Sunday, 19 September 2010

THE ELECTIONS ARE AROUND THE CORNER

Kombaini ya vyama saba vya upinzani Mjini Iringa vikifanya kampeni za uchaguzi kwa pamoja kama mbinu moja wapo ya kulitwa Jimbo la Iringa mjini, kama inavyoonekana gari kuwa na bendera ya vya mbalimabli kutundikwa ikielekea kwenye kampeni.






TANZANIA is going to general elections on October 31, 2010 and Elections are a process. It is important to bear in mind that what takes place on the polling day is a conclusion of struggles, campaigns and debates that have been going for quite some time.
Like a ‘Judgment Day’, the polling day is about decisions that have been long in the making. Even judging an election whether is free and fair or not, is not the matter of what happens on voting day, but what has been happening all along.
Obstacles to free and fair democratic elections
Among the most common obstacles are abject poverty, inequality, ignorance, electoral corruption, unethical polities, total despair, extremism, lack of courage, apathy, imposed political culture, discrimination, marginalization and political oppression.
1.       Electoral Corruption is a threat to free and fair elections because it leads to wrong choices of leaders and, eventually, to a government, central or local, that is corrupt.
2.       Poverty and Inequality- rich candidates might buy poor voters’ votes.
3.       Political Oppression –forcing people to vote for a candidate they would have otherwise not elected, as results are not free and fair.
4.       Apathy-non participation in election due to lack of provision of civic and voter education to people.
5.       Extremism- priorities are distorted and choices clouded.
6.       Discrimination and Marginalization-normally include people with handicaps, the physically challenged, and small indigenous groups such as hunter-gatherers.  

Thursday, 16 September 2010

MAMBO YA LIVYOKUWA KATIKA UZINDUZI WA DARAJA LA MOJA

Wakati wa jua kali na uchovu wa kazi baada ya uzinduzi wa Daraja la umoja linaloziunganisha nchi mbili za Tanzania na Msumbiji, Mtangazaji Maarufu wa TBC Taifa (zamani RTD), Bw. Malima Ndelema akipooza uso kwa maji ya Mto Ruvuma katika eneo la Mtambaswala upande wa Msumbiji hivi karibuni.

Daraja la Umoja linalounganisha nchi mbili za Tanzania na Msumbiji lenye urefu wa kilometa moja kasoro katika Mto Ruvuma eneo la Mtambaswala ni kivutio cha kipekee katika masuala mazima ya utalii na kukuza ushirikiano kati ya nchi hizi mbili.


 Ubovu wa miundombinu ya barabara katika maeneo mengi ya vijijini na mijini yanakwamisha maendeleo ya wananchi na nchi yao kiuchumi, eneo hili kama linavyoonekana mbele ya Mto Rufiji eneo la Nangulukulu  Wilaya ya Rufiji Mkoa wa Pwani ni kikwazo kikubwa cha wasafiri wa maeneo ya Kusini mwa Tanzania hasa wakati wa mvua. Msururu wa magari haya ni kielelezo tosha cha hali hiyo.

MTEMVU AWAONDOLEA WASIWASI WANANCHI

MGOMBEA kiti cha Ubunge Jimbo la Temeke kupitia tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM), Abasi Zuberi Mtemvu amewatoa wasiwasi wapangaji wa nyumba za kota zilizopo Temeke mwisho kwa kuwaeleza kuwa zoezi la kuvunjwa kwa nyumba hizo sasa limesitishwa.

Mgombea huyo alitoa kauli hiyo jana kwenye mkutano wa hadhara wa kampeni za uchaguzi uliyofanyika katika uwanja wa MjiMpya Kata ya Azimio jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa na umati wa watu.

Akifafanua zaidi kuhusu kauli yake hiyo Mtemvu alisema serikali iliyoko madarakani imejipanga kujenga majengo ya ghorofa katika eneo hilo ambapo ujenzi wake ukikamilika wapangaji wa awali wa kota watapewa umuhimu wa kwanza kufikiriwa katika kupanga kwenye maghorofa hayo.

Alisema si vyema kuanza zoezi la uvunjaji wa kota hizo bila kuzingatia usalama wa wananchi na mali zao katika kipindi cha mpango huo.

Kota hizo zilizopo eneo la Temeke mwisho zilijengwa miaka mingi iliyopita katika mfumo wa familia moja, mbili na tatu hata hivyo nyumba hizo zimeanza kuchoka na hata baadhi yake kuanza kuharibika.

Kwa upande mwingine mgombea huyo aliwataka wanawake wa jimbo hilo kujiunga pamoja na kuunda vikundi vidogo vidogo (VICOBA) ili waweze kupata misaada ya uwendelezaji wa vikundi vyao ili kuondokana na umasikini wa kipato na kuboresha familia zao.

Akizumgumzia huduma za jamii upande wa elimu alisema endapo atachaguliwa tena kuongoza jimbo hilo atahakikisha kuwa kata ya Azimio inapata sekondari ya kidato cha tana na sita.

Wednesday, 15 September 2010

ABASI MTEMVU


Bw. Abasi Zuberi Mtemvu Mgombea Mbunge katika Jimbo la Temeke kupitia tiketi ya CCM (mwenye mkono juu na vazi ya kijani la CCM katikati) akilakiwa na wanacchama na wananchi katika Mkutano wa Kampeni za Uchaguzi 2010 uliyofanuika Kata ya Azimio jijini Dar es Salaam.

MWANDISHI AVAA KHANGA YA CCM NA BAADAYE KUPANDA GARI LA MATANGAZO YA CHAMA HICHO NA KUTOKOMEA NALO----HABARI NDIYO HIYO!








Mwandishi wa habari ambaye akufahamika jina lake mara moja amekutwa akiwa amevaa Khanga ya Chama Cha Mapindizi (CCM) katika Mkutano wa Kampeni za Uchaguzi Mkuu 2010 uliyokuwa unahutubiwa na Mgombea Ubunge wa Jimbo la Temeke, Bw. Abasi Zuberi Mtemvu leo. Mkutano huo ulifanyika katika Uwanja wa MjiMpya-Tawi la Kichangani (CCM) Kata ya Azimio Wilaya ya Temeke jijini Dar es Salaam.

Tuesday, 14 September 2010

MAMBO YA PWANI


Wachuuzi wa samaki wakimuandaa samaki aina ya pweza katika soko la samaki Magogoni jijini Dar.

Residents of Dar es Salaam were enjoying a ride on the MV Magogoni in the Indian Ocean during the weekend going to Kigamboni.

USAILI WAANDISHI MATUMBO JOTO

Waandishi wa habari wakijisomea vijarida mbalimbali katika Ofisi ya Waandishi Mazingira (JET) jijini Dar es Salaam walipokuwa wakisubiri kuingia kwnye usaili ofisi hapa kwa ajili ya 'Exchange Programme' katika nchi za Ethiopia, Kenya, Uganda na Malawi jana.

MVULANA MPIKA VITUMBUA

UGUMU wa maisha na umaskini wa wazazi wa Adam Mussa (18) wampelekea kuwa mjasliamali wa kupika vitumbua Barabara ya Kawawa Kituo cha Moroco jijini Dar es Salaam.

ADHA YA USAFIRI DAR

ADHA  ya usafiri Dar es Salaam wanafunzi hawathaminiwi hii ilidhihirika jana katika Kituo cha daladala Mtoni Mtongani ambapo mwanafunzi huyu katika picha (watatu kutoka kulia) akionekana kushangaa wakati watu wazima wakigombea usafiri.

Sunday, 12 September 2010

ABOOD BUS SERVICE

Mafundi na abiria wa bus la Abood akisaidiana kutengenaza ekizoti paipi ya bus baada kukatika katika eneo la Igemi katikati ya Mahenge na Mtandika Wilaya ya Killolo mkoani Iringa jana majira ya saa 3 asubuhi. Bus la Abood lilianza safari kutoka Iringa Mjini kwenda Dar saa 1 asubuhi lakini lilipofika eneo la Igemi 'exhust pipe' ilichomoka na mafundi wa basi wakatengeza kidogo ndipo tulipofika Hoteli ya Aljazeera walilichomelea na tukaenedelea safari hadi Ubungo saa 9:30 hivi.

Foleni ya magari kama ilvyokutwa katika eneo la Igemi katika ya Mahenge na Mtandika wilayani Kilolo, Mkoa wa Iringa ya kisubiri kuruhusiwa na watengezaji wa barabara ya Tanzam.

WATOTO WAITAKA SERIKALI KUTUNGA SHERIA KALI ...

Na Friday Simbaya, Mufindi  Wanafunzi wa shule za msingi na sekondari wilayani Mufindi mkoani Iringa wameiomba serikali kwa kush...