmashauri ya wilaya ya Bagamoyo kabla ya ziara ya kuelekea katika kijiji cha Chasimba kukagua miradi inayofadhiliwa na TASAF katika wilaya ya Bagamoyo. Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF), Ladislaus Mwamanga.(Picha na Zainul Mzige wa modewjiblog).

SERIKALI ya Hispania imetoa shilingi bilioni 3.1 kusaidia miradi ya maendeleo ya jamii nchini ambayo mingine inatekelezwa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii, TASAF.

Tuesday, 9 June 2015

POLISI MKOANI IRINGA WAKAMATA MAGUNIA MATATU YA BANGI



Polisi mkoani Iringa wamefanya msako kali kwa kushirikiana na vyombo vingine vya ulinzi na uaslama na kufanyikwa kukamata magunia matatu ya bangi, CD za mafunzo ya jihadi za kialshaababu pamoja na nguzo 35 za umeme mali ya shirika la umeme Tanesco.

Akitoa taarifa kwa waandishi wa habari jana Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa, ACP Ramadhani Mungi alisema polisi walifanya opresheni kusaka mambo yanayohusu makosa ya jinai na kufanyikwa kukamata maguni ya bangi pamoja na kukamatwa watuhumiwa sugu katika eneo ya njiapanda ya Tosamaganga.

WATOTO WAITAKA SERIKALI KUTUNGA SHERIA KALI ...

Na Friday Simbaya, Mufindi  Wanafunzi wa shule za msingi na sekondari wilayani Mufindi mkoani Iringa wameiomba serikali kwa kush...